Waamuzi 9 Swahili & English

Listen/Download Audio
Waamuzi 9 (Swahili) Judges 9 (English)

Abimeleki, mwana wa Yerubaali, akaenda Shekemu kwa ndugu za mama yake, akanena nao, na wote waliokuwa wa nyumba ya baba ya mama yake, akasema, Waamuzi 9:1

Abimelech the son of Jerubbaal went to Shechem to his mother's brothers, and spoke with them, and with all the family of the house of his mother's father, saying,

Haya, neneni tafadhali masikioni mwa waume wote wa Shekemu, mkaulize, Je! Ni lipi lililo jema kwenu, kwamba hao wana wa Yerubaali wote, ambao ni watu sabini, watawale juu yenu, au kwamba mtu mmoja atawale juu yenu? Tena kumbukeni ya kwamba mimi ni mfupa na nyama yenu. Waamuzi 9:2

Please speak in the ears of all the men of Shechem, Whether is better for you, that all the sons of Jerubbaal, who are seventy persons, rule over you, or that one rule over you? Remember also that I am your bone and your flesh.

Hao ndugu za mama yake wakanena habari zake masikioni mwa hao watu wote wa Shekemu maneno hayo yote; na mioyo yao ikaelekea kumwandama Abimeleki; kwa kuwa walisema, Huyu ni ndugu yetu. Waamuzi 9:3

His mother's brothers spoke of him in the ears of all the men of Shechem all these words: and their hearts inclined to follow Abimelech; for they said, He is our brother.

Wakampa vipande vya fedha sabini vilivyotoka katika nyumba ya Baal-berithi, na kwa fedha hizo Abimeleki akaajiri watu wapuuzi mabaradhuli, wafuatane naye. Waamuzi 9:4

They gave him seventy [pieces] of silver out of the house of Baal Berith, with which Abimelech hired vain and light fellows, who followed him.

Kisha akaenda nyumbani kwa babaye huko Ofra, akawaua nduguze, hao wana wa Yerubaali, watu sabini, akawaua juu ya jiwe moja; lakini Yothamu, mwana mdogo wa Yerubaali, alisalia; kwa maana alijificha. Waamuzi 9:5

He went to his father's house at Ophrah, and killed his brothers the sons of Jerubbaal, being seventy persons, on one stone: but Jotham the youngest son of Jerubbaal was left; for he hid himself.

Kisha hao watu wote wa Shekemu wakakusanyika pamoja, na jamaa yote ya Milo, wakaenda na kumtawaza Abimeleki awe mfalme, karibu na huo mgandi ulio karibu na ngome iliyo katika Shekemu. Waamuzi 9:6

All the men of Shechem assembled themselves together, and all the house of Millo, and went and made Abimelech king, by the oak of the pillar that was in Shechem.

Kisha walipomwambia huyo Yothamu, yeye akaenda, akasimama juu ya kilele cha kilima cha Gerizimu, akapaza sauti yake, akapiga kelele, na kuwaambia, Nisikieni mimi, enyi watu wa Shekemu, ili kwamba Mungu naye apate kuwasikia ninyi. Waamuzi 9:7

When they told it to Jotham, he went and stood on the top of Mount Gerizim, and lifted up his voice, and cried, and said to them, Listen to me, you men of Shechem, that God may listen to you.

Siku moja miti ilitoka ili kuutia mmoja mafuta uwe mfalme juu yao; ikauambia mti mzeituni, Tawala wewe juu yetu. Waamuzi 9:8

The trees went forth on a time to anoint a king over them; and they said to the olive tree, Reign you over us.

Lakini huo mzeituni ukaiambia, Je! Niache mafuta yangu, ambayo kwangu mimi watu wamheshimu Mungu na wanadamu, ili niende nikayonge-yonge juu ya miti? Waamuzi 9:9

But the olive tree said to them, Should I leave my fatness, with which by me they honor God and man, and go to wave back and forth over the trees?

Kisha miti ikauambia mtini, Njoo wewe, utawale juu yetu. Waamuzi 9:10

The trees said to the fig tree, Come you, and reign over us.

