Isaya 16 Swahili & English

Listen/Download Audio
Isaya 16 (Swahili) Isaiah 16 (English)

Pelekeni wana-kondoo, kodi yake aitawalaye nchi toka Sela kuelekea jangwani, mpaka mlima wa binti Sayuni. Isaya 16:1

Send you the lambs for the ruler of the land from Selah to the wilderness, to the mountain of the daughter of Zion.

Na binti za Moabu watakuwa kama ndege warukao huko na huko, kama kioto cha ndege waliotiwa hofu, kwenye vivuko vya Arnoni. Isaya 16:2

For it shall be that, as wandering birds, as a scattered nest, so shall the daughters of Moab be at the fords of the Arnon.

Lete shauri; kata neno; fanya kivuli chako kuwa kama usiku kati ya mchana; wafiche waliofukuzwa; usiwachongee waliopotea. Isaya 16:3

Give counsel, execute justice; make your shade as the night in the midst of the noonday; hide the outcasts; don't betray the fugitive.

Watu wangu waliofukuzwa waache wakae pamoja nawe; katika habari za Moabu, uwe sitara kwake mbele ya uso wake anayeharibu; maana yeye atozaye kwa nguvu amekoma; afanyaye ukiwa ametoweka; waliokanyaga watu wametoka katika nchi. Isaya 16:4

Let my outcasts dwell with you; as for Moab, be a covert to him from the face of the destroyer. For the extortioner is brought to nothing, destruction ceases, the oppressors are consumed out of the land.

Na kiti cha enzi kitafanywa imara kwa rehema; na mmoja ataketi juu yake katika kweli, katika hema ya Daudi; akifanya hukumu, akitaka sana yaliyo haki, mwepesi wa kutenda haki. Isaya 16:5

A throne shall be established in loving kindness; and one shall sit thereon in truth, in the tent of David, judging, and seeking justice, and swift to do righteousness.

Tumesikia habari za kiburi cha Moabu, ya kwamba ni mwenye kiburi kingi; habari za majivuno yake, na kiburi chake, na ghadhabu yake; majivuno yake si kitu. Isaya 16:6

We have heard of the pride of Moab, [that] he is very proud; even of his arrogance, and his pride, and his wrath; his boastings are nothing.

Kwa sababu hiyo Moabu atalia kwa ajili ya Moabu, kila mmoja atalia, maana mtaiombolezea mikate ya zabibu ya Kir-Haresethi, mkipigwa sana. Isaya 16:7

Therefore shall Moab wail for Moab, everyone shall wail: for the raisin-cakes of Kir Hareseth shall you mourn, utterly stricken.

Maana makonde ya Heshboni yamenyauka, na mzabibu wa Sibma; mabwana wa mataifa wameyavunja matawi yake mateule; yamefika hata Yazeri, yalitanga-tanga hata nyikani; matawi yake yalitapakaa, yaliivuka bahari. Isaya 16:8

For the fields of Heshbon languish, [and] the vine of Sibmah; the lords of the nations have broken down the choice branches of it, which reached even to Jazer, which wandered into the wilderness; its shoots were spread abroad, they passed over the sea.

Basi, naililia mizabibu ya Sibma kwa kilio cha Yazeri, nitawanyeshea machozi yangu, Ee Heshboni na Eleale, kwa kuwa kelele za vita zimeyaangukia mavuno ya matunda yako, na mavuno ya mizabibu yako. Isaya 16:9

Therefore I will weep with the weeping of Jazer for the vine of Sibmah; I will water you with my tears, Heshbon, and Elealeh: for on your summer fruits and on your harvest the [battle] shout is fallen.

Na furaha imeondolewa, na shangwe toka mashamba yaliyozaa sana; hapana kuimba katika mashamba ya mizabibu, wala sauti za furaha; akanyagaye hakanyagi divai katika mashinikizo; nimeikomesha sauti ya furaha yake akanyagaye. Isaya 16:10

Gladness is taken away, and joy out of the fruitful field; and in the vineyards there shall be no singing, neither joyful noise: nobody shall tread out wine in the presses; I have made the [vintage] shout to cease.

Kwa sababu hiyo mtima wangu unamlilia Moabu kama kinubi, na matumbo yangu kwa ajili ya Kir-Heresi. Isaya 16:11

Why my heart sounds like a harp for Moab, and my inward parts for Kir Heres.

Tena itakuwa, Moabu akionekana, na kujichosha kwa kulia juu ya mahali pa juu, na kuingia katika patakatifu pake aombe, hatapata kushinda. Isaya 16:12

It shall happen, when Moab presents himself, when he wearies himself on the high place, and shall come to his sanctuary to pray, that he shall not prevail.

Hilo ndilo neno lile alilolisema Bwana juu ya Moabu zamani. Isaya 16:13

This is the word that Yahweh spoke concerning Moab in time past.

Lakini sasa Bwana asema hivi, Katika muda wa miaka mitatu, kama miaka ya mtu wa mshahara, utukufu wa Moabu utadharauliwa, pamoja na wingi wake wote; mabaki yake yatakuwa machache sana, kama si kitu kabisa. Isaya 16:14

But now Yahweh has spoken, saying, Within three years, as the years of a hireling, the glory of Moab shall be brought into contempt, with all his great multitude; and the remnant shall be very small and of no account.