Matendo ya Mitume 11 Swahili & English

Listen/Download Audio
Matendo ya Mitume 11 (Swahili) Acts 11 (English)

Basi mitume na ndugu waliokuwako katika Uyahudi wakapata habari ya kwamba watu wa Mataifa nao wamelipokea neno la Mungu. Matendo ya Mitume 11:1

Now the apostles and the brothers{The word for "brothers" here and where context allows may also be correctly translated "brothers and sisters" or "siblings."} who were in Judea heard that the Gentiles had also received the word of God.

Na Petro alipopanda kwenda Yerusalemu, wale walio wa tohara wakashindana naye, Matendo ya Mitume 11:2

When Peter had come up to Jerusalem, those who were of the circumcision contended with him,

wakisema, Uliingia kwa watu wasiotahiriwa ukala nao. Matendo ya Mitume 11:3

saying, "You went in to uncircumcised men, and ate with them!"

Petro akaanza kuwaeleza kwa taratibu, akasema, Matendo ya Mitume 11:4

But Peter began, and explained to them in order, saying,

Nalikuwa katika mji wa Yafa, nikiomba, roho yangu ikazimia, nikaona maono; chombo kinashuka, kama nguo kubwa inatelemshwa kutoka mbinguni kwa pembe zake nne, kikanifikilia. Matendo ya Mitume 11:5

"I was in the city of Joppa praying, and in a trance I saw a vision: a certain container descending, like it was a great sheet let down from heaven by four corners. It came as far as me.

Nikakitazama sana, nikifikiri, nikaona wanyama wa nchi wenye miguu minne, na wanyama wa mwituni, nao watambaao, na ndege wa angani. Matendo ya Mitume 11:6

When I had looked intently at it, I considered, and saw the four-footed animals of the earth, wild animals, creeping things, and birds of the sky.

Nikasikia na sauti ikiniambia, Ondoka, Petro, ukachinje ule. Matendo ya Mitume 11:7

I also heard a voice saying to me, 'Rise, Peter, kill and eat!'

Nikasema, Hasha, Bwana, kwa maana kitu kilicho kichafu au kilicho najisi hakijaingia kabisa kinywani mwangu. Matendo ya Mitume 11:8

But I said, 'Not so, Lord, for nothing unholy or unclean has ever entered into my mouth.'

Sauti ikanijibu mara ya pili kutoka mbinguni, Alivyovitakasa Mungu, usivinene wewe najisi. Matendo ya Mitume 11:9

But a voice answered me the second time out of heaven, 'What God has cleansed, don't you call unclean.'

Jambo hili likatendeka mara tatu, kisha vitu vyote vikavutwa tena juu mbinguni. Matendo ya Mitume 11:10

This was done three times, and all were drawn up again into heaven.

Na tazama, mara hiyo watu watatu wakasimama mbele ya nyumba tuliyokuwamo, waliotumwa kwangu kutoka Kaisaria. Matendo ya Mitume 11:11

Behold, immediately three men stood before the house where I was, having been sent from Caesarea to me.

Roho akaniambia nifuatane nao, nisione tashwishi. Ndugu hawa sita nao wakaenda pamoja nami, tukaingia katika nyumba ya mtu yule; Matendo ya Mitume 11:12

The Spirit told me to go with them, without discriminating. These six brothers also accompanied me, and we entered into the man's house.

akatueleza jinsi alivyomwona malaika aliyesimama nyumbani mwake na kumwambia, Tuma watu kwenda Yafa ukamwite Simoni aitwaye Petro, Matendo ya Mitume 11:13

He told us how he had seen the angel standing in his house, and saying to him, 'Send to Joppa, and get Simon, whose surname is Peter,

atakayekuambia maneno ambayo yatakuokoa, wewe na nyumba yako yote. Matendo ya Mitume 11:14

who will speak to you words by which you will be saved, you and all your house.'

Ikawa nilipoanza kunena, Roho Mtakatifu akawashukia kama alivyotushukia sisi mwanzo. Matendo ya Mitume 11:15

As I began to speak, the Holy Spirit fell on them, even as on us at the beginning.

