Ayabu 35 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 35 (Swahili) | Job 35 (English) |
---|---|
Tena Elihu akajibu na kusema, Ayabu 35:1 |
Moreover Elihu answered, |
Je! Wewe wadhani kwamba haya ni haki yako, Au je! Wasema, Haki yangu ni zaidi kuliko ya Mungu, Ayabu 35:2 |
"Do you think this to be your right, Or do you say, 'My righteousness is more than God's,' |
Maana wasema, Kutakuwa na faida gani kwako wewe? Tena, Nitapata faida gani, kuliko nikifanya dhambi? Ayabu 35:3 |
That you ask, 'What advantage will it be to you? What profit shall I have, more than if I had sinned?' |
Mimi nitakujibu, Na hawa wenzio pamoja nawe. Ayabu 35:4 |
I will answer you, And your companions with you. |
Ziangalie mbingu ukaone; Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe. Ayabu 35:5 |
Look to the heavens, and see. See the skies, which are higher than you. |
Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye? Ayabu 35:6 |
If you have sinned, what effect do you have against him? If your transgressions are multiplied, what do you do to him? |
Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako? Ayabu 35:7 |
If you are righteous, what do you give him? Or what does he receive from your hand? |
Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu. Ayabu 35:8 |
Your wickedness may hurt a man as you are; And your righteousness may profit a son of man. |
Kwa sababu ya wingi wa jeuri wao hulia; Walilia msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu. Ayabu 35:9 |
"By reason of the multitude of oppressions they cry out; They cry for help by reason of the arm of the mighty. |
Wala hapana asemaye, Yuko wapi Mungu Muumba wangu, Awapaye nyimbo wakati wa usiku; Ayabu 35:10 |
But none says, 'Where is God my Maker, Who gives songs in the night, |
Atufundishaye zaidi ya hayawani wa nchi, Na kutufanya wenye hekima kuliko ndege za angani? Ayabu 35:11 |
Who teaches us more than the animals of the earth, And makes us wiser than the birds of the sky?' |
Hulia huko, lakini hapana ajibuye, Kwa sababu ya kiburi cha watu waovu. Ayabu 35:12 |
There they cry, but none gives answer, Because of the pride of evil men. |
Hakika Mungu hatasikia ubatili, Wala Mwenyezi hatauangalia. Ayabu 35:13 |
Surely God will not hear an empty cry, Neither will the Almighty regard it. |
Sembuse usemapo wewe ya kuwa humwangalii, Hiyo daawa i mbele yake, nawe wamngojea! Ayabu 35:14 |
How much less when you say you don't see him. The cause is before him, and you wait for him! |
Lakini sasa, kwa sababu yeye hakukujilia katika hasira zake, Wala hauangalii sana unyeti; Ayabu 35:15 |
But now, because he has not visited in his anger, Neither does he greatly regard arrogance. |
Ndiposa Ayubu hufunua kinywa chake kwa ubatili; Huongeza maneno pasipo maarifa. Ayabu 35:16 |
Therefore Job opens his mouth with empty talk, And he multiplies words without knowledge." |