Waamuzi 11 Swahili & English

Listen/Download Audio
Waamuzi 11 (Swahili) Judges 11 (English)

Basi huyo Yeftha, Mgileadi, alikuwa mtu shujaa sana, naye alikuwa ni mwana wa mwanamke kahaba; Gileadi akamzaa Yeftha. Waamuzi 11:1

Now Jephthah the Gileadite was a mighty man of valor, and he was the son of a prostitute: and Gilead became the father of Jephthah.

Mkewe huyo Gileadi akamzalia wana; na hao wana wa mkewe hapo walipokuwa wamekua wakubwa wakamtoa Yeftha, na kumwambia, Wewe hutarithi katika nyumba ya babaetu; kwa sababu wewe u mwana wa mwanamke mwingine. Waamuzi 11:2

Gilead's wife bore him sons; and when his wife's sons grew up, they drove out Jephthah, and said to him, You shall not inherit in our father's house; for you are the son of another woman.

Ndipo Yeftha akawakimbia hao nduguze, akakaa katika nchi ya Tobu; na watu mabaradhuli walikwenda na kutangamana na Yeftha, wakatoka kwenda pamoja naye. Waamuzi 11:3

Then Jephthah fled from his brothers, and lived in the land of Tob: and there were gathered vain fellows to Jephthah, and they went out with him.

Ikawa baadaye, wana wa Amoni wakapigana na Israeli. Waamuzi 11:4

It happened after a while, that the children of Ammon made war against Israel.

Ikatukia, hapo wana wa Amoni walipopigana na Israeli, wazee wa Gileadi wakaenda kumtwaa huyo Yeftha katika ile nchi ya Tobu; Waamuzi 11:5

It was so, that when the children of Ammon made war against Israel, the elders of Gilead went to get Jephthah out of the land of Tob;

wakamwambia Yeftha, Njoo wewe uwe kichwa chetu, ili tupate kupigana na wana wa Amoni. Waamuzi 11:6

and they said to Jephthah, Come and be our chief, that we may fight with the children of Ammon.

Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi, Je! Ninyi hamkunichukia mimi na kunifukuza nitoke katika nyumba ya baba yangu? Basi kwani kunijilia hivi sasa wakati mlio katika taabu? Waamuzi 11:7

Jephthah said to the elders of Gilead, Didn't you hate me, and drive me out of my father's house? and why are you come to me now when you are in distress?

Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, Kwa ajili ya hayo sasa tumegeuka kukuelekea wewe tena, ili uende pamoja nasi na kupigana na wana wa Amoni, nawe utakuwa kichwa chetu juu ya wenyeji wote wa Gileadi. Waamuzi 11:8

The elders of Gilead said to Jephthah, Therefore are we turned again to you now, that you may go with us, and fight with the children of Ammon; and you shall be our head over all the inhabitants of Gilead.

Basi Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi Kwamba mwanirejeza kwetu tena ili kupigana na wana wa Amoni, naye Bwana akiwatoa mbele yangu, je! Mimi nitakuwa kichwa chenu? Waamuzi 11:9

Jephthah said to the elders of Gilead, If you bring me home again to fight with the children of Ammon, and Yahweh deliver them before me, shall I be your head?

Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, Yeye Bwana atakuwa shahidi kati yetu; hakika yetu tutafanya sawasawa na neno lako. Waamuzi 11:10

The elders of Gilead said to Jephthah, Yahweh shall be witness between us; surely according to your word so will we do.

Ndipo Yeftha akaenda pamoja na wazee wa Gileadi, na hao watu wakamfanya awe kichwa, tena mkuu, juu yao; naye Yeftha akanena maneno yake yote mbele ya Bwana huko Mispa. Waamuzi 11:11

Then Jephthah went with the elders of Gilead, and the people made him head and chief over them: and Jephthah spoke all his words before Yahweh in Mizpah.

Basi Yeftha akatuma wajumbe waende kwa mfalme wa wana wa Amoni akasema, Je! Wewe una nini nami, hata umenijilia kupigana juu ya nchi yangu? Waamuzi 11:12

Jephthah sent messengers to the king of the children of Ammon, saying, What have you to do with me, that you are come to me to fight against my land?

Mfalme wa wana wa Amoni akawajibu hao wajumbe wa Yeftha Kwa sababu Israeli waliitwaa nchi yangu, hapo walipokwea kutoka katika nchi ya Misri, tokea Arnoni mpaka Yaboki, na hata Yordani; basi sasa rudisha hizo nchi tena pasipo matata. Waamuzi 11:13

The king of the children of Ammon answered to the messengers of Jephthah, Because Israel took away my land, when he came up out of Egypt, from the Arnon even to the Jabbok, and to the Jordan: now therefore restore those [lands] again peaceably.

