Waamuzi 10 Swahili & English

Listen/Download Audio
Waamuzi 10 (Swahili) Judges 10 (English)

Baada yake Abimeleki, akainuka Tola mwana wa Pua, mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, kuwaokoa Israeli; naye alikuwa akikaa Shamiri, katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu. Waamuzi 10:1

After Abimelech there arose to save Israel Tola the son of Puah, the son of Dodo, a man of Issachar; and he lived in Shamir in the hill-country of Ephraim.

Huyo akawa mwamuzi wa Israeli muda wa miaka ishirini na mitatu, akafa, akazikwa katika Shamiri. Waamuzi 10:2

He judged Israel twenty-three years, and died, and was buried in Shamir.

Baada yake huyo akainuka Yairi, Mgileadi; naye akawa mwamuzi wa Israeli muda wa miaka ishirini na miwili. Waamuzi 10:3

After him arose Jair, the Gileadite; and he judged Israel twenty-two years.

Huyo alikuwa na wana thelathini waliokuwa wakipanda wana-punda thelathini, nao walikuwa na miji thelathini, ambayo inaitwa Hawoth-yairi hata hivi leo, nayo iko katika nchi ya Gileadi. Waamuzi 10:4

He had thirty sons who rode on thirty donkey colts, and they had thirty cities, which are called Havvoth Jair to this day, which are in the land of Gilead.

Yairi akafa, akazikwa huko Kamoni. Waamuzi 10:5

Jair died, and was buried in Kamon.

Kisha wana wa Israeli walifanya tena yaliyo maovu mbele za macho ya Bwana, wakawatumikia Mabaali, na Maashtorethi, na miungu ya Shamu, na miungu ya Sidoni, na miungu ya Moabu, na miungu ya wana wa Amoni, na miungu ya Wafilisti; nao wakamwacha Bwana, wala hawakumtumikia yeye. Waamuzi 10:6

The children of Israel again did that which was evil in the sight of Yahweh, and served the Baals, and the Ashtaroth, and the gods of Syria, and the gods of Sidon, and the gods of Moab, and the gods of the children of Ammon, and the gods of the Philistines; and they forsook Yahweh, and didn't serve him.

Hasira za Bwana ziliwaka juu ya Israeli, akawauza na kuwaua mikononi mwa Wafilisti, na mikononi mwa wana wa Amoni. Waamuzi 10:7

The anger of Yahweh was kindled against Israel, and he sold them into the hand of the Philistines, and into the hand of the children of Ammon.

Nao wakawasumbua na kuwaonea wana wa Israeli mwaka huo; waliwaonea wana wa Israeli wote waliokuwa ng'ambo ya pili ya Yordani katika nchi ya Waamori, iliyoko huko Gileadi, muda wa miaka kumi na minane. Waamuzi 10:8

They vexed and oppressed the children of Israel that year: eighteen years [oppressed they] all the children of Israel that were beyond the Jordan in the land of the Amorites, which is in Gilead.

Wana wa Amoni nao wakavuka Yordani ili wapigane na Yuda, na kupigana na Benyamini, na nyumba ya Efraimu; basi hivyo Israeli walikuwa wanasumbuliwa sana. Waamuzi 10:9

The children of Ammon passed over the Jordan to fight also against Judah, and against Benjamin, and against the house of Ephraim; so that Israel was sore distressed.

Ndipo wana wa Israeli wakamlilia Bwana, wakisema, Sisi tumekufanyia dhambi, kwa sababu tumemwacha Mungu wetu, na kuyatumikia Mabaali. Waamuzi 10:10

The children of Israel cried to Yahweh, saying, We have sinned against you, even because we have forsaken our God, and have served the Baals.

Naye Bwana akawaambia wana wa Israeli, Je! Sikuwaokoa ninyi na hao Wamisri, na Waamori, na wana wa Amoni, na Wafilisti? Waamuzi 10:11

Yahweh said to the children of Israel, Didn't I save you from the Egyptians, and from the Amorites, from the children of Ammon, and from the Philistines?

Hao Wasidoni nao, na Waamaleki, na Wamaoni, waliwaonea, nanyi mlinililia, nami niliwaokoa na mikono yao. Waamuzi 10:12

The Sidonians also, and the Amalekites, and the Maonites, did oppress you; and you cried to me, and I saved you out of their hand.

Lakini mmeniacha mimi, na kuitumikia miungu mingine; basi kwa ajili ya hayo mimi sitawaokoa tena. Waamuzi 10:13

Yet you have forsaken me, and served other gods: therefore I will save you no more.

Haya, endeni mkaililie hiyo miungu mliyoichagua; na hiyo iwaokoe wakati wa kusumbuka kwenu. Waamuzi 10:14

Go and cry to the gods which you have chosen; let them save you in the time of your distress.

Wana wa Israeli wakamwambia Bwana Tumefanya dhambi; utufanyie yote uyaonayo kuwa ni mema; lakini tuokoe, twakusihi, siku hii ya leo, haya tu. Waamuzi 10:15

The children of Israel said to Yahweh, We have sinned: do you to us whatever seems good to you; only deliver us, we pray you, this day.

Nao wakaiondoa hiyo miungu ya kigeni iliyokuwa kati yao, nao wakamtumikia Bwana; na roho yake ilihuzunika kwa sababu ya msiba wa Israeli. Waamuzi 10:16

They put away the foreign gods from among them, and served Yahweh; and his soul was grieved for the misery of Israel.

Wakati huo wana wa Amoni walikutana pamoja, wakapanga marago huko Gileadi. Wana wa Israeli nao wakajikusanya wakapanga marago Mispa. Waamuzi 10:17

Then the children of Ammon were gathered together, and encamped in Gilead. The children of Israel assembled themselves together, and encamped in Mizpah.

Na hao watu, wakuu wa Gileadi, wakaambiana wao kwa wao, Je! Ni mtu yupi atakayeanza kupigana na wana wa Amoni? Yeye atakuwa ni kichwa juu ya wenyeji wote wa Gileadi. Waamuzi 10:18

The people, the princes of Gilead, said one to another, What man is he who will begin to fight against the children of Ammon? he shall be head over all the inhabitants of Gilead.