Ayabu 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ayabu 3 (Swahili) Job 3 (English)

Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake. Ayabu 3:1

After this Job opened his mouth, and cursed the day of his birth.

Ayubu akajibu, na kusema; Ayabu 3:2

Job answered:

Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba. Ayabu 3:3

"Let the day perish in which I was born, The night which said, 'There is a man-child conceived.'

Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie. Ayabu 3:4

Let that day be darkness; Don't let God from above seek for it, Neither let the light shine on it.

Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe. Ayabu 3:5

Let darkness and the shadow of death claim it for their own. Let a cloud dwell on it. Let all that makes black the day terrify it.

Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi. Ayabu 3:6

As for that night, let thick darkness seize on it. Let it not rejoice among the days of the year. Let it not come into the number of the months.

Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe. Ayabu 3:7

Behold, let that night be barren. Let no joyful voice come therein.

Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani. Ayabu 3:8

Let them curse it who curse the day, Who are ready to rouse up leviathan.

Nyota za mapambazuko yake na ziwe giza; Na utafute mwanga lakini usiupate; Wala usiyaone makope ya asubuhi; Ayabu 3:9

Let the stars of the twilight of it be dark. Let it look for light, but have none, Neither let it see the eyelids of the morning,

Kwa sababu haukuifunga milango ya tumbo la mamangu. Wala kunifichia taabu machoni. Ayabu 3:10

Because it didn't shut up the doors of my mother's womb, Nor did it hide trouble from my eyes.

Mbona si kufa mimi tokea mimbani? Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni? Ayabu 3:11

"Why didn't I die from the womb? Why didn't I give up the spirit when my mother bore me?

Mbona hayo magoti kunipokea? Au hayo maziwa, hata nikanyonya? Ayabu 3:12

Why did the knees receive me? Or why the breast, that I should suck?

Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika; Ayabu 3:13

For now should I have lain down and been quiet. I should have slept, then I would have been at rest,

Pamoja na wafalme na washauri wa dunia, Hao waliojijengea maganjoni; Ayabu 3:14

With kings and counselors of the earth, Who built up waste places for themselves;

Au pamoja na wakuu wenye dhahabu, Waliozijaza fedha nyumba zao; Ayabu 3:15

Or with princes who had gold, Who filled their houses with silver:

Au, kama kuzikwa mimba iliyoharibika, nisingekuwako; Kama wachanga wasiouona mwanga kabisa. Ayabu 3:16

Or as a hidden untimely birth I had not been, As infants who never saw light.

Huko waovu huacha kusumbua; Huko nako hao waliochoka wapumzika Ayabu 3:17

There the wicked cease from troubling; There the weary are at rest.

Huko wafungwa waona raha pamoja; Hawaisikii sauti yake msimamizi. Ayabu 3:18

There the prisoners are at ease together. They don't hear the voice of the taskmaster.

Wakuu na wadogo wako huko; Mtumishi yu huru kwa bwana wake. Ayabu 3:19

The small and the great are there. The servant is free from his master.

Mbona yeye aliye mashakani kupewa mwanga, Na hao wenye uchungu rohoni kupewa uhai; Ayabu 3:20

"Why is light given to him who is in misery, Life to the bitter in soul,

Ambao wangojea mauti, lakini hawayapati; Na kuyachimbulia zaidi ya kutafuta hazina iliyostirika; Ayabu 3:21

Who long for death, but it doesn't come; Dig for it more than for hidden treasures,

Ambao wafurahi mno, Na kushangilia watakapoliona kaburi? Ayabu 3:22

Who rejoice exceedingly, Are glad, when they can find the grave?

Kwa nini mtu aliyezibiwa njia kupewa mwanga, Ambaye Mungu amemzingira kwa ukingo? Ayabu 3:23

Why is light given to a man whose way is hid, Whom God has hedged in?

Kwani kuugua kwangu kwaja kana kwamba ni chakula, Na kunguruma kwangu kumemiminika kama maji. Ayabu 3:24

For my sighing comes before I eat, My groanings are poured out like water.

Maana jambo hilo nichalo hunipata, Nalo linitialo hofu hunijilia. Ayabu 3:25

For the thing which I fear comes on me, That which I am afraid of comes to me.

Mimi sioni raha, wala situlii, wala kupumzika; Lakini huja taabu. Ayabu 3:26

I am not at ease, neither am I quiet, neither have I rest; But trouble comes."