Yeftha akatuma wajumbe mara ya pili waende kwa huyo mfalme wa wana wa Amoni; Waamuzi 11:14

Jephthah sent messengers again to the king of the children of Ammon;

akamwambia, Yeftha akuambia hivi; Israeli hakuitwaa nchi ya Moabu, wala nchi ya wana wa Amoni; Waamuzi 11:15

and he said to him, Thus says Jephthah: Israel didn't take away the land of Moab, nor the land of the children of Ammon,

lakini hapo walipokwea kutoka Misri, na Israeli walienenda katika bara hata kuifikilia Bahari ya Shamu, na kufikilia Kadeshi; Waamuzi 11:16

but when they came up from Egypt, and Israel went through the wilderness to the Red Sea, and came to Kadesh;

ndipo Israeli wakatuma wajumbe waende kwa mfalme wa Edomu, wakisema, Nakuomba sana unipe ruhusa nipite katika nchi yako; lakini mfalme wa Edomu hakusikia. Ni vivyo wakampelekea wajumbe mfalme wa Moabu; wala yeye hakukubali; basi Israeli wakakaa katika Kadeshi. Waamuzi 11:17

then Israel sent messengers to the king of Edom, saying, Please let me pass through your land; but the king of Edom didn't listen. In the same way, he sent to the king of Moab; but he would not: and Israel abode in Kadesh.

Kisha akaenda nyikani na kuizunguka hiyo nchi ya Edomu, na nchi ya Moabu, nao wakapita upande wa mashariki wa nchi ya Moabu, wakapanga marago upande wa pili wa Arnoni; wala hawakuingia ndani ya mpaka wa Moabu, kwa maana Arnoni ilikuwa ni mpaka wa Moabu. Waamuzi 11:18

Then they went through the wilderness, and went around the land of Edom, and the land of Moab, and came by the east side of the land of Moab, and they encamped on the other side of the Arnon; but they didn't come within the border of Moab, for the Arnon was the border of Moab.

Kisha Israeli wakatuma wajumbe waende kwa Sihoni mfalme wa Waamori, mfalme wa Heshboni: Israeli wakamwambia, Twakuomba utupe ruhusa tupite katika nchi yako, mpaka mahali pangu. Waamuzi 11:19

Israel sent messengers to Sihon king of the Amorites, the king of Heshbon; and Israel said to him, Let us pass, we pray you, through your land to my place.

Lakini huyo Sihoni hakuwaamini Israeli ili wapite ndani ya mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, nao wakapanga kambi katika Yahasa, wakapigana na Israeli. Waamuzi 11:20

But Sihon didn't trust Israel to pass through his border; but Sihon gathered all his people together, and encamped in Jahaz, and fought against Israel.

Bwana, Mungu wa Israeli, akamtia Sihoni na watu wake wote mikononi mwa Israeli, nao wakawapiga; basi Israeli wakaimiliki hiyo nchi ya Waamori, wenye kukaa nchi hiyo. Waamuzi 11:21

Yahweh, the God of Israel, delivered Sihon and all his people into the hand of Israel, and they struck them: so Israel possessed all the land of the Amorites, the inhabitants of that country.

Nao wakaumiliki mpaka wote wa Waamori, tokea Arnoni hata Yaboki, tokea hiyo bara hata Yordani. Waamuzi 11:22

They possessed all the border of the Amorites, from the Arnon even to the Jabbok, and from the wilderness even to the Jordan.

Basi sasa yeye Bwana, Mungu wa Israeli, amewapokonya Waamori watoke mbele ya watu wake Israeli, na wewe wataka kuwatamalaki? Waamuzi 11:23

So now Yahweh, the God of Israel, has dispossessed the Amorites from before his people Israel, and should you possess them?

Je! Wewe hutakitamalaki hicho ambacho huyo Kemoshi mungu wako akupa kukitamalaki? Kadhalika, awaye yote ambaye Bwana, Mungu wetu, amemfukuza atoke mbele yetu hao ndio tutakaowatamalaki. Waamuzi 11:24

Won't you possess that which Chemosh your god gives you to possess? So whoever Yahweh our God has dispossessed from before us, them will we possess.

Na wewe sasa, je! U mwema kuliko Balaki mwana wa Sipori, huyo mfalme wa Moabu, kwa lo lote? Je! Yeye alishindana na Israeli, au kupigana nao? Waamuzi 11:25

Now are you anything better than Balak the son of Zippor, king of Moab? did he ever strive against Israel, or did he ever fight against them?

Wakati Israeli waliokuwa wakikaa Heshboni na miji yake, na katika Aroeri na miji yake, na katika miji hiyo yote iliyo huko kando ya Arnoni, muda wa miaka mia tatu; mbona ninyi hamkuipata tena katika majira hayo? Waamuzi 11:26

While Israel lived in Heshbon and its towns, and in Aroer and its towns, and in all the cities that are along by the side of the Arnon, three hundred years; why didn't you recover them within that time?

Basi mimi sikukufanyia wewe dhambi, lakini wewe unanitenda uovu kwa kupigana nami; yeye Bwana, yeye Mwamuzi, na awe mwamuzi hivi leo kati ya wana wa Israeli na wana wa Amoni. Waamuzi 11:27

I therefore have not sinned against you, but you do me wrong to war against me: Yahweh, the Judge, be judge this day between the children of Israel and the children of Ammon.

