Isaya 53 Swahili & English
Listen/Download AudioIsaya 53 (Swahili) | Isaiah 53 (English) |
---|---|
Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani? Isaya 53:1 |
Who has believed our message? and to whom has the arm of Yahweh been revealed? |
Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani. Isaya 53:2 |
For he grew up before him as a tender plant, and as a root out of a dry ground: he has no form nor comeliness; and when we see him, there is no beauty that we should desire him. |
Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Isaya 53:3 |
He was despised, and rejected by men; a man of suffering, and acquainted with disease: and as one from whom men hide their face he was despised; and we didn't respect him. |
Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Isaya 53:4 |
Surely he has borne our sickness, and carried our suffering; yet we considered him plagued, struck by God, and afflicted. |
Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Isaya 53:5 |
But he was pierced for our transgressions, he was crushed for our iniquities; the punishment that brought our peace was on him; and by his wounds we are healed. |
Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote. Isaya 53:6 |
All we like sheep have gone astray; everyone has turned to his own way; and Yahweh has laid on him the iniquity of us all. |
Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake. Isaya 53:7 |
He was oppressed, yet when he was afflicted he didn't open his mouth; as a lamb that is led to the slaughter, and as a sheep that before its shearers is mute, so he didn't open his mouth. |
Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu. Isaya 53:8 |
By oppression and judgment he was taken away; and as for his generation, who [among them] considered that he was cut off out of the land of the living for the disobedience of my people to whom the stroke [was due]? |
Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake. Isaya 53:9 |
They made his grave with the wicked, and with a rich man in his death; although he had done no violence, neither was any deceit in his mouth. |
Lakini Bwana aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake; Isaya 53:10 |
Yet it pleased Yahweh to bruise him; he has put him to grief: when you shall make his soul an offering for sin, he shall see [his] seed, he shall prolong his days, and the pleasure of Yahweh shall prosper in his hand. |
Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao. Isaya 53:11 |
He shall see of the travail of his soul, [and] shall be satisfied: by the knowledge of himself shall my righteous servant justify many; and he shall bear their iniquities. |
Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini alichukua dhambi za watu wengi, Na kuwaombea wakosaji. Isaya 53:12 |
Therefore will I divide him a portion with the great, and he shall divide the spoil with the strong; because he poured out his soul to death, and was numbered with the transgressors: yet he bore the sin of many, and made intercession for the transgressors. |