Ayabu 30 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 30 (Swahili) | Job 30 (English) |
---|---|
Lakini sasa hao walio wadogo wangu hunifanyia mzaha, Ambao baba zao niliwadharau hata kuwaweka na mbwa wa kundi langu. Ayabu 30:1 |
"But now those who are younger than I, have me in derision, Whose fathers I would have disdained to put with my sheep dogs. |
Naam, uwezo wa mikono yao utanifaa nini? Watu ambao nguvu zao zimekoma. Ayabu 30:2 |
Of what use is the strength of their hands to me, Men in whom ripe age has perished? |
Wamekonda kwa uhitaji na njaa; Huguguna nchi kavu, penye giza la ukiwa na uharibifu. Ayabu 30:3 |
They are gaunt from lack and famine. They gnaw the dry ground, in the gloom of waste and desolation. |
Hung'oa mboga ya chumvi kwenye kichaka; Na mizizi ya mretemu ni chakula chao. Ayabu 30:4 |
They pluck salt herbs by the bushes. The roots of the broom are their food. |
Hufukuzwa watoke kati ya watu; Huwapigia kelele kama kumpigia mwivi. Ayabu 30:5 |
They are driven forth from the midst of men; They cry after them as after a thief; |
Lazima hukaa katika mianya ya mabonde, Katika mashimo ya nchi na ya majabali. Ayabu 30:6 |
So that they dwell in frightful valleys, And in holes of the earth and of the rocks. |
Hulia kama punda vichakani; Hukusanyika chini ya upupu. Ayabu 30:7 |
Among the bushes they bray; And under the nettles they are gathered together. |
Wao ni wana wa wapumbavu, naam, watoto wa wahuni; Walifukuzwa kwa mijeledi watoke katika nchi. Ayabu 30:8 |
They are children of fools, yes, children of base men. They were flogged out of the land. |
Na sasa mimi nimekuwa wimbo wao, Naam, nimekuwa simo kwao. Ayabu 30:9 |
"Now I have become their song. Yes, I am a byword to them. |
Wao hunichukia, na kujitenga nami, Hawaachi kunitemea mate usoni. Ayabu 30:10 |
They abhor me, they stand aloof from me, And don't hesitate to spit in my face. |
Kwani ameilegeza kamba yake, na kunitesa, Wala hawajizuii tena mbele yangu. Ayabu 30:11 |
For he has untied his cord, and afflicted me; And they have thrown off restraint before me. |
Kwa mkono wangu wa kuume huinuka kundi; Huisukuma miguu yangu kando, Na kunipandishia njia zao za uharibifu. Ayabu 30:12 |
On my right hand rise the rabble. They thrust aside my feet, They cast up against me their ways of destruction. |
Waiharibu njia yangu, Wauzidisha msiba wangu, Watu wasio na msaidizi. Ayabu 30:13 |
They mar my path, They set forward my calamity, Without anyone's help. |
Wanijilia kama wapitao katika ufa mpana; Katikati ya magofu wanishambulia. Ayabu 30:14 |
As through a wide breach they come, In the midst of the ruin they roll themselves in. |
Vitisho vimenigeukia; Huifukuza heshima yangu kama upepo; Na kufanikiwa kwangu kumepita kama wingu. Ayabu 30:15 |
Terrors are turned on me. They chase my honor as the wind. My welfare has passed away as a cloud. |
Sasa nafsi yangu inamwagika ndani yangu; Siku za mateso zimenishika. Ayabu 30:16 |
"Now my soul is poured out within me. Days of affliction have taken hold on me. |
Wakati wa usiku mifupa yangu huchomeka ndani yangu, Na maumivu yanayonitafuna hayapumziki. Ayabu 30:17 |
In the night season my bones are pierced in me, And the pains that gnaw me take no rest. |
Kwa ugonjwa wangu kuwa na nguvu nyingi Mavazi yangu yameharibika; Hunikaza kama shingo ya kanzu yangu. Ayabu 30:18 |
By great force is my garment disfigured. It binds me about as the collar of my coat. |
Yeye amenibwaga topeni, Nami nimekuwa kama mavumbi na majivu. Ayabu 30:19 |
He has cast me into the mire. I have become like dust and ashes. |
Nakulilia wewe, wala huniitikii; Nasimama, nawe wanitazama tu. Ayabu 30:20 |
I cry to you, and you do not answer me. I stand up, and you gaze at me. |
Wewe umegeuka kuwa mkali kwangu; Nawe waniudhi kwa uweza wa mkono wako. Ayabu 30:21 |
You have turned to be cruel to me. With the might of your hand you persecute me. |
Waniinua juu hata upeponi, na kunipandisha juu yake; Nawe waniyeyusha katika dhoruba. Ayabu 30:22 |
You lift me up to the wind, and drive me with it. You dissolve me in the storm. |
Kwani najua kuwa utanileta hata kifoni, Niifikilie nyumba waliyoandikiwa wenye uhai wote. Ayabu 30:23 |
For I know that you will bring me to death, To the house appointed for all living. |
Je! Mtu katika kuanguka kwake hanyoshi mkono? Na kulilia msaada katika msiba wake? Ayabu 30:24 |
"However doesn't one stretch out a hand in his fall? Or in his calamity therefore cry for help? |
Je! Mimi sikulia kwa ajili ya huyo aliyekuwa katika taabu? Nafsi yangu, je! Haikusononeka kwa ajili ya wahitaji? Ayabu 30:25 |
Didn't I weep for him who was in trouble? Wasn't my soul grieved for the needy? |
Hapo nilipotazamia mema, ndipo yakaja mabaya; Nami nilipongojea mwanga, likaja giza. Ayabu 30:26 |
When I looked for good, then evil came; When I waited for light, there came darkness. |
Matumbo yangu yatokota, wala hayaachi; Siku za taabu zimenijilia. Ayabu 30:27 |
My heart is troubled, and doesn't rest. Days of affliction have come on me. |
Naenda nikiomboleza pasipo jua; Nasimama katika mkutano, na kuulilia msaada. Ayabu 30:28 |
I go mourning without the sun. I stand up in the assembly, and cry for help. |
Mimi ni ndugu yao mbwa-mwitu, Ni mwenzao mbuni. Ayabu 30:29 |
I am a brother to jackals, And a companion to ostriches. |
Ngozi yangu ni nyeusi, nayo yanitoka, Na mifupa yangu imeteketea kwa hari. Ayabu 30:30 |
My skin grows black and peels from me. My bones are burned with heat. |
Kwa hiyo kinanda changu kimegeuzwa kuwa maombolezo, Na filimbi yangu kuwa sauti yao waliao. Ayabu 30:31 |
Therefore is my harp turned to mourning, And my pipe into the voice of those who weep. |