Lakini mfalme wa wana wa Amoni hakuyasikiza hayo maneno ya Yeftha aliompelekea. Waamuzi 11:28

However the king of the children of Ammon didn't listen to the words of Jephthah which he sent him.

Ndipo roho ya Bwana ikamjilia juu yake Yeftha, naye akapita katika Gileadi na Manase, akapita na katika Mispa ya Gileadi, na kutoka hapo Mispa ya Gileadi akapita kuwaendea wana wa Amoni. Waamuzi 11:29

Then the Spirit of Yahweh came on Jephthah, and he passed over Gilead and Manasseh, and passed over Mizpeh of Gilead, and from Mizpeh of Gilead he passed over to the children of Ammon.

Naye Yeftha akamwekea Bwana nadhiri, akasema, Kwamba wewe utawatia wana wa Amoni mkononi mwangu kweli, Waamuzi 11:30

Jephthah vowed a vow to Yahweh, and said, If you will indeed deliver the children of Ammon into my hand,

ndipo itakuwa ya kwamba, kile kitakachotoka katika milango ya nyumba yangu kunilaki, hapo nitakaporudi na amani kutoka kwa hao wana wa Amoni, kitu hicho kitakuwa ni cha Bwana, nami nitakisongeza kiwe sadaka ya kuteketezwa. Waamuzi 11:31

then it shall be, that whatever comes forth from the doors of my house to meet me, when I return in peace from the children of Ammon, it shall be Yahweh's, and I will offer it up for a burnt offering.

Basi Yeftha akavuka kuwaendea wana wa Amoni ili kupigana nao; naye Bwana akawaua mkononi mwake. Waamuzi 11:32

So Jephthah passed over to the children of Ammon to fight against them; and Yahweh delivered them into his hand.

Akawapiga kutoka Aroeri hata kufikilia Minithi, miji ishirini, na mpaka Abel-keramimu, akawapiga kwa machinjo makuu mno. Basi hivyo wana wa Amoni walishindwa mbele ya wana wa Israeli. Waamuzi 11:33

He struck them from Aroer until you come to Minnith, even twenty cities, and to Abelcheramim, with a very great slaughter. So the children of Ammon were subdued before the children of Israel.

Kisha Yeftha akafika Mispa nyumbani kwake, na tazama, binti yake akamtokea kumlaki, na matari na machezo; naye alikuwa ni mwanawe pekee; hakuwa na mwingine, mwana wala binti, ila yeye. Waamuzi 11:34

Jephthah came to Mizpah to his house; and, behold, his daughter came out to meet him with tambourines and with dances: and she was his only child; besides her he had neither son nor daughter.

Ikawa alipomwona akayararua mavazi yake, akasema, Ole wangu! Mwanangu, umenitweza sana, nawe u mmoja miongoni mwa hao wanisumbuao; kwa kuwa mimi nimemfunulia Bwana kinywa changu, nami siwezi kurejea nyuma. Waamuzi 11:35

It happened, when he saw her, that he tore his clothes, and said, Alas, my daughter! you have brought me very low, and you are one of those who trouble me; for I have opened my mouth to Yahweh, and I can't go back.

Binti yake akamwambia, Baba yangu, wewe umemfunulia Bwana kinywa chako; basi unifanyie sawasawa na hayo yaliyotoka kinywani mwako; kwa kuwa yeye Bwana amekulipia kisasi juu ya adui zako, hao wana wa Amoni. Waamuzi 11:36

She said to him, My father, you have opened your mouth to Yahweh; do to me according to that which has proceeded out of your mouth, because Yahweh has taken vengeance for you on your enemies, even on the children of Ammon.

Kisha akamwambia baba yake, Basi na nifanyiwe neno hili; niache peke yangu muda wa miezi miwili, ili nipate kwenenda milimani, na kuombolea uanawali wangu, mimi na wenzangu. Waamuzi 11:37

She said to her father, Let this thing be done for me: let me alone two months, that I may depart and go down on the mountains, and bewail my virginity, I and my companions.

Akamwambia, Haya, enda. Akampeleka mbali muda wa miezi miwili; naye akaenda zake, yeye na wenziwe, akauombolea uanawali wake huko milimani. Waamuzi 11:38

He said, Go. He sent her away for two months: and she departed, she and her companions, and mourned her virginity on the mountains.

Basi ikawa mwisho wa hiyo miezi miwili, akarudi kwa babaye, aliyemtenda sawasawa na ile nadhiri yake aliyokuwa ameiweka; naye alikuwa hajamjua mtu mume. Kisha ikawa desturi katika Israeli, Waamuzi 11:39

It happened at the end of two months, that she returned to her father, who did with her according to his vow which he had vowed: and she was a virgin. It was a custom in Israel,

kwamba binti za Israeli waende mwaka baada ya mwaka ili kumkumbuka huyo mwana wa Yeftha, Mgileadi, siku nne katika mwaka. Waamuzi 11:40

that the daughters of Israel went yearly to celebrate the daughter of Jephthah the Gileadite four days in a year.