Yeremia 49 Swahili & English
Listen/Download AudioYeremia 49 (Swahili) | Jeremiah 49 (English) |
---|---|
Habari za wana wa Amoni. Bwana asema hivi, Je, Israeli hana wana? Je! Hana mrithi? Basi, mbona Malkamu anamiliki Gadi, na watu wake wanakaa katika miji yake? Yeremia 49:1 |
Of the children of Ammon. Thus says Yahweh: Has Israel no sons? has he no heir? why then does Malcam possess Gad, and his people well in the cities of it? |
Basi, kwa sababu hiyo, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakaposikizisha mshindo wa vita juu ya Raba, mji wa Amoni, nao utakuwa magofu ya ukiwa, na binti zake watateketezwa kwa moto; ndipo Israeli watawamiliki wao waliokuwa wakimmiliki, asema Bwana. Yeremia 49:2 |
Therefore, behold, the days come, says Yahweh, that I will cause an alarm of war to be heard against Rabbah of the children of Ammon; and it shall become a desolate heap, and her daughters shall be burned with fire: then shall Israel possess those who did possess him, says Yahweh. |
Piga yowe, Ee Heshboni, Kwa maana Ai umeangamizwa; Lieni, enyi binti za Raba, Mjivike nguo za magunia; Ombolezeni, mkipiga mbio Huko na huko kati ya maboma; Maana Malkamu atakwenda kuhamishwa, Makuhani wake na wakuu wake pamoja. Yeremia 49:3 |
Wail, Heshbon, for Ai is laid waste; cry, you daughters of Rabbah, gird you with sackcloth: lament, and run back and forth among the fences; for Malcam shall go into captivity, his priests and his princes together. |
Mbona unajisifu kwa sababu ya mabonde, bonde lako litiririkalo, Ee binti mwenye kuasi? Utumainiaye hazina zako, ukisema, Ni nani atakayenijilia? Yeremia 49:4 |
Why glory you in the valleys, your flowing valley, backsliding daughter? who trusted in her treasures, [saying], Who shall come to me? |
Tazama, nitaleta hofu juu yako, asema Bwana, Bwana wa majeshi, itakayotoka kwa wote wakuzungukao; nanyi mtafukuzwa nje, kila mtu mbali kabisa, wala hapana mtu wa kuwakusanya wapoteao. Yeremia 49:5 |
Behold, I will bring a fear on you, says the Lord, Yahweh of Hosts, from all who are round about you; and you shall be driven out every man right forth, and there shall be none to gather together the fugitives. |
Lakini baada ya hayo nitawarudisha wana wa Amoni walio utumwani, asema Bwana. Yeremia 49:6 |
But afterward I will bring back the captivity of the children of Ammon, says Yahweh. |
Habari za Edomu. Bwana wa majeshi asema hivi, Je! Hapana tena hekima katika Temani? Mashauri yamewapotea wenye busara? Je! Imetoweka hekima yao? Yeremia 49:7 |
Of Edom. Thus says Yahweh of Hosts: Is wisdom no more in Teman? is counsel perished from the prudent? is their wisdom vanished? |
Kimbieni, rudini nyuma, kaeni chini sana, enyi mnaokaa Dedani; maana nitaleta msiba wa Esau juu yake, wakati nitakapomwangalia. Yeremia 49:8 |
Flee you, turn back, dwell in the depths, inhabitants of Dedan; for I will bring the calamity of Esau on him, the time that I shall visit him. |
Je! Kama wachuma zabibu wangekujia, wasingeacha zabibu ziokotwe? Kama wangekujia wevi usiku, wasingeharibu hata watakapopata vya kutosha? Yeremia 49:9 |
If grape-gatherers came to you, would they not leave some gleaning grapes? if thieves by night, wouldn't they destroy until they had enough? |
Lakini nimemwacha Esau hana kitu, nimepafunua mahali pake pa siri, wala hataweza kujificha; kizazi chake kimeangamizwa, na ndugu zake, na jirani zake, naye mwenyewe hayuko. Yeremia 49:10 |
But I have made Esau bare, I have uncovered his secret places, and he shall not be able to hide himself: his seed is destroyed, and his brothers, and his neighbors; and he is no more. |
Waache watoto wako wasio na baba, mimi nitawahifadhi hai, na wajane wako na wanitumaini mimi. Yeremia 49:11 |
Leave your fatherless children, I will preserve them alive; and let your widows trust in me. |
Maana Bwana asema hivi, Tazama, wale wasioandikiwa kunywea kikombe, watakinywea, ni hakika; na wewe je! U mtu ambaye hataadhibiwa kabisa? Hukosi utaadhibiwa, naam, kunywa utakunywa. Yeremia 49:12 |
For thus says Yahweh: Behold, they to whom it didn't pertain to drink of the cup shall assuredly drink; and are you he who shall altogether go unpunished? you shall not go unpunished, but you shall surely drink. |
Kwa maana nimeapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba Bozra utakuwa ajabu, na aibu, na ukiwa, na laana; na miji yake yote itakuwa ukiwa wa daima. Yeremia 49:13 |
