Waamuzi 16 Swahili & English

Listen/Download Audio
Waamuzi 16 (Swahili) Judges 16 (English)

Samsoni akaenda Gaza, akaona huko mwanamke kahaba, akaingia kwake. Waamuzi 16:1

Samson went to Gaza, and saw there a prostitute, and went in to her.

Watu wa Gaza wakaambiwa, ya kwamba, huyo Samsoni amekuja huku. Wakamzingira, wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji, wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, Na tungoje mpaka mapambazuko, ndipo tutamwua. Waamuzi 16:2

[It was told] the Gazites, saying, Samson is come here. They compassed him in, and laid wait for him all night in the gate of the city, and were quiet all the night, saying, [Let be] until morning light, then we will kill him.

Basi Samsoni akalala hata usiku wa manane, akaondoka katikati ya usiku, akaishika milango ya lango la mji, na miimo yake miwili, akaing'oa pamoja na komeo lake, akajitwika mabegani, akavichukua hata kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni. Waamuzi 16:3

Samson lay until midnight, and arose at midnight, and laid hold of the doors of the gate of the city, and the two posts, and plucked them up, bar and all, and put them on his shoulders, and carried them up to the top of the mountain that is before Hebron.

Ikawa baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki, jina lake akiitwa Delila. Waamuzi 16:4

It came to pass afterward, that he loved a woman in the valley of Sorek, whose name was Delilah.

Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja. Waamuzi 16:5

The lords of the Philistines came up to her, and said to her, Entice him, and see in which his great strength lies, and by what means we may prevail against him, that we may bind him to afflict him: and we will each give you of us eleven hundred [pieces] of silver.

Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe. Waamuzi 16:6

Delilah said to Samson, Tell me, Please, in which your great strength lies, and with which you might be bound to afflict you.

Samsoni akamwambia, Wakinifunga kwa kamba mbichi saba ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu. Waamuzi 16:7

Samson said to her, If they bind me with seven green cords that were never dried, then shall I become weak, and be as another man.

Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamletea kamba mbichi saba zisizokauka, naye akamfunga nazo. Waamuzi 16:8

Then the lords of the Philistines brought up to her seven green cords which had not been dried, and she bound him with them.

Na yule mwanamke alikuwa na watu katika chumba cha ndani, wakimwotea. Basi akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Ndipo akazikata zile kamba kama vile uzi wa pamba ukatwavyo ukiguswa na moto. Basi hiyo asili ya nguvu zake haikujulikana. Waamuzi 16:9

Now she had liers-in-wait abiding in the inner chamber. She said to him, The Philistines are on you, Samson. He broke the cords, as a string of tow is broken when it touches the fire. So his strength was not known.

Delila akamwambia Samsoni, Tazama, umenidhihaki, na kuniambia uongo; sasa tafadhali, niambie, waweza kufungwa kwa kitu gani? Waamuzi 16:10

Delilah said to Samson, Behold, you have mocked me, and told me lies: now tell me, Please, with which you might be bound.

Akamwambia Wakinifunga tu kwa kamba mpya ambazo mtu hakufanya kazi nazo, hapo ndipo nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu. Waamuzi 16:11

He said to her, If they only bind me with new ropes with which no work has been done, then shall I become weak, and be as another man.

Basi Delila akatwaa kamba mpya akamfunga nazo, akamwambia, Wafilisti wanakujia, Samsoni. Na wale wenye kuotea walikuwa katika chumba cha ndani. Naye akazikata, akazitupa kutoka mikononi mwake kama uzi. Waamuzi 16:12

So Delilah took new ropes, and bound him therewith, and said to him, The Philistines are on you, Samson. The liers-in-wait were abiding in the inner chamber. He broke them off his arms like a thread.

Delila akamwambia Samsoni, Hata sasa umenidhihaki, umeniambia maneno ya uongo; niambie sasa, waweza kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia, Ukivifuma hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo. Waamuzi 16:13

Delilah said to Samson, Hitherto you have mocked me, and told me lies: tell me with which you might be bound. He said to her, If you weave the seven locks of my head with the web.

Basi akazifunga kwa msumari, akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Naye akaamka usingizini, akaung'oa ule msumari, na ule mtande. Waamuzi 16:14

She fastened it with the pin, and said to him, The Philistines are on you, Samson. He awakened out of his sleep, and plucked away the pin of the beam, and the web.

Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi. Waamuzi 16:15

She said to him, How can you say, I love you, when your heart is not with me? you have mocked me these three times, and have not told me in which your great strength lies.

Ikawa, kwa vile alivyomsumbua kwa maneno yake kila siku, na kumwudhi, roho yake ikadhikika hata kufa. Waamuzi 16:16

It happened, when she pressed him daily with her words, and urged him, that his soul was vexed to death.

Ndipo alipomwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akamwambia, Wembe haukupita juu ya kichwa changu kamwe; maana mimi nimekuwa Mnadhiri wa Mungu, tangu tumboni mwa mama yangu; nikinyolewa, ndipo nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu. Waamuzi 16:17

He told her all his heart, and said to her, "No razor has ever come on my head; for I have been a Nazirite to God from my mother's womb. If I am shaved, then my strength will go from me, and I will become weak, and be like any other man."

