Kumbukumbu la Torati 15

Deuteronomy Chapter 15

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Kila miaka saba, mwisho wake, fanya maachilio.
At the end of every seven years you shall make a release.
2
Na jinsi ya maachilio ni hii, kila mkopeshaji na akiache alichomkopesha mwenziwe, wala asimlipize mwenziwe wala nduguye; kwa kuwa imepigwa mbiu ya maachilio ya Bwana.
This is the manner of the release: every creditor shall release that which he has lent to his neighbor; he shall not exact it of his neighbor and his brother; because Yahweh's release has been proclaimed.
3
Waweza kumtoza mgeni; lakini kila uwiacho kwa nduguyo mkono wako utamwachilia.
Of a foreigner you may exact it: but whatever of your is with your brother your hand shall release.
4
Lakini hawatakuwako maskini kwenu; (kwa kuwa Bwana atakubarikia kweli katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, uimiliki, iwe urithi wako;)
However there shall be no poor with you; (for Yahweh will surely bless you in the land which Yahweh your God gives you for an inheritance to possess it;)
5
kwamba utaisikiza tu kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, uyatunze maagizo haya yote nikuagizayo leo, kuyafanya.
if only you diligently listen to the voice of Yahweh your God, to observe to do all this commandment which I command you this day.
6
Kwani Bwana, Mungu wako, atakubarikia, kama alivyokuahidi; nawe utakopesha mataifa mengi, lakini hutakopa; tena utayatawala mataifa mengi, usitawaliwe na wao.
For Yahweh your God will bless you, as he promised you: and you shall lend to many nations, but you shall not borrow; and you shall rule over many nations, but they shall not rule over you.
7
Kama akiwapo mtu maskini pamoja nawe, nduguzo mmojawapo, ndani ya malango yako mojawapo, katika nchi yako akupayo Bwana, Mungu wako, usifanye moyo wako kuwa mgumu, wala usimfumbie mkono wako nduguyo maskini;
If there be with you a poor man, one of your brothers, within any of your gates in your land which Yahweh your God gives you, you shall not harden your heart, nor shut your hand from your poor brother;
8
lakini mfumbulie mkono wako kwa kweli, umkopeshe kwa kweli yatoshayo haja yake katika ahitajiayo.
but you shall surely open your hand to him, and shall surely lend him sufficient for his need [in that] which he wants.
9
Jitunze, msiwe na neno lisilofaa moyoni mwako, kusema, Umekaribia mwaka wa saba, mwaka wa maachilio; jicho lako likawa ovu juu ya nduguyo usimpe kitu; naye akamlilia Bwana juu yako, ikawa ni dhambi kwako.
Beware that there not be a base thought in your heart, saying, The seventh year, the year of release, is at hand; and your eye be evil against your poor brother, and you give him nothing; and he cry to Yahweh against you, and it be sin to you.
10
Mpe kwa kweli, wala moyo wako usisikitike utakapompa; kwa kuwa atakubarikia Bwana, Mungu wako, kwa neno hili katika kazi yako yote, na katika kila utakalotia mkono wako.
You shall surely give him, and your heart shall not be grieved when you give to him; because that for this thing Yahweh your God will bless you in all your work, and in all that you put your hand to.
11
Kwa maana maskini hawatakoma katika nchi milele; ndipo ninakuamuru na kukuambia, Mfumbulie kwa kweli mkono wako nduguyo, mhitaji wako, maskini wako, katika nchi yako.
For the poor will never cease out of the land: therefore I command you, saying, You shall surely open your hand to your brother, to your needy, and to your poor, in your land.
12
Ikiwa nduguyo, mume wa Kiebrania, au mwanamke wa Kiebrania, akiuzwa kwako, naye amekutumikia miaka sita; basi mwaka wa saba mwache huru aondoke kwako.
If your brother, a Hebrew man, or a Hebrew woman, be sold to you, and serve you six years; then in the seventh year you shall let him go free from you.
13
Nawe utakapomwacha huru aondoke kwako, usimwache aende zake mikono mitupu;
When you let him go free from you, you shall not let him go empty:
14
umwangalie kwa wema katika kundi lako, na sakafu yako ya nafaka, na kinu chako cha divai; mpe kama alivyokubarikia Bwana, Mungu wako.
you shall furnish him liberally out of your flock, and out of your threshing floor, and out of your winepress; as Yahweh your God has blessed you, you shall give to him.
15
Nawe kumbuka kwamba ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri, akakukomboa Bwana, Mungu wako; kwa hiyo mimi nakuamuru neno hili hivi leo.
You shall remember that you were a bondservant in the land of Egypt, and Yahweh your God redeemed you: therefore I command you this thing today.
16
Hata itakuwa, akikuambia, Siondoki kwako; kwa sababu akupenda wewe na nyumba yako, kwa kuwa yu hali njema kwako;
It shall be, if he tell you, I will not go out from you; because he loves you and your house, because he is well with you;
17
ndipo utwae uma, uupenyeze katika sikio lake uingie katika ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako milele. Na kijakazi chako naye mfanye vivyo.
then you shall take an awl, and thrust it through his ear to the door, and he shall be your servant forever. Also to your maid-servant you shall do likewise.
18
Wala usione ugumu, utakapomwacha huru kuondoka kwako; kwani amekutumikia miaka sita kwa ujira mara mbili wa mwajiriwa; na Bwana, Mungu wako, atakubarikia kwa yote utakayofanya.
It shall not seem hard to you, when you let him go free from you; for to the double of the hire of a hireling has he served you six years: and Yahweh your God will bless you in all that you do.
19
Wazaliwa wa kwanza waume wote wazaliwao katika kundi lako la ng'ombe na la kondoo, uwatakase kwa Bwana, Mungu wako; usifanye kazi kwa mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe wako, wala usimkate manyoya mzaliwa wa kwanza wa kundi lako la kondoo.
All the firstborn males that are born of your herd and of your flock you shall sanctify to Yahweh your God: you shall do no work with the firstborn of your herd, nor shear the firstborn of your flock.
20
Utamla mbele za Bwana, Mungu wako, mwaka hata mwaka mahali atakapochagua Bwana, wewe na nyumba yako.
You shall eat it before Yahweh your God year by year in the place which Yahweh shall choose, you and your household.
21
Lakini akiwa na kilema, akichechea, au akiwa kipofu, au mwenye kilema kibaya cho chote, usimsongezee Bwana, Mungu wako, sadaka.
If it have any blemish, [as if it be] lame or blind, any ill blemish whatever, you shall not sacrifice it to Yahweh your God.
22
Utamla ndani ya malango yako; wasio tohara na wenye tohara pia watakula, kama unavyokula paa na kulungu.
You shall eat it within your gates: the unclean and the clean [shall eat it] alike, as the gazelle, and as the hart.
23
Pamoja na haya usile damu yake; uimwage nchi kama maji.
Only you shall not eat its blood; you shall pour it out on the ground as water.
« 14 16 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)