Nikalikumbuka neno lile la Bwana, jinsi alivyosema, Yohana alibatiza kwa maji kweli, bali ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu. Matendo ya Mitume 11:16

I remembered the word of the Lord, how he said, 'John indeed baptized in water, but you will be baptized in the Holy Spirit.'

Basi ikiwa Mwenyezi Mungu amewapa wao karama ile ile aliyotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani niweze kumpinga Mungu? Matendo ya Mitume 11:17

If then God gave to them the same gift as us, when we believed in the Lord Jesus Christ, who was I, that I could withstand God?"

Waliposikia maneno haya wakanyamaza, wakamtukuza Mungu, wakisema, Basi, Mungu amewajalia hata mataifa nao toba liletalo uzima. Matendo ya Mitume 11:18

When they heard these things, they held their peace, and glorified God, saying, "Then God has also granted to the Gentiles repentance to life!"

Basi wale waliotawanyika kwa sababu ya ile dhiki iliyotukia kwa habari ya Stefano, wakasafiri hata Foinike na Kipro na Antiokia, wasilihubiri lile neno ila kwa Wayahudi peke yao. Matendo ya Mitume 11:19

They therefore who were scattered abroad by the oppression that arose about Stephen traveled as far as Phoenicia, Cyprus, and Antioch, speaking the word to no one except to Jews only.

Lakini baadhi ya hao walikuwa watu wa Kipro na Kirene, nao walipofika Antiokia wakasema na Wayahudi wa Kiyunani, wakihubiri habari njema za Bwana Yesu. Matendo ya Mitume 11:20

But there were some of them, men of Cyprus and Cyrene, who, when they had come to Antioch, spoke to the Greeks, preaching the Lord Jesus.

Mkono wa Bwana ukawa pamoja nao, watu wengi wakaamini, wakamwelekea Bwana. Matendo ya Mitume 11:21

The hand of the Lord was with them, and a great number believed and turned to the Lord.

Habari hizo za watu hao zikafika masikioni mwa kanisa lililokuwako katika Yerusalemu; wakamtuma Barnaba, aende hata Antiokia. Matendo ya Mitume 11:22

The report concerning them came to the ears of the assembly which was in Jerusalem. They sent out Barnabas to go as far as Antioch,

Naye, alipokwisha kufika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo. Matendo ya Mitume 11:23

who, when he had come, and had seen the grace of God, was glad. He exhorted them all, that with purpose of heart they should remain near to the Lord.

Maana alikuwa mtu mwema amejaa Roho Mtakatifu na imani; watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana. Matendo ya Mitume 11:24

For he was a good man, and full of the Holy Spirit and of faith, and many people were added to the Lord.

Kisha akatoka akaenda Tarso kumtafuta Sauli; Matendo ya Mitume 11:25

Barnabas went out to Tarsus to look for Saul.

hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia. Matendo ya Mitume 11:26

When he had found him, he brought him to Antioch. It happened, that for a whole year they were gathered together with the assembly, and taught many people. The disciples were first called Christians in Antioch.

Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia. Matendo ya Mitume 11:27

Now in these days, prophets came down from Jerusalem to Antioch.

Na tulipokusanyika akasimama mmoja wao, jina lake Agabo, akaonyesha kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itakuja karibu katika dunia nzima, nayo ikatukia katika siku za Klaudio. Matendo ya Mitume 11:28

One of them named Agabus stood up, and indicated by the Spirit that there should be a great famine all over the world, which also happened in the days of Claudius.

Na wale wanafunzi, kila mtu kwa kadiri ya alivyofanikiwa, wakaazimu kupeleka msaada kwa ndugu zao waliokaa Uyahudi. Matendo ya Mitume 11:29

As any of the disciples had plenty, each determined to send relief to the brothers who lived in Judea;

Wakafanya hivyo, wakawapelekea wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli. Matendo ya Mitume 11:30

which they also did, sending it to the elders by the hands of Barnabas and Saul.