Matendo ya Mitume 18 Swahili & English

Listen/Download Audio
Matendo ya Mitume 18 (Swahili) Acts 18 (English)

Baada ya mambo hayo, Paulo akatoka Athene akafika Korintho. Matendo ya Mitume 18:1

After these things Paul departed from Athens, and came to Corinth.

Akamwona Myahudi mmoja, jina lake Akila, mzalia wa Ponto; naye amekuja kutoka nchi ya Italia siku za karibu, pamoja na Prisila mkewe, kwa sababu Klaudio amewaamuru Wayahudi wote watoke Rumi, naye akafikilia kwao; Matendo ya Mitume 18:2

He found a certain Jew named Aquila, a man of Pontus by race, who had recently come from Italy, with his wife Priscilla, because Claudius had commanded all the Jews to depart from Rome. He came to them,

na kwa kuwa kazi yao ya ufundi ilikuwa moja, akakaa kwao, wakafanya kazi pamoja, kwa maana walikuwa mafundi wa kushona hema. Matendo ya Mitume 18:3

and because he practiced the same trade, he lived with them and worked, for by trade they were tent makers.

Akatoa hoja zake katika sinagogi kila sabato, akajaribu kuwavuta Wayahudi na Wayunani. Matendo ya Mitume 18:4

He reasoned in the synagogue every Sabbath, and persuaded Jews and Greeks.

Hata Sila na Timotheo walipotelemka kutoka Makedonia, Paulo akasongwa sana na lile neno, akiwashuhudia Wayahudi ya kwamba Yesu ni Kristo. Matendo ya Mitume 18:5

But when Silas and Timothy came down from Macedonia, Paul was compelled by the Spirit, testifying to the Jews that Jesus was the Christ.

Walipopingamana naye na kumtukana Mungu, akakung'uta mavazi yake, akawaambia, Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu; mimi ni safi; tangu sasa nitakwenda kwa watu wa Mataifa. Matendo ya Mitume 18:6

When they opposed him and blasphemed, he shook out his clothing and said to them, "Your blood be on your own heads! I am clean. From now on, I will go to the Gentiles!"

Akaondoka huko akaingia katika nyumba ya mtu mmoja jina lake Tito Yusto, mcha Mungu, ambaye nyumba yake ilikuwa mpaka mmoja na sinagogi. Matendo ya Mitume 18:7

He departed there, and went into the house of a certain man named Justus, one who worshiped God, whose house was next door to the synagogue.

Na Krispo, mkuu wa sinagogi, akamwamini Bwana pamoja na nyumba yake yote. Wakorintho wengi waliposikia, waliamini, wakabatizwa. Matendo ya Mitume 18:8

Crispus, the ruler of the synagogue, believed in the Lord with all his house. Many of the Corinthians, when they heard, believed and were baptized.

Bwana akamwambia Paulo kwa maono usiku, Usiogope, bali nena, wala usinyamaze, Matendo ya Mitume 18:9

The Lord said to Paul in the night by a vision, "Don't be afraid, but speak and don't be silent;

kwa kuwa mimi ni pamoja nawe, wala hapana mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana mimi nina watu wengi katika mji huu. Matendo ya Mitume 18:10

for I am with you, and no one will attack you to harm you, for I have many people in this city."

Akakaa huko muda wa mwaka mmoja na miezi sita akifundisha kati yao neno la Mungu. Matendo ya Mitume 18:11

He lived there a year and six months, teaching the word of God among them.

Hata Galio alipokuwa liwali wa Akaya, Wayahudi wakamwinukia Paulo kwa nia moja, wakamleta mbele ya kiti cha hukumu, Matendo ya Mitume 18:12

But when Gallio was proconsul of Achaia, the Jews with one accord rose up against Paul and brought him before the judgment seat,

wakisema Mtu huyu huwavuta watu ili wamwabudu Mungu kinyume cha sheria. Matendo ya Mitume 18:13

saying, "This man persuades men to worship God contrary to the law."

Na Paulo alipotaka kufunua kinywa chake, Galio akawaambia Wayahudi, Kama lingekuwa jambo la dhuluma au la hila mbaya, enyi Wayahudi, ingekuwa haki mimi kuchukuliana nanyi; Matendo ya Mitume 18:14

But when Paul was about to open his mouth, Gallio said to the Jews, "If indeed it were a matter of wrong or of wicked crime, you Jews, it would be reasonable that I should bear with you;

bali ikiwa ni hoja juu ya maneno na majina na sheria yenu, liangalieni ninyi wenyewe, maana mimi sitaki kuwa mwamuzi wa mambo hayo. Matendo ya Mitume 18:15

but if they are questions about words and names and your own law, look to it yourselves. For I don't want to be a judge of these matters."