Lakini huo mtini ukaiambia, Je! Niuache utamu wangu, na matunda yangu mazuri, niende nikayonge-yonge juu ya miti? Waamuzi 9:11

But the fig tree said to them, Should I leave my sweetness, and my good fruit, and go to wave back and forth over the trees?

Kisha miti ikauambia mzabibu, Njoo wewe, utawale juu yetu. Waamuzi 9:12

The trees said to the vine, Come you, and reign over us.

Huo mzabibu nao ukaiambia, Je! Niiache divai yangu, ambayo humfurahisha Mungu na wanadamu, ili niende nikayonge-yonge juu ya miti? Waamuzi 9:13

The vine said to them, Should I leave my new wine, which cheers God and man, and go to wave back and forth over the trees?

Ndipo hiyo miti yote ikauambia mti wa miiba, Njoo wewe, utawale juu yetu. Waamuzi 9:14

Then said all the trees to the bramble, Come you, and reign over us.

Huo mti wa miiba ukaiambia miti, Kwamba ninyi mwanitia mafuta niwe mfalme juu yenu kwelikweli, basi njoni mtumaini kivuli changu; na kwamba sivyo, na utoke moto katika mti wa miiba na kuiteketeza mierezi ya Lebanoni. Waamuzi 9:15

The bramble said to the trees, If in truth you anoint me king over you, then come and take refuge in my shade; and if not, let fire come out of the bramble, and devour the cedars of Lebanon.

Basi sasa ikiwa mmetenda kwa uaminifu na uelekevu, katika kumtawaza Abimeleki awe mfalme, na ikiwa mmemtendea mema Yerubaali na nyumba yake, na kumtendea kama ilivyostahili mikono yake; Waamuzi 9:16

Now therefore, if you have dealt truly and righteously, in that you have made Abimelech king, and if you have dealt well with Jerubbaal and his house, and have done to him according to the deserving of his hands

(kwa maana baba yangu aliwatetea ninyi, na kuhatirisha uhai wake, na kuwaokoa na mikono ya Midiani; Waamuzi 9:17

(for my father fought for you, and adventured his life, and delivered you out of the hand of Midian:

nanyi mmeinuka juu ya nyumba ya baba yangu hivi leo nanyi mmewaua wanawe, watu sabini, juu ya jiwe moja, nanyi mmemtawaza Abimeleki, mwana wa kijakazi chake, awe mfalme juu ya watu wa Shekemu kwa sababu yeye ni ndugu yenu;) Waamuzi 9:18

and you are risen up against my father's house this day, and have slain his sons, seventy persons, on one stone, and have made Abimelech, the son of his maid-servant, king over the men of Shechem, because he is your brother);

basi ikiwa mmemtendea kwa uaminifu na uelekevu Yerubaali na nyumba yake hivi leo, basi furahini ninyi katika huyo Abimeleki, yeye naye na afurahi kwenu ninyi; Waamuzi 9:19

if you then have dealt truly and righteously with Jerubbaal and with his house this day, then rejoice you in Abimelech, and let him also rejoice in you:

lakini kwamba sivyo hivyo, basi, moto na utoke katika Abimeleki na kuwateketeza watu wa Shekemu, na jamaa ya Milo; kisha moto na utoke katika hao watu wa Shekemu, na katika jamaa ya Milo, na kumteketeza Abimeleki. Waamuzi 9:20

but if not, let fire come out from Abimelech, and devour the men of Shechem, and the house of Millo; and let fire come out from the men of Shechem, and from the house of Millo, and devour Abimelech.

Kisha Yothamu akaenda zake na kukimbia, akaenda Beeri, na kukaa kuko, kwa kumwogopa Abimeleki nduguye. Waamuzi 9:21

Jotham ran away, and fled, and went to Beer, and lived there, for fear of Abimelech his brother.

Basi Abimeleki alitawala juu ya Israeli muda wa miaka mitatu. Waamuzi 9:22

Abimelech was prince over Israel three years.

