Isaya 53 Swahili & English

Listen/Download Audio
Isaya 53 (Swahili) Isaiah 53 (English)

Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani? Isaya 53:1

Who has believed our message? and to whom has the arm of Yahweh been revealed?

Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani. Isaya 53:2

For he grew up before him as a tender plant, and as a root out of a dry ground: he has no form nor comeliness; and when we see him, there is no beauty that we should desire him.

Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Isaya 53:3

He was despised, and rejected by men; a man of suffering, and acquainted with disease: and as one from whom men hide their face he was despised; and we didn't respect him.

Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Isaya 53:4

Surely he has borne our sickness, and carried our suffering; yet we considered him plagued, struck by God, and afflicted.

Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Isaya 53:5

But he was pierced for our transgressions, he was crushed for our iniquities; the punishment that brought our peace was on him; and by his wounds we are healed.

Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote. Isaya 53:6

All we like sheep have gone astray; everyone has turned to his own way; and Yahweh has laid on him the iniquity of us all.

Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake. Isaya 53:7

He was oppressed, yet when he was afflicted he didn't open his mouth; as a lamb that is led to the slaughter, and as a sheep that before its shearers is mute, so he didn't open his mouth.

Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu. Isaya 53:8

By oppression and judgment he was taken away; and as for his generation, who [among them] considered that he was cut off out of the land of the living for the disobedience of my people to whom the stroke [was due]?

Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake. Isaya 53:9

They made his grave with the wicked, and with a rich man in his death; although he had done no violence, neither was any deceit in his mouth.

Lakini Bwana aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake; Isaya 53:10

Yet it pleased Yahweh to bruise him; he has put him to grief: when you shall make his soul an offering for sin, he shall see [his] seed, he shall prolong his days, and the pleasure of Yahweh shall prosper in his hand.

Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao. Isaya 53:11

He shall see of the travail of his soul, [and] shall be satisfied: by the knowledge of himself shall my righteous servant justify many; and he shall bear their iniquities.

Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini alichukua dhambi za watu wengi, Na kuwaombea wakosaji. Isaya 53:12

Therefore will I divide him a portion with the great, and he shall divide the spoil with the strong; because he poured out his soul to death, and was numbered with the transgressors: yet he bore the sin of many, and made intercession for the transgressors.