For I have sworn by myself, says Yahweh, that Bozrah shall become an astonishment, a reproach, a waste, and a curse; and all the cities of it shall be perpetual wastes. |
Nimepata habari kwa Bwana, Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, Akisema, Jikusanyeni, mkaujie, Mkainuke kwenda vitani. Yeremia 49:14 |
I have heard news from Yahweh, and an ambassador is sent among the nations, [saying], Gather yourselves together, and come against her, and rise up to the battle. |
Maana nimekufanya mdogo kati ya mataifa, Na kudharauliwa katika watu. Yeremia 49:15 |
For, behold, I have made you small among the nations, and despised among men. |
Katika habari za kuogofya kwako, Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Ushikaye kilele cha milima; Ujapofanya kioto chako juu sana kama tai, Nitakushusha kutoka huko; asema Bwana. Yeremia 49:16 |
As for your terror, the pride of your heart has deceived you, O you who dwell in the clefts of the rock, who hold the height of the hill: though you should make your nest as high as the eagle, I will bring you down from there, says Yahweh. |
Na Edomu atakuwa ajabu; kila mtu apitaye atashangaa, na kuzomea, kwa sababu ya mapigo yake yote. Yeremia 49:17 |
Edom shall become an astonishment: everyone who passes by it shall be astonished, and shall hiss at all the plagues of it. |
Kama vile vilivyotokea wakati wa kuangushwa Sodoma na Gomora, na miji iliyokuwa karibu nayo, asema Bwana; hapana mtu atakayekaa huko, wala hapana mwanadamu atakayekaa huko kama mgeni akaavyo. Yeremia 49:18 |
As in the overthrow of Sodom and Gomorrah and the neighbor cities of it, says Yahweh, no man shall dwell there, neither shall any son of man sojourn therein. |
Angalia, atapanda kama simba toka kiburi cha Yordani juu ya malisho yasiyonyauka; lakini nitamkimbiza ghafula ayaache; na yeye aliye mteule nitamweka juu yake; maana ni nani aliye kama mimi? Tena ni nani atakayeniandikia muda? Tena ni mchungaji yupi atakayesimama mbele zangu? Yeremia 49:19 |
Behold, he shall come up like a lion from the pride of the Jordan against the strong habitation: for I will suddenly make them run away from it; and whoever is chosen, him will I appoint over it: for who is like me? and who will appoint me a time? and who is the shepherd who will stand before me? |
Basi, lisikieni shauri la Bwana; Alilolifanya juu ya Edomu; Na makusudi yake aliyoyakusudia Juu yao wakaao Temani; Hakika watawaburura, naam, wadogo wa kundi; Hakika malisho yao yatafadhaika kwa ajili yao. Yeremia 49:20 |
Therefore hear the counsel of Yahweh, that he has taken against Edom; and his purposes, that he has purposed against the inhabitants of Teman: Surely they shall drag them away, [even] the little ones of the flock; surely he shall make their habitation desolate over them. |
Nchi yatetemeka kwa sauti ya kuanguka kwao; Kuna kilio, sauti yake yasikiwa katika Bahari ya Shamu. Yeremia 49:21 |
The earth trembles at the noise of their fall; there is a cry, the noise which is heard in the Red Sea. |
Tazama, atapanda na kuruka kama tai, na kutandaza mabawa yake juu ya Bozra; na mioyo ya mashujaa wa Edomu siku hiyo itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wake. Yeremia 49:22 |
Behold, he shall come up and fly as the eagle, and spread out his wings against Bozrah: and the heart of the mighty men of Edom at that day shall be as the heart of a woman in her pangs. |
Habari za Dameski. Hamathi umetahayarika, na Arpadi pia; Maana wamesikia habari mbaya; Wameyeyuka kabisa; Huzuni iko baharini, haiwezi kutulia. Yeremia 49:23 |
Of Damascus. Hamath is confounded, and Arpad; for they have heard evil news, they are melted away: there is sorrow on the sea; it can't be quiet. |
Dameski umedhoofika; Umejigeuza kukimbia; tetemko limeushika; Dhiki na huzuni zimeupata, Kama za mwanamke katika utungu wake. Yeremia 49:24 |
Damascus has grown feeble, she turns herself to flee, and trembling has seized on her: anguish and sorrows have taken hold of her, as of a woman in travail. |
Imekuwaje mji wa sifa haukuachwa, mji wa furaha yangu? Yeremia 49:25 |
How is the city of praise not forsaken, the city of my joy? |
Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika njia kuu zake, na watu wote wa vita watanyamazishwa katika siku hiyo, asema Bwana wa majeshi. Yeremia 49:26 |
