Isaya 14 Swahili & English

Listen/Download Audio
Isaya 14 (Swahili) Isaiah 14 (English)

Maana Bwana atamhurumia Yakobo, atamchagua Israeli tena, naye atawaweka katika nchi yao wenyewe; na mgeni atajiunga nao, nao wataambatana na nyumba ya Yakobo. Isaya 14:1

For Yahweh will have compassion on Jacob, and will yet choose Israel, and set them in their own land: and the foreigner shall join himself with them, and they shall cleave to the house of Jacob.

Na hao mataifa watawatwaa na kuwaleta mpaka mahali pao wenyewe, na nyumba ya Israeli watawamiliki, na kuwafanya watumishi na wajakazi katika nchi ya Bwana; nao watawachukua hali ya kufungwa watu wale waliowafunga wao, nao watawamiliki watu wale waliowaonea. Isaya 14:2

The peoples shall take them, and bring them to their place; and the house of Israel shall possess them in the land of Yahweh for servants and for handmaids: and they shall take them captive whose captives they were; and they shall rule over their oppressors.

Tena itakuwa katika siku ile, ambayo Bwana atakupa raha baada ya huzuni yako, na baada ya taabu yako, na baada ya utumishi ule mgumu uliotumikishwa; Isaya 14:3

It shall happen in the day that Yahweh shall give you rest from your sorrow, and from your trouble, and from the hard service in which you were made to serve,

utatunga mithali hii juu ya mfalme wa Babeli, na kusema, Jinsi alivyokoma mwenye kuonea; Jinsi ulivyokoma mji ule wenye jeuri! Isaya 14:4

that you shall take up this parable against the king of Babylon, and say, How has the oppressor ceased! the golden city ceased!

Bwana amelivunja gongo la wabaya, Fimbo ya enzi yao wenye kutawala. Isaya 14:5

Yahweh has broken the staff of the wicked, the scepter of the rulers;

Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu. Isaya 14:6

who struck the peoples in wrath with a continual stroke, who ruled the nations in anger, with a persecution that none restrained.

Dunia yote inastarehe na kutulia; Hata huanzilisha kuimba. Isaya 14:7

The whole earth is at rest, [and] is quiet: they break forth into singing.

Naam, misunobari inakufurahia, Na mierezi ya Lebanoni, ikisema, Tokea wakati ulipolazwa chini wewe, Hapana mkata miti aliyetujia. Isaya 14:8

Yes, the fir trees rejoice at you, [and] the cedars of Lebanon, [saying], Since you are laid low, no lumberjack is come up against us.

Kuzimu chini kumetaharuki kwa ajili yako, Ili kukulaki utakapokuja; Huwaamsha waliokufa kwa ajili yako, Naam, walio wakuu wote wa dunia; Huwainua wafalme wote wa mataifa, Watoke katika viti vyao vya enzi. Isaya 14:9

Sheol from beneath is moved for you to meet you at your coming; it stirs up the dead for you, even all the chief ones of the earth; it has raised up from their thrones all the kings of the nations.

Hao wote watajibu na kukuambia, Je! Wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe umekuwa kama sisi! Isaya 14:10

All they shall answer and tell you, Are you also become weak as we? are you become like us?

Fahari yako imeshushwa hata kuzimu, Na sauti ya vinanda vyako; Funza wametandazwa chini yako, Na vidudu vinakufunika. Isaya 14:11

Your pomp is brought down to Sheol, [and] the noise of your viols: the worm is spread under you, and worms cover you.

Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! Isaya 14:12

How you are fallen from heaven, day-star, son of the morning! How you are cut down to the ground, who laid the nations low!

Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. Isaya 14:13

You said in your heart, I will ascend into heaven, I will exalt my throne above the stars of God; and I will sit on the mountain of congregation, in the uttermost parts of the north;

Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. Isaya 14:14

I will ascend above the heights of the clouds; I will make myself like the Most High.

Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo. Isaya 14:15

Yet you shall be brought down to Sheol, to the uttermost parts of the pit.

Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme; Isaya 14:16

Those who see you shall gaze at you, they shall consider you, [saying], "Is this the man who made the earth to tremble, who shook kingdoms;

Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao? Isaya 14:17

who made the world as a wilderness, and overthrew the cities of it; who didn't let loose his prisoners to their home?"

Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima, Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe; Isaya 14:18

All the kings of the nations, all of them, sleep in glory, everyone in his own house.

