Isaya 29 Swahili & English

Listen/Download Audio
Isaya 29 (Swahili) Isaiah 29 (English)

Ole wa Arieli, Arieli, mji ambao Daudi alifanya kituo chake ndani yake; ongezeni mwaka baada ya mwaka; sikukuu na zirudi wakati wake, Isaya 29:1

Ho Ariel, Ariel, the city where David encamped! add you year to year; let the feasts come round:

ndipo nitamwudhi Arieli; kutakuwapo maombolezo na kilio; naye atakuwa kwangu kama Arieli. Isaya 29:2

then will I distress Ariel, and there shall be mourning and lamentation; and she shall be to me as Ariel.

Nami nitapiga kimo juu yako pande zote, nitakuhusuru kwa ngome, nami nitajenga maboma yakuzunguke. Isaya 29:3

I will encamp against you round about, and will lay siege against you with posted troops, and I will raise siege works against you.

Nawe utashushwa, nawe utanena toka chini ya nchi, na maneno yako yatakuwa chini toka mavumbini; na sauti yako itakuwa kama sauti ya mtu mwenye pepo, ikitoka katika nchi, na matamko yako yatanong'ona toka mavumbini. Isaya 29:4

You shall be brought down, and shall speak out of the ground, and your speech shall be low out of the dust; and your voice shall be as of one who has a familiar spirit, out of the ground, and your speech shall whisper out of the dust.

Lakini wingi wa adui zako utakuwa kama mavumbi membamba, na wingi wao watishao utakuwa kama makapi yapitayo; naam, itakuwa mara na kwa ghafula. Isaya 29:5

But the multitude of your foes shall be like small dust, and the multitude of the awesome ones as chaff that passes away: yes, it shall be in an instant suddenly.

Naye atajiliwa na Bwana wa majeshi kwa ngurumo, na tetemeko la nchi, na sauti kuu, na chamchela, na tufani, na mwali wa moto uteketezao. Isaya 29:6

She shall be visited of Yahweh of Hosts with thunder, and with earthquake, and great noise, with whirlwind and tempest, and the flame of a devouring fire.

Na wingi wa mataifa wapiganao na Arieli, wote wapiganao naye na ngome yake, nao wamwudhio, watakuwa kama ndoto, na maono ya usiku. Isaya 29:7

The multitude of all the nations that fight against Ariel, even all who fight against her and her stronghold, and who distress her, shall be as a dream, a vision of the night.

Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni. Isaya 29:8

It shall be as when a hungry man dreams, and, behold, he eats; but he awakes, and his soul is empty: or as when a thirsty man dreams, and, behold, he drinks; but he awakes, and, behold, he is faint, and his soul has appetite: so shall the multitude of all the nations be, that fight against Mount Zion.

Ngojeni mstaajabu; fanyeni anasa zenu na kuwa vipofu; wamelewa wala si kwa mvinyo; wamewaya-waya wala si kwa sababu ya kileo. Isaya 29:9

Stay you and wonder; take your pleasure and be blind: they are drunken, but not with wine; they stagger, but not with strong drink.

Kwa maana Bwana amewamwagieni roho ya usingizi, amefumba macho yenu, yaani, manabii; amefunika vichwa vyenu, yaani, waonaji. Isaya 29:10

For Yahweh has poured out on you the spirit of deep sleep, and has closed your eyes, the prophets; and your heads, the seers, has he covered.

Na maono yote yamekuwa kwenu kama maneno ya chuo kilichotiwa muhuri, ambacho watu humpa mtu aliye na maarifa, wakisema, Tafadhali ukisome hiki; akasema, Siwezi, kwa kuwa kimetiwa muhuri; Isaya 29:11

All vision is become to you as the words of a book that is sealed, which men deliver to one who is learned, saying, Read this, I pray you; and he says, I can't, for it is sealed:

kisha chuo hiki apewa mtu asiye na maarifa, akaambiwa, Kisome hicho tafadhali, akasema, Sina maarifa mimi. Isaya 29:12

and the book is delivered to him who is not learned, saying, Read this, I pray you; and he says, I am not learned.

Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walicho nacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa; Isaya 29:13

The Lord said, Because this people draw near [to me], and with their mouth and with their lips to honor me, but have removed their heart far from me, and their fear of me is a commandment of men which has been taught [them];

kwa sababu hiyo mimi nitafanya tena kazi ya ajabu kati ya watu hawa, kazi ya ajabu na mwujiza; na akili za watu wao wenye akili zitapotea, na ufahamu wa wenye busara wao utafichwa. Isaya 29:14

therefore, behold, I will proceed to do a marvelous work among this people, even a marvelous work and a wonder; and the wisdom of their wise men shall perish, and the understanding of their prudent men shall be hid.

Ole wao wanaojitahidi kumficha Bwana mashauri yao, na matendo yao yamo gizani, nao husema, Ni nani atuonaye? Nani atujuaye? Isaya 29:15

Woe to those who hide deep their counsel from Yahweh, and whose works are in the dark, and who say, Who sees us? and who knows us?

Ninyi mnapindua mambo; Je! Mfinyanzi ahesabiwe kuwa kama udongo; kitu kilichofinyangwa kimnene yeye aliyekifinyanga, Hakunifinyanga huyu; au kitu kilichoumbwa kimnene yeye aliyekiumba, Yeye hana ufahamu? Isaya 29:16

You turn things upside down! Shall the potter be esteemed as clay; that the thing made should say of him who made it, He didn't make me; or the thing formed say of him who formed it, He has no understanding?

Je! Si muda mdogo uliobaki, na Lebanoni itageuzwa kuwa shamba lizaalo sana, na lile shamba lizaalo sana litahesabiwa kuwa msitu? Isaya 29:17

Is it not yet a very little while, and Lebanon shall be turned into a fruitful field, and the fruitful field shall be esteemed as a forest?

Na katika siku hiyo viziwi watasikia maneno ya hicho chuo, na macho ya vipofu yataona katika upofu na katika giza. Isaya 29:18

In that day shall the deaf hear the words of the book, and the eyes of the blind shall see out of obscurity and out of darkness.

Wanyenyekevu nao wataongeza furaha yao katika Bwana, na maskini katika wanadamu watafurahi katika Mtakatifu wa Israeli. Isaya 29:19

The humble also shall increase their joy in Yahweh, and the poor among men shall rejoice in the Holy One of Israel.

Kwa maana mwenye kutisha ameangamizwa, naye mwenye dharau amekoma, nao wote watazamiao uovu wamekatiliwa mbali; Isaya 29:20

For the terrible one is brought to nothing, and the scoffer ceases, and all those who watch for iniquity are cut off;

hao wamfanyao mtu kuwa amekosa katika neno, na kumtegea mtego yeye aonyaye langoni, na kumgeuza mwenye haki kwa kitu kisichofaa. Isaya 29:21

that make a man an offender in [his] cause, and lay a snare for him who reproves in the gate, and turn aside the just with a thing of nothing.

Basi, Bwana aliyemkomboa Ibrahimu asema hivi, katika habari za nyumba ya Yakobo; Yakobo hatatahayarika sasa, wala uso wake hautabadilika rangi yake. Isaya 29:22

Therefore thus says Yahweh, who redeemed Abraham, concerning the house of Jacob: Jacob shall not now be ashamed, neither shall his face now wax pale.

Bali atakapowaona watoto wake, walio kazi ya mikono yangu, katikati yake, wao watalitakasa jina langu; naam, watamtakasa Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli. Isaya 29:23

But when he sees his children, the work of my hands, in the midst of him, they shall sanctify my name; yes, they shall sanctify the Holy One of Jacob, and shall stand in awe of the God of Israel.

Hao nao wakosao rohoni mwao watapata kufahamu, na hao wanung'unikao watajifunza elimu. Isaya 29:24

They also who err in spirit shall come to understanding, and those who murmur shall receive instruction.