1
Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume.
And Saul was there, giving approval to Stephen’s death. On that day a great persecution broke out against the church in Jerusalem, and all except the apostles were scattered throughout Judea and Samaria.
2
Watu watauwa wakamzika Stefano, wakamfanyia maombolezo makuu.
God-fearing men buried Stephen and mourned deeply over him.
3
Sauli akaliharibu kanisa, akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani.
But Saul began to destroy the church. Going from house to house, he dragged off men and women and put them in prison.
4
Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.
Those who had been scattered preached the word wherever they went.
5
Filipo akatelemka akaingia mji wa Samaria, akawahubiri Kristo.
Philip went down to a city in Samaria and proclaimed the Christ to them.
6
Na makutano kwa nia moja wakasikiliza maneno yale yaliyosemwa na Filipo walipoyasikia na kuziona ishara alizokuwa akizifanya.
The crowds all paid close attention to Philip’s message and to the signs they saw him perform.
7
Kwa maana pepo wachafu wakawatoka wengi waliopagawa nao, wakilia kwa sauti kuu; na watu wengi waliopooza, na viwete, wakaponywa.
With loud shrieks, unclean spirits came out of many who were possessed, and many of the paralyzed and lame were healed.
8
Ikawa furaha kubwa katika mji ule.
So there was great joy in that city.
9
Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.
Prior to that time, a man named Simon had practiced sorcery in the city and astounded the people of Samaria. He claimed to be someone great,
10
Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.
and all the people, from the least to the greatest, heeded his words and said, “This man is the divine power called the Great Power.”
11
Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.
They paid close attention to him because he had astounded them for a long time with his sorcery.
12
Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake.
But when they believed Philip as he preached the gospel of the kingdom of God and the name of Jesus Christ, they were baptized, both men and women.
13
Na yeye Simoni mwenyewe aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo; akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa inayotendeka.
Even Simon himself believed and was baptized. He followed Philip closely and was astounded by the great signs and miracles he observed.
14
Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;
When the apostles in Jerusalem heard that Samaria had received the word of God, they sent Peter and John to them.
15
ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;
On their arrival, they prayed for them to receive the Holy Spirit.
16
kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.
For the Holy Spirit had not yet fallen upon any of them; they had simply been baptized into the name of the Lord Jesus.
17
Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
Then Peter and John laid their hands on them, and they received the Holy Spirit.
18
Hata Simoni alipoona ya kuwa watu wanapewa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono ya mitume, akataka kuwapa fedha akisema,
When Simon saw that the Spirit was given through the laying on of the apostles’ hands, he offered them money.
19
Nipeni na mimi uwezo huu, ili kila mtu nitakayemweka mikono yangu, apokee Roho Mtakatifu.
“Give me this power as well,” he said, “so that everyone on whom I lay my hands may receive the Holy Spirit.”
20
Lakini Petro akamwambia, Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.
But Peter replied, “May your silver perish with you, because you thought you could buy the gift of God with money!
21
Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za Mungu.
You have no part or share in our ministry, because your heart is not right before God.
22
Basi, tubia uovu wako huu, ukamwombe Bwana, ili kama yamkini, usamehewe fikira hii ya moyo wako.
Repent, therefore, of your wickedness, and pray to the Lord. Perhaps He will forgive you for the intent of your heart.
23
Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo, na tena u katika kifungo cha uovu.
For I see that you are poisoned by bitterness and captive to iniquity.”
24
Simoni akajibu, akasema, Niombeeni ninyi kwa Bwana, yasinifikilie mambo haya mliyosema hata moja.
Then Simon answered, “Pray to the Lord for me, so that nothing you have said may happen to me.”
25
Nao walipokwisha kushuhudia na kulihubiri neno la Bwana wakarudi Yerusalemu, wakaihubiri Injili katika vijiji vingi vya Wasamaria.
And after Peter and John had testified and spoken the word of the Lord, they returned to Jerusalem, preaching the gospel in many of the Samaritan villages.
26
Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa.
Now an angel of the Lord said to Philip, “Get up and go south to the desert road that goes down from Jerusalem to Gaza.”
27
Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu,
So he started out, and on his way he met an Ethiopian eunuch, a court official in charge of the entire treasury of Candace, queen of the Ethiopians. He had gone to Jerusalem to worship,
28
akawa akirejea, ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.
and on his return was sitting in his chariot reading Isaiah the prophet.
29
Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.
The Spirit said to Philip, “Go over to that chariot and stay by it.”
30
Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma?
So Philip ran up and heard the man reading Isaiah the prophet. “Do you understand what you are reading?” Philip asked.
31
Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.
“How can I,” he said, “unless someone guides me?” And he invited Philip to come up and sit with him.
32
Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.
The eunuch was reading this passage of Scripture: “He was led like a sheep to the slaughter, and as a lamb before the shearer is silent, so He did not open His mouth.
33
Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.
In His humiliation He was deprived of justice. Who can recount His descendants? For His life was removed from the earth.”
34
Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?
“Tell me,” said the eunuch, “who is the prophet talking about, himself or someone else?”
35
Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.
Then Philip began with this very Scripture and told him the good news about Jesus.
36
Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?
As they traveled along the road and came to some water, the eunuch said, “Look, here is water! What is there to prevent me from being baptized?”
37
Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
38
Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.
And he gave orders to stop the chariot. Then both Philip and the eunuch went down into the water, and Philip baptized him.
39
Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
When they came up out of the water, the Spirit of the Lord carried Philip away, and the eunuch saw him no more, but went on his way rejoicing.
40
Lakini Filipo akaonekana katika Azoto, na alipokuwa akipita akahubiri Injili katika miji yote, hata akafika Kaisaria.
But Philip appeared at Azotus and traveled through that region, preaching the gospel in all the towns until he came to Caesarea.