Delila alipoona ya kuwa amemwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akatuma mtu akawaita wakuu wa Wafilisti, akisema, Njoni huku mara hii tu, maana ameniambia yote aliyo nayo moyoni mwake. Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamwendea wakachukua ile fedha mikononi mwao. Waamuzi 16:18

When Delilah saw that he had told her all his heart, she sent and called for the lords of the Philistines, saying, Come up this once, for he has told me all his heart. Then the lords of the Philistines came up to her, and brought the money in their hand.

Naye akamlaza usingizi magotini pake. Kisha akamwita mtu akavinyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake; akaanza kumsumbua, nguvu zake zikamtoka. Waamuzi 16:19

She made him sleep on her knees; and she called for a man, and shaved off the seven locks of his head; and she began to afflict him, and his strength went from him.

Kisha akasema, Samsoni, Wafilisti wanakujia. Akaamka katika usingizi wake, akasema, Nitakwenda nje kama siku nyingine, na kujinyosha. Lakini hakujua ya kuwa Bwana amemwacha. Waamuzi 16:20

She said, The Philistines are on you, Samson. He awoke out of his sleep, and said, I will go out as at other times, and shake myself free. But he didn't know that Yahweh had departed from him.

Wafilisti wakamkamata, wakamng'oa macho; wakatelemka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba; naye alikuwa akisaga ngano katika gereza. Waamuzi 16:21

The Philistines laid hold on him, and put out his eyes; and they brought him down to Gaza, and bound him with fetters of brass; and he did grind in the prison-house.

Lakini zile nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa kwake. Waamuzi 16:22

However the hair of his head began to grow again after he was shaved.

Kisha wakuu wa Wafilisti wakakusanyika ili kumtolea sadaka Dagoni mungu wao, na kufurahi; maana walisema, Mungu wetu amemtia Samsoni adui wetu mikononi mwetu. Waamuzi 16:23

The lords of the Philistines gathered them together to offer a great sacrifice to Dagon their god, and to rejoice; for they said, Our god has delivered Samson our enemy into our hand.

Na hao watu walipomwona wakamhimidi mungu wao, maana walisema, Mungu wetu amemtia mikononi mwetu huyu adui wetu, aliyeiharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu. Waamuzi 16:24

When the people saw him, they praised their god; for they said, Our god has delivered into our hand our enemy, and the destroyer of our country, who has slain many of us.

Ikawa mioyo yao iliposhangilia, wakasema, Mwiteni Samsoni, ili atufanyie michezo. Basi wakamwita Samsoni atoke gerezani, akacheze mbele yao wakamweka katikati ya nguzo mbili. Waamuzi 16:25

It happened, when their hearts were merry, that they said, Call for Samson, that he may make us sport. They called for Samson out of the prison-house; and he made sport before them. They set him between the pillars:

Samsoni akamwambia yule kijana aliyemshika mkono, Niache nizipapase nguzo ambazo nyumba hii inazikalia, nipate kuzitegemea. Waamuzi 16:26

and Samson said to the boy who held him by the hand, Allow me that I may feel the pillars whereupon the house rests, that I may lean on them.

Basi nyumba ile ilikuwa imejaa watu waume kwa wake; na wakuu wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na juu ya dari palikuwa na watu elfu tatu waume kwa wake waliokuwa wakitazama, wakati Samsoni alipocheza. Waamuzi 16:27

Now the house was full of men and women; and all the lords of the Philistines were there; and there were on the roof about three thousand men and women, who saw while Samson made sport.

Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili. Waamuzi 16:28

Samson called to Yahweh, and said, Lord Yahweh, remember me, Please, and strengthen me, Please, only this once, God, that I may be at once avenged of the Philistines for my two eyes.

Kisha Samsoni akazishika nguzo mbili za katikati ambazo nyumba ile ilikaa juu yake, akazitegemea, moja kwa mkono wake wa kuume na moja kwa mkono wake wa kushoto. Waamuzi 16:29

Samson took hold of the two middle pillars on which the house rested, and leaned on them, the one with his right hand, and the other with his left.

Samsoni akasema; Na nife pamoja na hawa Wafilisti. Akainama kwa nguvu zake zote; ile nyumba ikawaangukia hao wakuu, na watu wote waliokuwa ndani yake. Basi wale watu aliowaua wakati wa kufa kwake walikuwa wengi kuliko wale aliowaua wakati wa uhai wake. Waamuzi 16:30

Samson said, Let me die with the Philistines. He bowed himself with all his might; and the house fell on the lords, and on all the people who were therein. So the dead that he killed at his death were more than those who he killed in his life.

Ndipo ndugu zake, na watu wote wa nyumba ya baba yake wakatelemka, wakamtwaa wakamchukua, wakamzika kati ya Sora na Eshtaoli, katika kiwanja cha kuzikia cha Manoa baba yake. Naye alikuwa mwamuzi wa Israeli muda wa miaka ishirini. Waamuzi 16:31

Then his brothers and all the house of his father came down, and took him, and brought him up, and buried him between Zorah and Eshtaol in the burying-place of Manoah his father. He judged Israel twenty years.