Ayabu 19

Job Chapter 19

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
Then Job answered,
2
Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini, Na kunivunja-vunja kwa maneno?
"How long will you torment me, And crush me with words?
3
Mara kumi hizi mmenishutumu; Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu.
You have reproached me ten times. You aren't ashamed that you attack me.
4
Ingawaje nimekosa, Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe.
If it is true that I have erred, My error remains with myself.
5
Kwamba mtajitukuza juu yangu, Na kunena juu yangu shutumu langu;
If indeed you will magnify yourselves against me, And plead against me my reproach;
6
Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha, Na kunizingira kwa wavu wake.
Know now that God has subverted me, And has surrounded me with his net.
7
Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi; Naulilia msaada, wala hapana hukumu.
"Behold, I cry out of wrong, but I am not heard: I cry for help, but there is no justice.
8
Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu.
He has walled up my way so that I can't pass, And has set darkness in my paths.
9
Amenivua utukufu wangu, Na kuiondoa taji kichwani mwangu.
He has stripped me of my glory, And taken the crown from my head.
10
Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka; Na tumaini langu ameling'oa kama mti.
He has broken me down on every side, and I am gone. My hope he has plucked up like a tree.
11
Tena ameziwasha ghadhabu zake juu yangu, Akanihesabia kuwa mmoja katika watesi wake.
He has also kindled his wrath against me. He counts me among his adversaries.
12
Majeshi yake husongea pamoja, na kunipandishia njia yao, Na kupiga marago kuizunguka hema yangu.
His troops come on together, Build a siege ramp against me, And encamp around my tent.
13
Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa.
"He has put my brothers far from me. My acquaintances are wholly estranged from me.
14
Watu wa mbari yangu wamekoma, Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau.
My relatives have gone away. My familiar friends have forgotten me.
15
Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni; Mimi ni mgeni machoni pao.
Those who dwell in my house, and my maids, count me for a stranger. I am an alien in their sight.
16
Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii, Ingawa namsihi kwa kinywa changu.
I call to my servant, and he gives me no answer; I beg him with my mouth.
17
Pumzi zangu ni kama za mgeni kwa mke wangu, Nami ni machukizo kwa ndugu zangu.
My breath is offensive to my wife. I am loathsome to the children of my own mother.
18
Hata watoto wadogo hunidharau; Nikiondoka, huninena.
Even young children despise me. If I arise, they speak against me.
19
Wasiri wangu wote wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia.
All my familiar friends abhor me. They whom I loved have turned against me.
20
Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu, Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu.
My bones stick to my skin and to my flesh. I have escaped by the skin of my teeth.
21
Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.
"Have pity on me, have pity on me, you my friends; For the hand of God has touched me.
22
Mbona ninyi mnaniudhi kama Mungu, Wala hamkutosheka na nyama yangu?
Why do you persecute me as God, And are not satisfied with my flesh?
23
Laiti maneno yangu yangeandikwa sasa! Laiti yangeandikwa kitabuni!
"Oh that my words were now written! Oh that they were inscribed in a book!
24
Yakachorwa katika mwamba milele, Kwa kalamu ya chuma na risasi.
That with an iron pen and lead They were engraved in the rock forever!
25
Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
But as for me, I know that my Redeemer lives. In the end, he will stand upon the earth.
26
Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;
After my skin is destroyed, Then in my flesh shall I see God,
27
Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu.
Whom I, even I, shall see on my side. My eyes shall see, and not as a stranger. "My heart is consumed within me.
28
Kama mkisema, Jinsi tutakavyomwudhi! Kwa kuwa shina la jambo hili limeonekana kwake;
If you say, 'How we will persecute him!' Because the root of the matter is found in me,
29
Uogopeni upanga; Kwa maana adhabu za upanga zina ghadhabu, Mpate kujua ya kwamba hukumu iko.
Be afraid of the sword, For wrath brings the punishments of the sword, That you may know there is a judgment."
« 18 20 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)