Ayabu 9 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 9 (Swahili) | Job 9 (English) |
---|---|
Ndipo Ayubu akajibu, na kusema, Ayabu 9:1 |
Then Job answered, |
Kweli najua kuwa ndivyo hivyo; Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu? Ayabu 9:2 |
"Truly I know that it is so, But how can man be just with God? |
Kama akipenda kushindana naye, Hawezi kumjibu neno moja katika elfu. Ayabu 9:3 |
If he is pleased to contend with him, He can't answer him one time in a thousand. |
Yeye ni mwenye hekima moyoni, na mwenye uwezo katika nguvu; Ni nani aliyejifanya kuwa mgumu juu yake, naye akafanikiwa? Ayabu 9:4 |
God who is wise in heart, and mighty in strength: Who has hardened himself against him, and prospered? |
Aiondoaye milima, nayo haina habari, Akiipindua katika hasira zake. Ayabu 9:5 |
Who removes the mountains, and they don't know it, When he overturns them in his anger |
Aitikisaye dunia itoke mahali pake, Na nguzo zake hutetema. Ayabu 9:6 |
Who shakes the earth out of its place; The pillars of it tremble; |
Aliamuruye jua, nalo halichomozi; Nazo nyota huzipiga muhuri. Ayabu 9:7 |
Who commands the sun, and it doesn't rise, And seals up the stars; |
Ambaye peke yake ni mwenye kuzitandika mbingu, Na kuyakanyaga mawimbi ya bahari. Ayabu 9:8 |
Who alone stretches out the heavens, Treads on the waves of the sea; |
Yeye afanyaye hizo nyota za Dubu, na Orioni, na hicho Kilimia, Na makundi ya nyota ya kusini. Ayabu 9:9 |
Who makes the Bear, Orion, and the Pleiades, And the chambers of the south; |
Atendaye mambo makuu yasiyotafutikana; Naam, mambo ya ajabu yasiyohesabika. Ayabu 9:10 |
Who does great things past finding out, Yes, marvelous things without number. |
Tazama, yuaenenda karibu nami, nisimwone; Tena yuapita kwenda mbele, nisimtambue. Ayabu 9:11 |
Behold, he goes by me, and I don't see him. He passes on also, but I don't perceive him. |
Tazama, yuakamata, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwuliza, Wafanya nini? Ayabu 9:12 |
Behold, he snatches away; who can hinder him? Who will ask him, 'What are you doing?' |
Mungu haondoi hasira zake; Hao wamsaidiao Rahabu huinama chini yake. Ayabu 9:13 |
"God will not withdraw his anger; The helpers of Rahab stoop under him. |
Je! Mimi nitamjibuje, Na kuyachagua maneno yangu kuhojiana naye? Ayabu 9:14 |
How much less shall I answer him, Choose my words to argue with him? |
Ambaye, nijapokuwa mimi ni mwenye haki, nisingemjibu; Ningemsihi-sihi mtesi wangu. Ayabu 9:15 |
Whom, though I were righteous, yet would I not answer. I would make supplication to my judge. |
Kama ningemwita, naye akaniitikia; Hata hivyo singeamini kuwa amesikiza sauti yangu. Ayabu 9:16 |
If I had called, and he had answered me, Yet would I not believe that he listened to my voice. |
Yeye anipondaye kwa dhoruba, Na kuziongeza jeraha zangu pasipokuwa na sababu. Ayabu 9:17 |
For he breaks me with a tempest, Multiplies my wounds without cause. |
Haniachi nipate kuvuta pumzi, Lakini hunijaza uchungu. Ayabu 9:18 |
He will not allow me to take my breath, But fills me with bitterness. |
Kama tukitaja nguvu za mashujaa, tazama yupo hapo! Kama tukitaja hukumu, ni nani atakayeniwekea muhula? Ayabu 9:19 |
If it is a matter of strength, behold, he is mighty! If of justice, 'Who,' says he, 'will summon me?' |
Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; Ingawa ni mkamilifu, kitanishuhudia kuwa ni mpotovu. Ayabu 9:20 |
Though I am righteous, my own mouth shall condemn me. Though I am blameless, it shall prove me perverse. |
Mimi ni mkamilifu; siangalii nafsi yangu; Naudharau uhai wangu. Ayabu 9:21 |
I am blameless. I don't regard myself. I despise my life. |
Hayo yote ni mamoja; kwa hiyo nasema, Yeye huangamiza wakamilifu na waovu pia. Ayabu 9:22 |
"It is all the same. Therefore I say, He destroys the blameless and the wicked. |
Kama hilo pigo likiua ghafula, Atayadhihaki majaribu yake asiye na kosa. Ayabu 9:23 |
If the scourge kills suddenly, He will mock at the trial of the innocent. |
Dunia imetiwa mkononi mwa waovu; Yeye hufunika nyuso za waamuzi wake; Kama si yeye, ni nani basi? Ayabu 9:24 |
The earth is given into the hand of the wicked. He covers the faces of the judges of it. If not he, then who is it? |
Basi siku zangu zina mbio kuliko tarishi; Zakimbia, wala hazioni mema. Ayabu 9:25 |
"Now my days are swifter than a runner. They flee away, they see no good, |
Zimepita kama merikebu ziendazo mbio; Mfano wa tai ayashukiaye mawindo. Ayabu 9:26 |
They have passed away as the swift ships, As the eagle that swoops on the prey. |
Nikisema, Mimi nitasahau kuugua kwangu, Nitaacha kununa uso nikachangamke moyo; Ayabu 9:27 |
If I say, 'I will forget my complaint, I will put off my sad face, and cheer up;' |
Mimi huziogopa huzuni zangu zote, Najua kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia. Ayabu 9:28 |
I am afraid of all my sorrows, I know that you will not hold me innocent. |
Nitahukumiwa kuwa ni mkosa; Ya nini basi nitaabike bure? Ayabu 9:29 |
I shall be condemned; Why then do I labor in vain? |
Ingawaje najiosha kwa maji ya theluji, Na kuitakasa mikono yangu kwa sabuni; Ayabu 9:30 |
If I wash myself with snow, And cleanse my hands with lye, |
Lakini utanitupa shimoni, Nami hata nguo zangu zitanichukia. Ayabu 9:31 |
Yet you will plunge me in the ditch. My own clothes shall abhor me. |
Kwani yeye si mtu, kama mimi, hata nimjibu, Hata tukaribiane katika hukumu. Ayabu 9:32 |
For he is not a man, as I am, that I should answer him, That we should come together in judgment. |
Hapana mwenye kuamua katikati yetu, Awezaye kutuwekea mkono sote wawili. Ayabu 9:33 |
There is no umpire between us, That might lay his hand on us both. |
Na aniondolee fimbo yake, Na utisho wake usinitie hofu; Ayabu 9:34 |
Let him take his rod away from me, Let his terror not make me afraid: |
Ndipo hapo ningesema, nisimwogope; Kwani sivyo nilivyo nafsini mwangu. Ayabu 9:35 |
Then I would speak, and not fear him, For I am not so in myself. |