Isaya 65 Swahili & English
Listen/Download AudioIsaya 65 (Swahili) | Isaiah 65 (English) |
---|---|
Watu wasionitaka wanauliza habari zangu; nimeonekana na hao wasionitafuta; naliliambia taifa lisiloitwa kwa jina langu, Isaya 65:1 |
I am inquired of by those who didn't ask; I am found by those who didn't seek me: I said, See me, see me, to a nation that was not called by my name. |
Nitazameni, nitazameni. Mchana kutwa nimewanyoshea mikono yangu watu walioasi, watu waendao katika njia isiyo njema, wakifuata mawazo yao wenyewe; Isaya 65:2 |
I have spread out my hands all the day to a rebellious people, who walk in a way that is not good, after their own thoughts; |
watu wanikasirishao mbele za uso wangu daima, wakitoa dhabihu katika bustani zao, na kufukiza uvumba juu ya matofali; Isaya 65:3 |
a people who provoke me to my face continually, sacrificing in gardens, and burning incense on bricks; |
waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao; Isaya 65:4 |
who sit among the graves, and lodge in the secret places; who eat pig's flesh, and broth of abominable things is in their vessels; |
watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe; watu hao ni moshi puani mwangu, moto uwakao mchana kutwa. Isaya 65:5 |
who say, Stand by yourself, don't come near to me, for I am holier than you. These are a smoke in my nose, a fire that burns all the day. |
Tazama, neno hili limeandikwa mbele zangu. Sitanyamaza, lakini nitalipa, naam, mimi nitawalipa ujira wao vifuani mwao; Isaya 65:6 |
Behold, it is written before me: I will not keep silence, but will recompense, yes, I will recompense into their bosom, |
maovu yenu na maovu ya baba zenu pamoja, asema Bwana, ninyi mliofukiza uvumba juu ya milima, na kunitukana juu ya vilima; basi, kwa ajili ya hayo nitawapimia kwanza kazi yao vifuani mwao. Isaya 65:7 |
your own iniquities, and the iniquities of your fathers together, says Yahweh, who have burned incense on the mountains, and blasphemed me on the hills; therefore will I first measure their work into their bosom. |
Bwana asema hivi, Kama vile divai mpya ipatikanavyo katika kichala, na mtu mmoja husema, Usikiharibu kwa maana mna baraka ndani yake; ndivyo nitakavyotenda kwa ajili ya watumishi wangu, ili nisiwaharibu wote. Isaya 65:8 |
Thus says Yahweh, As the new wine is found in the cluster, and one says, Don't destroy it, for a blessing is in it: so will I do for my servants' sake, that I may not destroy them all. |
Nami nitaleta uzao toka Yakobo, na mrithi wa milima yangu toka Yuda, na mteule wangu atairithi, na watumishi wangu watakaa huko. Isaya 65:9 |
I will bring forth a seed out of Jacob, and out of Judah an inheritor of my mountains; and my chosen shall inherit it, and my servants shall dwell there. |
Na Sharoni itakuwa zizi la makundi ya kondoo, na bonde la Akori mahali pa kulala makundi ya ng'ombe, kwa ajili ya watu wangu walionitafuta. Isaya 65:10 |
Sharon shall be a fold of flocks, and the valley of Achor a place for herds to lie down in, for my people who have sought me. |
Bali ninyi mmwachao Bwana, na kuusahau mlima wangu mtakatifu, na kuandika meza kwa ajili ya Bahati, na kuijazia Ajali vyombo vya divai iliyochanganyika; Isaya 65:11 |
But you who forsake Yahweh, who forget my holy mountain, who prepare a table for Fortune, and who fill up mixed wine to Destiny; |
mimi nitawaandikia kuuawa kwa upanga, na ninyi nyote mtainama ili kuchinjwa; kwa sababu nilipoita hamkuitika; niliponena, hamkusikia; bali mlitenda yaliyo mabaya machoni pangu, mlichagua mambo nisiyoyafurahia. Isaya 65:12 |
I will destine you to the sword, and you shall all bow down to the slaughter; because when I called, you did not answer; when I spoke, you did not hear; but you did that which was evil in my eyes, and chose that in which I didn't delight. |
Kwa hiyo Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi, bali ninyi mtatahayarika; Isaya 65:13 |
Therefore thus says the Lord Yahweh, Behold, my servants shall eat, but you shall be hungry; behold, my servants shall drink, but you shall be thirsty; behold, my servants shall rejoice, but you shall be disappointed; |
tazama, watumishi wangu wataimba kwa furaha ya moyo, bali ninyi mtalia kwa huzuni ya moyo; mtapiga kelele kwa sababu ya uchungu wa roho zenu. Isaya 65:14 |
behold, my servants shall sing for joy of heart, but you shall cry for sorrow of heart, and shall wail for vexation of spirit. |
Nanyi mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa wateule wangu. Na Bwana MUNGU atakuua; naye atawaita watumishi wake kwa jina lingine. Isaya 65:15 |
You shall leave your name for a curse to my chosen; and the Lord Yahweh will kill you; and he will call his servants by another name: |
Hata itakuwa yeye atakayejibariki duniani, atajibariki kwa Mungu wa kweli; naye atakayeapa duniani, ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za kwanza zimesahauliwa, na kwa kuwa zimefichwa machoni pangu. Isaya 65:16 |
so that he who blesses himself in the earth shall bless himself in the God of truth; and he who swears in the earth shall swear by the God of truth; because the former troubles are forgotten, and because they are hid from my eyes. |
Maana, tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni. Isaya 65:17 |
For, behold, I create new heavens and a new earth; and the former things shall not be remembered, nor come into mind. |
Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha. Isaya 65:18 |
But be you glad and rejoice forever in that which I create; for, behold, I create Jerusalem a rejoicing, and her people a joy. |
Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza. Isaya 65:19 |
I will rejoice in Jerusalem, and joy in my people; and there shall be heard in her no more the voice of weeping and the voice of crying. |
Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa. Isaya 65:20 |
There shall be no more there an infant of days, nor an old man who has not filled his days; for the child shall die one hundred years old, and the sinner being one hundred years old shall be accursed. |
Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Isaya 65:21 |
They shall build houses, and inhabit them; and they shall plant vineyards, and eat the fruit of them. |
Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi. Isaya 65:22 |
They shall not build, and another inhabit; they shall not plant, and another eat: for as the days of a tree shall be the days of my people, and my chosen shall long enjoy the work of their hands. |
Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na Bwana, na watoto wao pamoja nao. Isaya 65:23 |
They shall not labor in vain, nor bring forth for calamity; for they are the seed of the blessed of Yahweh, and their offspring with them. |
Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia. Isaya 65:24 |
It shall happen that, before they call, I will answer; and while they are yet speaking, I will hear. |
Mbwa-mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ng'ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote, asema Bwana. Isaya 65:25 |
The wolf and the lamb shall feed together, and the lion shall eat straw like the ox; and dust shall be the serpent's food. They shall not hurt nor destroy in all my holy mountain, says Yahweh. |