Isaya 29 Swahili & English
Listen/Download AudioIsaya 29 (Swahili) | Isaiah 29 (English) |
---|---|
Ole wa Arieli, Arieli, mji ambao Daudi alifanya kituo chake ndani yake; ongezeni mwaka baada ya mwaka; sikukuu na zirudi wakati wake, Isaya 29:1 |
Ho Ariel, Ariel, the city where David encamped! add you year to year; let the feasts come round: |
ndipo nitamwudhi Arieli; kutakuwapo maombolezo na kilio; naye atakuwa kwangu kama Arieli. Isaya 29:2 |
then will I distress Ariel, and there shall be mourning and lamentation; and she shall be to me as Ariel. |
Nami nitapiga kimo juu yako pande zote, nitakuhusuru kwa ngome, nami nitajenga maboma yakuzunguke. Isaya 29:3 |
I will encamp against you round about, and will lay siege against you with posted troops, and I will raise siege works against you. |
Nawe utashushwa, nawe utanena toka chini ya nchi, na maneno yako yatakuwa chini toka mavumbini; na sauti yako itakuwa kama sauti ya mtu mwenye pepo, ikitoka katika nchi, na matamko yako yatanong'ona toka mavumbini. Isaya 29:4 |
You shall be brought down, and shall speak out of the ground, and your speech shall be low out of the dust; and your voice shall be as of one who has a familiar spirit, out of the ground, and your speech shall whisper out of the dust. |
Lakini wingi wa adui zako utakuwa kama mavumbi membamba, na wingi wao watishao utakuwa kama makapi yapitayo; naam, itakuwa mara na kwa ghafula. Isaya 29:5 |
But the multitude of your foes shall be like small dust, and the multitude of the awesome ones as chaff that passes away: yes, it shall be in an instant suddenly. |
Naye atajiliwa na Bwana wa majeshi kwa ngurumo, na tetemeko la nchi, na sauti kuu, na chamchela, na tufani, na mwali wa moto uteketezao. Isaya 29:6 |
She shall be visited of Yahweh of Hosts with thunder, and with earthquake, and great noise, with whirlwind and tempest, and the flame of a devouring fire. |
Na wingi wa mataifa wapiganao na Arieli, wote wapiganao naye na ngome yake, nao wamwudhio, watakuwa kama ndoto, na maono ya usiku. Isaya 29:7 |
The multitude of all the nations that fight against Ariel, even all who fight against her and her stronghold, and who distress her, shall be as a dream, a vision of the night. |
Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni. Isaya 29:8 |
It shall be as when a hungry man dreams, and, behold, he eats; but he awakes, and his soul is empty: or as when a thirsty man dreams, and, behold, he drinks; but he awakes, and, behold, he is faint, and his soul has appetite: so shall the multitude of all the nations be, that fight against Mount Zion. |
Ngojeni mstaajabu; fanyeni anasa zenu na kuwa vipofu; wamelewa wala si kwa mvinyo; wamewaya-waya wala si kwa sababu ya kileo. Isaya 29:9 |
Stay you and wonder; take your pleasure and be blind: they are drunken, but not with wine; they stagger, but not with strong drink. |
Kwa maana Bwana amewamwagieni roho ya usingizi, amefumba macho yenu, yaani, manabii; amefunika vichwa vyenu, yaani, waonaji. Isaya 29:10 |
For Yahweh has poured out on you the spirit of deep sleep, and has closed your eyes, the prophets; and your heads, the seers, has he covered. |
Na maono yote yamekuwa kwenu kama maneno ya chuo kilichotiwa muhuri, ambacho watu humpa mtu aliye na maarifa, wakisema, Tafadhali ukisome hiki; akasema, Siwezi, kwa kuwa kimetiwa muhuri; Isaya 29:11 |
All vision is become to you as the words of a book that is sealed, which men deliver to one who is learned, saying, Read this, I pray you; and he says, I can't, for it is sealed: |
kisha chuo hiki apewa mtu asiye na maarifa, akaambiwa, Kisome hicho tafadhali, akasema, Sina maarifa mimi. Isaya 29:12 |
and the book is delivered to him who is not learned, saying, Read this, I pray you; and he says, I am not learned. |
Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walicho nacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa; Isaya 29:13 |
The Lord said, Because this people draw near [to me], and with their mouth and with their lips to honor me, but have removed their heart far from me, and their fear of me is a commandment of men which has been taught [them]; |
kwa sababu hiyo mimi nitafanya tena kazi ya ajabu kati ya watu hawa, kazi ya ajabu na mwujiza; na akili za watu wao wenye akili zitapotea, na ufahamu wa wenye busara wao utafichwa. Isaya 29:14 |
therefore, behold, I will proceed to do a marvelous work among this people, even a marvelous work and a wonder; and the wisdom of their wise men shall perish, and the understanding of their prudent men shall be hid. |
Ole wao wanaojitahidi kumficha Bwana mashauri yao, na matendo yao yamo gizani, nao husema, Ni nani atuonaye? Nani atujuaye? Isaya 29:15 |
Woe to those who hide deep their counsel from Yahweh, and whose works are in the dark, and who say, Who sees us? and who knows us? |
Ninyi mnapindua mambo; Je! Mfinyanzi ahesabiwe kuwa kama udongo; kitu kilichofinyangwa kimnene yeye aliyekifinyanga, Hakunifinyanga huyu; au kitu kilichoumbwa kimnene yeye aliyekiumba, Yeye hana ufahamu? Isaya 29:16 |
You turn things upside down! Shall the potter be esteemed as clay; that the thing made should say of him who made it, He didn't make me; or the thing formed say of him who formed it, He has no understanding? |
Je! Si muda mdogo uliobaki, na Lebanoni itageuzwa kuwa shamba lizaalo sana, na lile shamba lizaalo sana litahesabiwa kuwa msitu? Isaya 29:17 |
Is it not yet a very little while, and Lebanon shall be turned into a fruitful field, and the fruitful field shall be esteemed as a forest? |
Na katika siku hiyo viziwi watasikia maneno ya hicho chuo, na macho ya vipofu yataona katika upofu na katika giza. Isaya 29:18 |
In that day shall the deaf hear the words of the book, and the eyes of the blind shall see out of obscurity and out of darkness. |
Wanyenyekevu nao wataongeza furaha yao katika Bwana, na maskini katika wanadamu watafurahi katika Mtakatifu wa Israeli. Isaya 29:19 |
The humble also shall increase their joy in Yahweh, and the poor among men shall rejoice in the Holy One of Israel. |
Kwa maana mwenye kutisha ameangamizwa, naye mwenye dharau amekoma, nao wote watazamiao uovu wamekatiliwa mbali; Isaya 29:20 |
For the terrible one is brought to nothing, and the scoffer ceases, and all those who watch for iniquity are cut off; |
hao wamfanyao mtu kuwa amekosa katika neno, na kumtegea mtego yeye aonyaye langoni, na kumgeuza mwenye haki kwa kitu kisichofaa. Isaya 29:21 |
that make a man an offender in [his] cause, and lay a snare for him who reproves in the gate, and turn aside the just with a thing of nothing. |
Basi, Bwana aliyemkomboa Ibrahimu asema hivi, katika habari za nyumba ya Yakobo; Yakobo hatatahayarika sasa, wala uso wake hautabadilika rangi yake. Isaya 29:22 |
Therefore thus says Yahweh, who redeemed Abraham, concerning the house of Jacob: Jacob shall not now be ashamed, neither shall his face now wax pale. |
Bali atakapowaona watoto wake, walio kazi ya mikono yangu, katikati yake, wao watalitakasa jina langu; naam, watamtakasa Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli. Isaya 29:23 |
But when he sees his children, the work of my hands, in the midst of him, they shall sanctify my name; yes, they shall sanctify the Holy One of Jacob, and shall stand in awe of the God of Israel. |
Hao nao wakosao rohoni mwao watapata kufahamu, na hao wanung'unikao watajifunza elimu. Isaya 29:24 |
They also who err in spirit shall come to understanding, and those who murmur shall receive instruction. |