Kisha Mungu akapeleka roho mbaya kati ya Abimeleki na watu wa Shekemu; nao watu wa Shekemu wakamtendea Abimeleki kwa udanganyifu; Waamuzi 9:23

God sent an evil spirit between Abimelech and the men of Shechem; and the men of Shechem dealt treacherously with Abimelech:

ili kwamba huo udhalimu waliotendewa hao wana sabini wa Yerubaali uje, tena kwamba damu yao iandikwe juu ya Abimeleki ndugu yao, aliyewaua, na juu ya watu wa Shekemu, waliomtia nguvu mikono yake ili awaue hao nduguze. Waamuzi 9:24

that the violence done to the seventy sons of Jerubbaal might come, and that their blood might be laid on Abimelech their brother, who killed them, and on the men of Shechem, who strengthened his hands to kill his brothers.

Basi watu wa Shekemu wakaweka watu kumvizia juu ya vilele vya milima, ambao waliwanyang'anya vitu vyao watu wote waliopita njia hiyo karibu nao; naye Abimeleki aliambiwa. Waamuzi 9:25

The men of Shechem set liers-in-wait for him on the tops of the mountains, and they robbed all who came along that way by them: and it was told Abimelech.

Kisha Gaali, mwana wa Ebedi, akaenda pamoja na nduguze, wakavuka na kufika Shekemu; na watu wa Shekemu wakamtumaini yeye. Waamuzi 9:26

Gaal the son of Ebed came with his brothers, and went over to Shechem; and the men of Shechem put their trust in him.

Nao wakatoka kwenda mashambani, wakavuna mashamba yao ya mizabibu, na kuzishindika hizo zabibu, na kufanya sikukuu, kisha wakaingia nyumbani mwa mungu wao, wakala na kunywa na kumlaani huyo Abimeleki. Waamuzi 9:27

They went out into the field, and gathered their vineyards, and trod [the grapes], and held festival, and went into the house of their god, and did eat and drink, and cursed Abimelech.

Naye Gaali mwana wa Ebedi akasema, Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani, hata tukamtumikie yeye? Yeye, je! Si mwana wa Yerubaali? Na Zebuli siye akida wake? Haya, ninyi watumikieni hao watu wa Hamori, babaye Shekemu; Lakini sisi je! Tumtumikie kwa sababu gani? Waamuzi 9:28

Gaal the son of Ebed said, Who is Abimelech, and who is Shechem, that we should serve him? Isn't he the son of Jerubbaal? and Zebul his officer? serve you the men of Hamor the father of Shechem: but why should we serve him?

Laiti watu hawa wangekuwa chini ya mkono wangu! Hapo basi mimi ningemwondoa huyo Abimeleki. Kisha akamwambia Abimeleki, Haya, ongeza askari zako, utoke nje. Waamuzi 9:29

Would that this people were under my hand! then would I remove Abimelech. He said to Abimelech, Increase your army, and come out.

Basi hapo Zebuli, aliyekuwa liwali wa mji, alipoyasikia hayo maneno ya Gaali mwana wa Ebedi, hasira zake zikamwaka. Waamuzi 9:30

When Zebul the ruler of the city heard the words of Gaal the son of Ebed, his anger was kindled.

Naye akatuma wajumbe waende kwa Abimeleki kwa siri, akasema, Tazama, Gaali, mwana wa Ebedi, na ndugu zake wamekuja Shekemu; na tazama waufitinisha mji huu kinyume chako. Waamuzi 9:31

He sent messengers to Abimelech craftily, saying, Behold, Gaal the son of Ebed and his brothers are come to Shechem; and, behold, they constrain the city [to take part] against you.

Basi sasa, inuka wewe, usiku, wewe na watu walio pamoja nawe, mvizie mashambani; Waamuzi 9:32

Now therefore, up by night, you and the people who are with you, and lie in wait in the field:

kisha itakuwa, asubuhi, mara litakapokucha jua, wewe utaamka asubuhi na mapema, na kuushambulia mji huo; tena, angalia, hapo yeye na wale watu walio pamoja naye watakapokutokea nje kupigana nawe, ndipo utapata kuwatenda kama utakavyopata nafasi. Waamuzi 9:33

and it shall be, that in the morning, as soon as the sun is up, you shall rise early, and rush on the city; and, behold, when he and the people who are with him come out against you, then may you do to them as you shall find occasion.