Therefore her young men shall fall in her streets, and all the men of war shall be brought to silence in that day, says Yahweh of Hosts. |
Nami nitawasha moto katika ukuta wa Dameski, nao utayateketeza majumba ya Ben-hadadi. Yeremia 49:27 |
I will kindle a fire in the wall of Damascus, and it shall devour the palaces of Ben Hadad. |
Habari za Kedari, na za falme za Hazori, ambazo Nebukadreza, mfalme wa Babeli, alizipiga. Bwana asema hivi, Ondokeni, pandeni hata Kedari, mkawateke nyara wana wa mashariki. Yeremia 49:28 |
Of Kedar, and of the kingdoms of Hazor, which Nebuchadrezzar king of Babylon struck. Thus says Yahweh: Arise you, go up to Kedar, and destroy the children of the east. |
Hema zao na makundi yao watayatwaa; watachukulia mbali mapazia yao kwa faida yao wenyewe, na vyombo vyao vyote, na ngamia zao; nao watawapigia kelele wakisema, Hofu ziko pande zote. Yeremia 49:29 |
Their tents and their flocks shall they take; they shall carry away for themselves their curtains, and all their vessels, and their camels; and they shall cry to them, Terror on every side! |
Kimbieni ninyi, enendeni mbali mkitanga-tanga, kaeni chini sana, enyi mkaao Hazori, asema Bwana; maana Nebukadreza, mfalme wa Babeli, amefanya shauri juu yenu, naye amekusudia neno juu yenu. Yeremia 49:30 |
Flee you, wander far off, dwell in the depths, you inhabitants of Hazor, says Yahweh; for Nebuchadrezzar king of Babylon has taken counsel against you, and has conceived a purpose against you. |
Ondokeni, pandeni hata taifa lililo katika hali ya raha, likaalo bila kuhangaika, asema Bwana; wasio na malango wala makomeo, wakaao peke yao. Yeremia 49:31 |
Arise, go up to a nation that is at ease, that dwells without care, says Yahweh; that have neither gates nor bars, that dwell alone. |
Na ngamia zao watakuwa mateka, na wingi wa makundi yao utakuwa nyara; nami nitawatawanya hata pepo zote watu wale wanyoao denge; nami nitaleta msiba wao toka pande zao zote, asema Bwana. Yeremia 49:32 |
Their camels shall be a booty, and the multitude of their cattle a spoil: and I will scatter to all winds those who have the corners [of their hair] cut off; and I will bring their calamity from every side of them, says Yahweh. |
Na Hazori utakuwa kao la mbwa-mwitu; ukiwa milele; hapana mtu atakayekaa huko, wala hapana mwanadamu atakayekaa huko kama mgeni akaavyo. Yeremia 49:33 |
Hazor shall be a dwelling-place of jackals, a desolation forever: no man shall dwell there, neither shall any son of man sojourn therein. |
Neno la Bwana lililomjia Yeremia, nabii, juu ya Elamu, mwanzo wa kumiliki kwake Sedekia, mfalme wa Yuda, kusema, Yeremia 49:34 |
The word of Yahweh that came to Jeremiah the prophet concerning Elam, in the beginning of the reign of Zedekiah king of Judah, saying, |
Bwana wa majeshi asema hivi, Tazama nitauvunja upinde wa Elamu, ulio mkuu katika nguvu zao. Yeremia 49:35 |
Thus says Yahweh of Hosts: Behold, I will break the bow of Elam, the chief of their might. |
Na juu ya Elamu nitazileta pepo nne, toka pembe nne za mbinguni, nami nitawatawanya hata pepo nne zote, wala hapana taifa ambalo hawatalifikilia watu wa Elamu waliofukuzwa. Yeremia 49:36 |
On Elam will I bring the four winds from the four quarters of the sky, and will scatter them toward all those winds; and there shall be no nation where the outcasts of Elam shall not come. |
Nami nitawafadhaisha watu wa Elamu mbele ya adui zao, na mbele ya hao wanaowatafuta roho zao; nami nitawaletea mabaya, naam, hasira yangu kali, asema Bwana; nami nitautuma upanga uwafuatie, hata nitakapowaangamiza; Yeremia 49:37 |
I will cause Elam to be dismayed before their enemies, and before those who seek their life; and I will bring evil on them, even my fierce anger, says Yahweh; and I will send the sword after them, until I have consumed them; |
nami nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu, nami nitawaharibu, mfalme na wakuu, watoke huko, asema Bwana. Yeremia 49:38 |
and I will set my throne in Elam, and will destroy from there king and princes, says Yahweh. |
Lakini itakuwa, katika siku za mwisho, nitawarudisha wafungwa wa Elamu, asema Bwana. Yeremia 49:39 |
But it shall happen in the latter days, that I will bring back the captivity of Elam, says Yahweh. |