Matendo ya Mitume 1 Swahili & English

Listen/Download Audio
Matendo ya Mitume 1 (Swahili) Acts 1 (English)

Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, Theofilo, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, Matendo ya Mitume 1:1

The first book I wrote, Theophilus, concerned all that Jesus began both to do and to teach,

hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua; Matendo ya Mitume 1:2

until the day in which he was received up, after he had given commandment through the Holy Spirit to the apostles whom he had chosen.

wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu. Matendo ya Mitume 1:3

To these he also showed himself alive after he suffered, by many proofs, appearing to them over a period of forty days, and speaking about God's Kingdom.

Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; Matendo ya Mitume 1:4

Being assembled together with them, he charged them, "Don't depart from Jerusalem, but wait for the promise of the Father, which you heard from me.

ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache. Matendo ya Mitume 1:5

For John indeed baptized in water, but you will be baptized in the Holy Spirit not many days from now."

Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? Matendo ya Mitume 1:6

Therefore, when they had come together, they asked him, "Lord, are you now restoring the kingdom to Israel?"

Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Matendo ya Mitume 1:7

He said to them, "It isn't for you to know times or seasons which the Father has set within His own authority.

Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi. Matendo ya Mitume 1:8

But you will receive power when the Holy Spirit has come upon you. You will be witnesses to me in Jerusalem, in all Judea and Samaria, and to the uttermost parts of the earth."

Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao. Matendo ya Mitume 1:9

When he had said these things, as they were looking, he was taken up, and a cloud received him out of their sight.

Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, Matendo ya Mitume 1:10

While they were looking steadfastly into the sky as he went, behold, two men stood by them in white clothing,

wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni. Matendo ya Mitume 1:11

who also said, "You men of Galilee, why do you stand looking into the sky? This Jesus, who was received up from you into the sky will come back in the same way as you saw him going into the sky."

Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato. Matendo ya Mitume 1:12

Then they returned to Jerusalem from the mountain called Olivet, which is near Jerusalem, a Sabbath day's journey away.

Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo. Matendo ya Mitume 1:13

When they had come in, they went up into the upper room, where they were staying; that is Peter, John, James, Andrew, Philip, Thomas, Bartholomew, Matthew, James the son of Alphaeus, Simon the Zealot, and Judas the son of James.

Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake. Matendo ya Mitume 1:14

All these with one accord continued steadfastly in prayer and supplication, along with the women, and Mary the mother of Jesus, and with his brothers.

Siku zile akasimama Petro kati ya hao ndugu (jumla ya majina ilipata mia na ishirini), akasema, Matendo ya Mitume 1:15

In these days, Peter stood up in the midst of the disciples (and the number of names was about one hundred twenty), and said,

Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi, katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu; Matendo ya Mitume 1:16

"Brothers, it was necessary that this Scripture should be fulfilled, which the Holy Spirit spoke before by the mouth of David concerning Judas, who was guide to those who took Jesus.

kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii. Matendo ya Mitume 1:17

For he was numbered with us, and received his portion in this ministry.

(Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka. Matendo ya Mitume 1:18

Now this man obtained a field with the reward for his wickedness, and falling headlong, his body burst open, and all his intestines gushed out.

Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.) Matendo ya Mitume 1:19

It became known to everyone who lived in Jerusalem that in their language that field was called 'Akeldama,' that is, 'The field of blood.'

Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa, Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo; Matendo ya Mitume 1:20

For it is written in the book of Psalms, 'Let his habitation be made desolate, Let no one dwell therein,' and, 'Let another take his office.'

Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu, Matendo ya Mitume 1:21

Of the men therefore who have accompanied us all the time that the Lord Jesus went in and out among us,

kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi. Matendo ya Mitume 1:22

beginning from the baptism of John, to the day that he was received up from us, of these one must become a witness with us of his resurrection."

Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya. Matendo ya Mitume 1:23

They put forward two, Joseph called Barsabbas, who was surnamed Justus, and Matthias.

Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili, Matendo ya Mitume 1:24

They prayed, and said, "You, Lord, who know the hearts of all men, show which one of these two you have chosen

ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. Matendo ya Mitume 1:25

to take part in this ministry and apostleship from which Judas fell away, that he might go to his own place."

Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja. Matendo ya Mitume 1:26

They drew lots for them, and the lot fell on Matthias, and he was numbered with the eleven apostles.