Matendo ya Mitume 14 Swahili & English

Listen/Download Audio
Matendo ya Mitume 14 (Swahili) Acts 14 (English)

Ikawa huko Ikonio wakaingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi; na kwa vile walivyonena, kundi kubwa la Wayahudi na la Wayunani wakaamini. Matendo ya Mitume 14:1

It happened in Iconium that they entered together into the synagogue of the Jews, and so spoke that a great multitude both of Jews and of Greeks believed.

Walakini Wayahudi wasioamini wakawataharakisha watu wa Mataifa na kuwatia nia mbaya juu ya ndugu. Matendo ya Mitume 14:2

But the disbelieving{or, disobedient} Jews stirred up and embittered the souls of the Gentiles against the brothers.

Basi wakakaa huko wakati mwingi, wakinena kwa ushujaa katika Bwana, aliyelishuhudia neno la neema yake, akiwajalia ishara na maajabu yatendeke kwa mikono yao. Matendo ya Mitume 14:3

Therefore they stayed there a long time, speaking boldly in the Lord, who testified to the word of his grace, granting signs and wonders to be done by their hands.

Lakini jamii ya watu wa mjini wakafarakana; hawa walikuwa upande wa Wayahudi, na hawa upande wa Mitume. Matendo ya Mitume 14:4

But the multitude of the city was divided. Part sided with the Jews, and part with the apostles.

Hata palipotokea shambulio la watu wa Mataifa na Wayahudi pamoja na wakubwa wao juu yao, kuwatenda jeuri na kuwapiga kwa mawe, Matendo ya Mitume 14:5

When some of both the Gentiles and the Jews, with their rulers, made a violent attempt to mistreat and stone them,

wao wakapata habari wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia, na nchi zilizo kando kando; Matendo ya Mitume 14:6

they became aware of it, and fled to the cities of Lycaonia, Lystra, Derbe, and the surrounding region.

wakakaa huko, wakiihubiri Injili. Matendo ya Mitume 14:7

There they preached the Gospel.

Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja, dhaifu wa miguu, kiwete tangu tumboni mwa mamaye, ambaye hajaenda kabisa. Matendo ya Mitume 14:8

At Lystra a certain man sat, impotent in his feet, a cripple from his mother's womb, who never had walked.

Mtu huyo alimsikia Paulo alipokuwa akinena; ambaye akamkazia macho na kuona ya kuwa ana imani ya kuponywa, Matendo ya Mitume 14:9

He was listening to Paul speaking, who, fastening eyes on him, and seeing that he had faith to be made whole,

akasema kwa sauti kuu, Simama kwa miguu yako sawasawa. Akasimama upesi akaenda. Matendo ya Mitume 14:10

said with a loud voice, "Stand upright on your feet!" He leaped up and walked.

Na makutano walipoona aliyoyafanya Paulo wakapaza sauti zao, wakisema kwa Kilikaonia, Miungu wametushukia kwa mifano ya wanadamu. Matendo ya Mitume 14:11

When the multitude saw what Paul had done, they lifted up their voice, saying in the language of Lycaonia, "The gods have come down to us in the likeness of men!"

Wakamwita Barnaba, Zeu, na Paulo, Herme, kwa sababu ndiye aliyekuwa mnenaji. Matendo ya Mitume 14:12

They called Barnabas "Jupiter," and Paul "Mercury," because he was the chief speaker.

Kuhani wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta ng'ombe na taji za maua hata malangoni, akitaka kutoa dhabihu pamoja na makutano. Matendo ya Mitume 14:13

The priest of Jupiter, whose temple was in front of their city, brought oxen and garlands to the gates, and would have made a sacrifice along with the multitudes.

Walakini mitume Barnaba na Paulo, walipopata habari, wakararua nguo zao, wakaenda mbio wakaingia katika makutano, wakipiga kelele, Matendo ya Mitume 14:14

But when the apostles, Barnabas and Paul, heard of it, they tore their clothes, and sprang into the multitude, crying out,

wakisema, Akina bwana, mbona mnafanya haya? Sisi nasi tu wanadamu hali moja na ninyi; twawahubiri habari njema, ili mgeuke na kuyaacha mambo haya ya ubatili na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; Matendo ya Mitume 14:15

"Men, why are you doing these things? We also are men of like passions with you, and bring you good news, that you should turn from these vain things to the living God, who made the sky and the earth and the sea, and all that is in them;

ambaye zamani zilizopita aliwaacha mataifa yote waende katika njia zao wenyewe. Matendo ya Mitume 14:16

who in the generations gone by allowed all the nations to walk in their own ways.

Lakini hakujiacha pasipo ushuhuda, kwa kuwa alitenda mema, akiwapeni mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha. Matendo ya Mitume 14:17

Yet he didn't leave himself without witness, in that he did good and gave you{TR reads "us" instead of "you"} rains from the sky and fruitful seasons, filling our hearts with food and gladness."

Na kwa maneno hayo wakawazuia makutano kwa shida, wasiwatolee dhabihu. Matendo ya Mitume 14:18

Even saying these things, they hardly stopped the multitudes from making a sacrifice to them.

Lakini Wayahudi wakafika toka Antiokia na Ikonio, wakawashawishi makutano hata wakampiga kwa mawe Paulo, wakamburuta nje ya mji, wakidhania ya kuwa amekwisha kufa. Matendo ya Mitume 14:19

But some Jews from Antioch and Iconium came there, and having persuaded the multitudes, they stoned Paul, and dragged him out of the city, supposing that he was dead.

Lakini wanafunzi walipokuwa wakimzunguka pande zote, akasimama, akaingia ndani ya mji; na siku ya pili yake akatoka, akaenda zake pamoja na Barnaba mpaka Derbe. Matendo ya Mitume 14:20

But as the disciples stood around him, he rose up, and entered into the city. On the next day he went out with Barnabas to Derbe.

Hata walipokwisha kuihubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia, Matendo ya Mitume 14:21

When they had preached the Gospel to that city, and had made many disciples, they returned to Lystra, Iconium, and Antioch,

wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi. Matendo ya Mitume 14:22

confirming the souls of the disciples, exhorting them to continue in the faith, and that through many afflictions we must enter into the Kingdom of God.

Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini. Matendo ya Mitume 14:23

When they had appointed elders for them in every assembly, and had prayed with fasting, they commended them to the Lord, on whom they had believed.

Wakapita kati ya Pisidia wakaingia Pamfilia. Matendo ya Mitume 14:24

They passed through Pisidia, and came to Pamphylia.

Na baada ya kuhubiri lile neno katika Perge wakatelemka mpaka Atalia. Matendo ya Mitume 14:25

When they had spoken the word in Perga, they went down to Attalia.

Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza. Matendo ya Mitume 14:26

From there they sailed to Antioch, from where they had been committed to the grace of God for the work which they had fulfilled.

Hata walipofika wakalikutanisha kanisa, wakawaeleza mambo yote aliyoyafanya Mungu pamoja nao, na ya kwamba amewafungulia Mataifa mlango wa imani. Matendo ya Mitume 14:27

When they had arrived, and had gathered the assembly together, they reported all the things that God had done with them, and that he had opened a door of faith to the Gentiles.

Wakaketi huko wakati usiokuwa mchache, pamoja na wanafunzi. Matendo ya Mitume 14:28

They stayed there with the disciples for a long time.