Akawafukuza waondoke mbele ya kiti cha hukumu. Matendo ya Mitume 18:16

He drove them from the judgment seat.

Nao wote wakamshika Sosthene, mkuu wa sinagogi, wakampiga mbele ya kiti cha hukumu. Wala Galio hakuyaona mambo hayo kuwa ni kitu. Matendo ya Mitume 18:17

Then all the Greeks laid hold on Sosthenes, the ruler of the synagogue, and beat him before the judgment seat. Gallio didn't care about any of these things.

Baada ya hayo Paulo akazidi kukaa huko siku nyingi, kisha akaagana na ndugu akaabiri kwenda Shamu; na Prisila na Akila wakaenda pamoja naye, alipokwisha kunyoa kichwa chake huko Kenkrea; maana alikuwa ana nadhiri. Matendo ya Mitume 18:18

Paul, having stayed after this many more days, took his leave of the brothers,{The word for "brothers" here and where the context allows may also be correctly translated "brothers and sisters" or "siblings."} and sailed from there for Syria, together with Priscilla and Aquila. He shaved his head in Cenchreae, for he had a vow.

Wakafika Efeso, akawaacha huko. Yeye mwenyewe akaingia katika sinagogi, akahojiana na Wayahudi. Matendo ya Mitume 18:19

He came to Ephesus, and he left them there; but he himself entered into the synagogue, and reasoned with the Jews.

Walipomtaka akae wakati mwingi zaidi, hakukubali; Matendo ya Mitume 18:20

When they asked him to stay with them a longer time, he declined;

bali aliagana nao, akisema, Nitarejea kwenu tena, Mungu akinijalia. Akatweka, akatoka Efeso, Matendo ya Mitume 18:21

but taking his leave of them, and saying, "I must by all means keep this coming feast in Jerusalem, but I will return again to you if God wills," he set sail from Ephesus.

na alipokwisha kushuka Kaisaria, akapanda juu, akawasalimu kanisa, kisha akatelemkia Antiokia. Matendo ya Mitume 18:22

When he had landed at Caesarea, he went up and greeted the assembly, and went down to Antioch.

Hata akiisha kukaa huko siku kadha wa kadha akaondoka, akapita kati ya nchi ya Galatia na Frigia, mji kwa mji, akiwathibitisha wanafunzi. Matendo ya Mitume 18:23

Having spent some time there, he departed, and went through the region of Galatia, and Phrygia, in order, establishing all the disciples.

Basi Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Iskanderia, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alikuwa hodari katika maandiko. Matendo ya Mitume 18:24

Now a certain Jew named Apollos, an Alexandrian by race, an eloquent man, came to Ephesus. He was mighty in the Scriptures.

Mtu huyo alikuwa amefundishwa njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikimwaka, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye alijua ubatizo wa Yohana tu. Matendo ya Mitume 18:25

This man had been instructed in the way of the Lord; and being fervent in spirit, he spoke and taught accurately the things concerning Jesus, although he knew only the baptism of John.

Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila walipomsikia wakamchukua kwao, wakamweleza njia ya Bwana kwa usahihi zaidi. Matendo ya Mitume 18:26

He began to speak boldly in the synagogue. But when Priscilla and Aquila heard him, they took him aside, and explained to him the way of God more accurately.

Na alipotaka kuvuka bahari aende mpaka Akaya, ndugu wakamhimiza, wakawaandikia wale wanafunzi wamkaribishe, naye alipofika akawasaidia sana wale waliokwisha kuamini kwa neema ya Mungu. Matendo ya Mitume 18:27

When he had determined to pass over into Achaia, the brothers encouraged him, and wrote to the disciples to receive him. When he had come, he greatly helped those who had believed through grace;

Kwa maana aliwashinda Wayahudi kabisa kabisa mbele ya watu wote, akionyesha kwa maneno ya maandiko ya kuwa Yesu ni Kristo. Matendo ya Mitume 18:28

for he powerfully refuted the Jews, publicly showing by the Scriptures that Jesus was the Christ.