Ayabu 3 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 3 (Swahili) | Job 3 (English) |
---|---|
Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake. Ayabu 3:1 |
After this Job opened his mouth, and cursed the day of his birth. |
Ayubu akajibu, na kusema; Ayabu 3:2 |
Job answered: |
Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba. Ayabu 3:3 |
"Let the day perish in which I was born, The night which said, 'There is a man-child conceived.' |
Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie. Ayabu 3:4 |
Let that day be darkness; Don't let God from above seek for it, Neither let the light shine on it. |
Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe. Ayabu 3:5 |
Let darkness and the shadow of death claim it for their own. Let a cloud dwell on it. Let all that makes black the day terrify it. |
Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi. Ayabu 3:6 |
As for that night, let thick darkness seize on it. Let it not rejoice among the days of the year. Let it not come into the number of the months. |
Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe. Ayabu 3:7 |
Behold, let that night be barren. Let no joyful voice come therein. |
Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani. Ayabu 3:8 |
Let them curse it who curse the day, Who are ready to rouse up leviathan. |
Nyota za mapambazuko yake na ziwe giza; Na utafute mwanga lakini usiupate; Wala usiyaone makope ya asubuhi; Ayabu 3:9 |
Let the stars of the twilight of it be dark. Let it look for light, but have none, Neither let it see the eyelids of the morning, |
Kwa sababu haukuifunga milango ya tumbo la mamangu. Wala kunifichia taabu machoni. Ayabu 3:10 |
Because it didn't shut up the doors of my mother's womb, Nor did it hide trouble from my eyes. |
Mbona si kufa mimi tokea mimbani? Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni? Ayabu 3:11 |
"Why didn't I die from the womb? Why didn't I give up the spirit when my mother bore me? |
Mbona hayo magoti kunipokea? Au hayo maziwa, hata nikanyonya? Ayabu 3:12 |
Why did the knees receive me? Or why the breast, that I should suck? |
Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika; Ayabu 3:13 |
For now should I have lain down and been quiet. I should have slept, then I would have been at rest, |
Pamoja na wafalme na washauri wa dunia, Hao waliojijengea maganjoni; Ayabu 3:14 |
With kings and counselors of the earth, Who built up waste places for themselves; |
Au pamoja na wakuu wenye dhahabu, Waliozijaza fedha nyumba zao; Ayabu 3:15 |
Or with princes who had gold, Who filled their houses with silver: |
Au, kama kuzikwa mimba iliyoharibika, nisingekuwako; Kama wachanga wasiouona mwanga kabisa. Ayabu 3:16 |
Or as a hidden untimely birth I had not been, As infants who never saw light. |
Huko waovu huacha kusumbua; Huko nako hao waliochoka wapumzika Ayabu 3:17 |
There the wicked cease from troubling; There the weary are at rest. |
Huko wafungwa waona raha pamoja; Hawaisikii sauti yake msimamizi. Ayabu 3:18 |
There the prisoners are at ease together. They don't hear the voice of the taskmaster. |
Wakuu na wadogo wako huko; Mtumishi yu huru kwa bwana wake. Ayabu 3:19 |
The small and the great are there. The servant is free from his master. |
Mbona yeye aliye mashakani kupewa mwanga, Na hao wenye uchungu rohoni kupewa uhai; Ayabu 3:20 |
"Why is light given to him who is in misery, Life to the bitter in soul, |
Ambao wangojea mauti, lakini hawayapati; Na kuyachimbulia zaidi ya kutafuta hazina iliyostirika; Ayabu 3:21 |
Who long for death, but it doesn't come; Dig for it more than for hidden treasures, |
Ambao wafurahi mno, Na kushangilia watakapoliona kaburi? Ayabu 3:22 |
Who rejoice exceedingly, Are glad, when they can find the grave? |
Kwa nini mtu aliyezibiwa njia kupewa mwanga, Ambaye Mungu amemzingira kwa ukingo? Ayabu 3:23 |
Why is light given to a man whose way is hid, Whom God has hedged in? |
Kwani kuugua kwangu kwaja kana kwamba ni chakula, Na kunguruma kwangu kumemiminika kama maji. Ayabu 3:24 |
For my sighing comes before I eat, My groanings are poured out like water. |
Maana jambo hilo nichalo hunipata, Nalo linitialo hofu hunijilia. Ayabu 3:25 |
For the thing which I fear comes on me, That which I am afraid of comes to me. |
Mimi sioni raha, wala situlii, wala kupumzika; Lakini huja taabu. Ayabu 3:26 |
I am not at ease, neither am I quiet, neither have I rest; But trouble comes." |