Bali wewe umetupwa mbali na kaburi lako, Kama chipukizi lililochukiza kabisa; Kama vazi la wale waliouawa, Wale waliochomwa kwa upanga, Wale washukao mpaka misingi ya shimo; Kama mzoga uliokanyagwa chini ya miguu. Isaya 14:19

But you are cast forth away from your tomb like an abominable branch, clothed with the slain, who are thrust through with the sword, who go down to the stones of the pit; as a dead body trodden under foot.

Hutaungamanishwa pamoja nao katika mazishi, Kwa maana umeiharibu nchi yako, Umewaua watu wako; Kizazi chao watendao uovu hakitatajwa milele. Isaya 14:20

You shall not be joined with them in burial, because you have destroyed your land, you have killed your people; the seed of evil-doers shall not be named forever.

Fanyeni tayari machinjo kwa watoto wake. Kwa sababu ya uovu wa baba zao; Wasije wakainuka na kuitamalaki nchi, Na kuujaza miji uso wa ulimwengu. Isaya 14:21

Prepare slaughter for his children for the iniquity of their fathers, that they not rise up, and possess the earth, and fill the surface of the world with cities.

Nami nitainuka, nishindane nao; asema Bwana wa majeshi; na katika Babeli nitang'oa jina na mabaki, mwana na mjukuu; asema Bwana. Isaya 14:22

I will rise up against them, says Yahweh of Hosts, and cut off from Babylon name and remnant, and son and son's son, says Yahweh.

Tena nitaifanya hiyo nchi kuwa makao ya nungu, na maziwa ya maji; nami nitaifagilia mbali kwa ufagio wa uharibifu; asema Bwana wa majeshi. Isaya 14:23

I will also make it a possession for the porcupine, and pools of water: and I will sweep it with the broom of destruction, says Yahweh of Hosts.

Bwana wa majeshi ameapa, akisema, Hakika yangu kama vile vilivyoazimia, ndivyo itakavyokuwa; na kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyotokea; Isaya 14:24

Yahweh of Hosts has sworn, saying, Surely, as I have thought, so shall it happen; and as I have purposed, so shall it stand:

kwamba nitamvunja huyo Mwashuri vipande vipande katika nchi yangu, na juu ya mlima wangu nitamkanyaga chini ya miguu yangu; ndipo nira yake iliyo juu yao itakapoondoka, na mzigo wake utatoka mabegani mwao. Isaya 14:25

that I will break the Assyrian in my land, and on my mountains tread him under foot: then shall his yoke depart from off them, and his burden depart from off their shoulder.

Hilo ndilo kusudi lililokusudiwa duniani mwote, na huo ndio mkono ulionyoshwa juu ya mataifa yote. Isaya 14:26

This is the purpose that is purposed on the whole earth; and this is the hand that is stretched out on all the nations.

Maana Bwana wa majeshi amekusudia, naye ni nani atakayelibatili? Na mkono wake ulionyoshwa, ni nani atakayeugeuza nyuma? Isaya 14:27

For Yahweh of Hosts has purposed, and who shall annul it? and his hand is stretched out, and who shall turn it back?

Ufunuo huu ulikuja mwaka ule alipokufa mfalme Ahazi. Isaya 14:28

In the year that king Ahaz died was this burden.

Usifurahi, Ee Ufilisti, pia wote, Kwa sababu fimbo ile iliyokupiga imevunjika; Maana katika shina la nyoka atatoka fira, Na uzao wake ni joka la moto arukaye Isaya 14:29

Don't rejoice, O Philistia, all of you, because the rod that struck you is broken; for out of the serpent's root shall come forth an adder, and his fruit shall be a fiery flying serpent.

Nao walio maskini kabisa watakula, Na wahitaji watajilaza salama; Nami nitatia shina lako kwa njaa, Na mabaki yako watauawa. Isaya 14:30

The firstborn of the poor shall feed, and the needy shall lie down in safety; and I will kill your root with famine, and your remnant shall be killed.

Piga yowe, Ee lango; lia, Ee mji; Ee Ufilisti, pia wote, umeyeyuka kabisa; Maana moshi unakuja toka kaskazini, Wala hakuna atakayechelewa katika majeshi yake. Isaya 14:31

Howl, gate; cry, city; you are melted away, Philistia, all of you; for there comes a smoke out of the north, and there is no straggler in his ranks.

Wajumbe wa taifa hilo waletewe jibu gani? Ya kuwa Bwana ameiweka misingi ya Sayuni, na ndani yake wale walioonewa katika watu wake wataona kimbilio. Isaya 14:32

What then shall one answer the messengers of the nation? That Yahweh has founded Zion, and in her shall the afflicted of his people take refuge.