Basi Abimeleki akainuka na watu wote waliokuwa pamoja naye, usiku nao wakauvizia Shekemu kwa vikosi vinne. Waamuzi 9:34

Abimelech rose up, and all the people who were with him, by night, and they laid wait against Shechem in four companies.

Huyo Gaali mwana wa Ebedi akatoka nje, akasimama penye maingilio ya lango la mji; naye Abimeleki na hao watu waliokuwa pamoja naye wakainuka kutoka mahali pale walipokuwa wanavizia. Waamuzi 9:35

Gaal the son of Ebed went out, and stood in the entrance of the gate of the city: and Abimelech rose up, and the people who were with him, from the ambush.

Basi Gaali alipowaona hao watu, akamwambia Zebuli, Tazama, watu washuka kutoka katika vilele vya milima. Zebuli akamwambia, Ni kivuli cha milima unachokiona kama ndio watu. Waamuzi 9:36

When Gaal saw the people, he said to Zebul, Behold, there come people down from the tops of the mountains. Zebul said to him, You see the shadow of the mountains as if they were men.

Kisha Gaali akasema mara ya pili, akanena, Angalia, watu washuka katikati ya nchi, na kikosi kimoja kinakuja kwa njia ya mwaloni wa Meonenimu. Waamuzi 9:37

Gaal spoke again and said, Behold, there come people down by the middle of the land, and one company comes by the way of the oak of Meonenim.

Ndipo Zebuli akamwambia, Je! Kinywa chako sasa ki wapi, hata ukasema Huyo Abimeleki ni nani, hata inatupasa kumtumikia yeye? Je! Hawa sio watu hao uliowadharau wewe? Haya, toka nje sasa, tafadhali, upigane nao. Waamuzi 9:38

Then said Zebul to him, Where is now your mouth, that you said, Who is Abimelech, that we should serve him? is not this the people that you have despised? go out now, I pray, and fight with them.

Basi Gaali akatoka nje mbele ya watu wa Shekemu, akapigana na Abimeleki. Waamuzi 9:39

Gaal went out before the men of Shechem, and fought with Abimelech.

Lakini Abimeleki akamkimbiza, naye akakimbia mbele yake, wengi wakaanguka waliojeruhiwa hata kufikilia maingilio ya hilo lango. Waamuzi 9:40

Abimelech chased him, and he fled before him, and there fell many wounded, even to the entrance of the gate.

Abimeleki akakaa Aruma; naye Zebuli akawatoa Gaali na ndugu zake, wasikae katika Shekemu. Waamuzi 9:41

Abimelech lived at Arumah: and Zebul drove out Gaal and his brothers, that they should not dwell in Shechem.

Ikawa siku ya pili yake, watu wakatoka waende mashambani; naye Abimeleki aliambiwa. Waamuzi 9:42

It happened on the next day, that the people went out into the field; and they told Abimelech.

Naye akawatwaa watu wake, na kuwagawanya wawe vikosi vitatu, nao wakavizia mashambani; naye akaangalia, na tazama, watu walikuwa watoka humo mjini; basi akainuka na kupigana nao, akawapiga. Waamuzi 9:43

He took the people, and divided them into three companies, and laid wait in the field; and he looked, and, behold, the people came forth out of the city; He rose up against them, and struck them.

Abimeleki, na vile vikosi vilivyokuwa pamoja naye, wakafuliza kwenda mbele, wakasimama penye maingilio ya lango la mji, na vile vikosi viwili vikawarukia hao wote waliokuwa mashambani, na kuwapiga. Waamuzi 9:44

Abimelech, and the companies that were with him, rushed forward, and stood in the entrance of the gate of the city: and the two companies rushed on all who were in the field, and struck them.

Abimeleki akapigana na huo mji mchana kutwa; akautwaa mji, akawaua watu waliokuwamo ndani yake; kisha akaupomosha mji, na kuutia chumvi. Waamuzi 9:45

Abimelech fought against the city all that day; and he took the city, and killed the people who were therein: and he beat down the city, and sowed it with salt.

