Ayabu 11 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ayabu 11 (Swahili) Job 11 (English)

Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu, na kusema, Ayabu 11:1

Then Zophar, the Naamathite, answered,

Je! Huu wingi wa maneno usijibiwe? Na mtu aliyejaa maneno, je! Ahesabiwe kuwa na haki? Ayabu 11:2

"Shouldn't the multitude of words be answered? Should a man full of talk be justified?

Je! Majivuno yako yawanyamazishe watu wawe kimya? Nawe hapo ufanyapo dhihaka, je! Hapana mtu atakayekutahayarisha? Ayabu 11:3

Should your boastings make men hold their peace? When you mock, shall no man make you ashamed?

Kwa kuwa wewe wasema, Mafunzo yangu ni safi, Nami ni safi machoni pako. Ayabu 11:4

For you say, 'My doctrine is pure, I am clean in your eyes.'

Lakini, laiti Mungu angenena, Na kuifunua midomo yake juu yako; Ayabu 11:5

But oh that God would speak, And open his lips against you,

Tena akuonyeshe hizo siri za hekima, Ya kuwa hufanikiwa katika kuyatimiza makusudi yake! Ujue basi ya kuwa Mungu akuachilia katika uovu wako. Ayabu 11:6

That he would show you the secrets of wisdom! For true wisdom has two sides. Know therefore that God exacts of you less than your iniquity deserves.

Je! Wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu? Waweza kuufikilia upeo wa huyo Mwenyezi? Ayabu 11:7

"Can you fathom the mystery of God? Or can you probe the limits of the Almighty?

Ni juu mno kama mbingu; waweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kuliko kuzimuni; waweza kujua nini wewe? Ayabu 11:8

They are high as heaven. What can you do? Deeper than Sheol: what can you know?

Cheo chake ni kirefu kuliko dunia, Ni kipana zaidi ya bahari. Ayabu 11:9

The measure of it is longer than the earth, And broader than the sea.

Yeye akipita, na kufunga watu, Na kuwaita hukumuni, ni nani basi awezaye kumzuia? Ayabu 11:10

If he passes by, or confines, Or convenes a court, then who can oppose him?

Kwani yeye awajua watu baradhuli; Huona na uovu pia, hata asipoufikiri. Ayabu 11:11

For he knows false men. He sees iniquity also, even though he doesn't consider it.

Lakini mpumbavu aweza kupata ufahamu, Ingawa mwanadamu huzaliwa kama mtoto wa punda-mwitu. Ayabu 11:12

But vain man can become wise If a man can be born as a wild donkey's colt.

Wewe ukiuweka moyo wako kwa uelekevu, Na kumnyoshea mikono yako; Ayabu 11:13

"If you set your heart aright, Stretch out your hands toward him.

Ikiwa una uovu mkononi mwako, uweke mbali nawe, Wala usikubali upuzi kukaa hemani mwako; Ayabu 11:14

If iniquity is in your hand, put it far away, Don't let unrighteousness dwell in your tents.

Hakika ndipo utakapopata kuinua uso pasipo ila; Naam, utathibitika, wala hutakuwa na hofu; Ayabu 11:15

Surely then shall you lift up your face without spot; Yes, you shall be steadfast, and shall not fear:

Kwa kuwa utasahau mashaka yako; Utayakumbuka kama maji yaliyokwisha pita; Ayabu 11:16

For you shall forget your misery; You shall remember it as waters that are passed away,

Na maisha yako yatakuwa meupe kuliko adhuhuri; Lijapokuwa ni giza, litakuwa kama alfajiri. Ayabu 11:17

Life shall be clearer than the noonday; Though there is darkness, it shall be as the morning.

Nawe utakuwa salama, kwa sababu kuna matumaini; Naam, utatafuta-tafuta kando yako, na kupumzika katika salama. Ayabu 11:18

You shall be secure, because there is hope; Yes, you shall search, and shall take your rest in safety.

Tena utalala, wala hapana atakayekutia hofu; Naam, wengi watakutafuta uso wako. Ayabu 11:19

Also you shall lie down, and none shall make you afraid; Yes, many shall court your favor.

Lakini macho ya waovu yataingia kiwi, Nao hawatakuwa na njia ya kukimbilia, Na matumaini yao yatakuwa ni kutoa roho. Ayabu 11:20

But the eyes of the wicked shall fail, They shall have no way to flee; Their hope shall be the giving up of the spirit."