Kisha watu wote waliokaa katika ile buruji ya Shekemu waliposikia habari hiyo wakaingia ndani ya ngome ya nyumba ya El-berithi. Waamuzi 9:46

When all the men of the tower of Shechem heard of it, they entered into the stronghold of the house of Elberith.

Abimeleki aliambiwa ya kuwa watu hao wote wa buruji ya Shekemu wamekutana pamoja. Waamuzi 9:47

It was told Abimelech that all the men of the tower of Shechem were gathered together.

Basi Abimeleki akakwea kwenda kilima cha Salmoni, yeye na wote waliokuwa pamoja naye; naye Abimeleki akashika shoka mkononi mwake, akakata tawi moja katika miti, akalishika na kujitweka fuzini mwake; akawaambia hao watu waliokuwa pamoja naye, Haya, mliyoniona mimi kufanya, fanyeni upesi vivyo, kama nilivyofanya mimi. Waamuzi 9:48

Abimelech got him up to Mount Zalmon, he and all the people who were with him; and Abimelech took an axe in his hand, and cut down a bough from the trees, and took it up, and laid it on his shoulder: and he said to the people who were with him, What you have seen me do, make haste, and do as I have done.

Basi watu hao wote vivyo wakakata kila mtu tawi lake, wakamwandama Abimeleki, wakayaweka hayo matawi pale ngomeni, na kuiteketeza moto hiyo ngome juu yao; basi hivyo watu wote wa hiyo buruji ya Shekemu wakafa, walipata kama watu elfu, waume kwa wake. Waamuzi 9:49

All the people likewise cut down every man his bough, and followed Abimelech, and put them to the stronghold, and set the stronghold on fire on them; so that all the men of the tower of Shechem died also, about a thousand men and women.

Ndipo Abimeleki alipokwenda Thebesi, akapanga kinyume cha Thebesi na kuutwaa. Waamuzi 9:50

Then went Abimelech to Thebez, and encamped against Thebez, and took it.

Lakini ndani ya huo mji palikuwa na buruji yenye nguvu, na watu wote waume na wake wakakimbilia huko, na watu wote wa mji, nao wakajifungia ndani, wakapanda paa la buruji. Waamuzi 9:51

But there was a strong tower within the city, and there fled all the men and women, and all they of the city, and shut themselves in, and got them up to the roof of the tower.

Abimeleki akaiendea hiyo buruji na kupigana nayo; naye akaukaribia mlango wa buruji ili auteketeze kwa moto. Waamuzi 9:52

Abimelech came to the tower, and fought against it, and drew near to the door of the tower to burn it with fire.

Na mwanamke mmoja akabwaga jiwe la kusagia la juu, nalo likampiga Abimeleki kichwani, na kulivunja fuvu la kichwa chake. Waamuzi 9:53

A certain woman cast an upper millstone on Abimelech's head, and broke his skull.

Ndipo akamwita kwa haraka huyo kijana aliyekuwa anamchukulia silaha zake, na kumwambia, Futa upanga wako, uniue, ili watu wasiseme juu yangu Aliuawa na mwanamke. Basi huyo kijana wake akamchoma upanga, naye akafa. Waamuzi 9:54

Then he called hastily to the young man his armor bearer, and said to him, Draw your sword, and kill me, that men not say of me, A woman killed him. His young man thrust him through, and he died.

Basi hapo watu wa Israeli walipoona ya kuwa Abimeleki amekufa, wakaondoka wakaenda kila mtu mahali pake. Waamuzi 9:55

When the men of Israel saw that Abimelech was dead, they departed every man to his place.

Basi hivyo Mungu akalipiza kisasi juu ya uovu wa Abimeleki aliomtenda baba yake, katika kuwaua hao nduguze watu sabini; Waamuzi 9:56

Thus God requited the wickedness of Abimelech, which he did to his father, in killing his seventy brothers;

uovu wote wa watu wa Shekemu Mungu alilipiza juu ya vichwa vyao; na hiyo laana ya Yothamu mwana wa Yerubaali ikawajilia juu yao. Waamuzi 9:57

and all the wickedness of the men of Shechem did God requite on their heads: and on them came the curse of Jotham the son of Jerubbaal.