1 Wafalme 16 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Wafalme 16 (Swahili) 1st Kings 16 (English)

Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani juu ya Baasha, kusema, 1 Wafalme 16:1

The word of Yahweh came to Jehu the son of Hanani against Baasha, saying,

Kwa kuwa mimi nilikuinua kutoka katika mavumbi, na kukufanya uwe mkuu juu ya watu wangu Israeli; nawe umeiendea njia ya Yeroboamu, na kuwakosesha watu wangu Israeli, hata wanighadhibishe kwa makosa yao; 1 Wafalme 16:2

Because I exalted you out of the dust, and made you prince over my people Israel, and you have walked in the way of Jeroboam, and have made my people Israel to sin, to provoke me to anger with their sins;

angalia, kuondoa nitawaondoa Baasha na jamaa yake; tena nitaifanya nyumba yako iwe kama nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati. 1 Wafalme 16:3

behold, I will utterly sweep away Baasha and his house; and I will make your house like the house of Jeroboam the son of Nebat.

Mtu amfiaye Baasha mjini mbwa watamla; naye amfiaye mashambani ndege wa angani watamla. 1 Wafalme 16:4

Him who dies of Baasha in the city shall the dogs eat; and him who dies of his in the field shall the birds of the sky eat.

Basi, mambo yote ya Baasha yaliyosalia, na aliyoyafanya, na nguvu zake, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli? 1 Wafalme 16:5

Now the rest of the acts of Baasha, and what he did, and his might, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Israel?

Baasha akalala na babaze, akazikwa katika Tirza; naye Ela mwanawe akatawala mahali pake. 1 Wafalme 16:6

Baasha slept with his fathers, and was buried in Tirzah; and Elah his son reigned in his place.

Tena neno la Bwana likaja kwa mkono wa nabii Yehu mwana wa Hanani juu ya Baasha, na juu ya nyumba yake, kwa sababu ya mabaya yote aliyoyatenda machoni pa Bwana, akimghadhibisha kwa kazi ya mikono yake, kwa kufanana na nyumba ya Yeroboamu, na kwa sababu aliiharibu. 1 Wafalme 16:7

Moreover by the prophet Jehu the son of Hanani came the word of Yahweh against Baasha, and against his house, both because of all the evil that he did in the sight of Yahweh, to provoke him to anger with the work of his hands, in being like the house of Jeroboam, and because he struck him.

Katika mwaka wa ishirini na sita wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha alianza kutawala juu ya Israeli huko Tirza, akatawala miaka miwili. 1 Wafalme 16:8

In the twenty-sixth year of Asa king of Judah began Elah the son of Baasha to reign over Israel in Tirzah, [and reigned] two years.

Na mtumwa wake Zimri, jemadari wa nusu ya magari yake, akamfanyia fitina; alipokuwako Tirza akinywa hata kulewa nyumbani mwa Arsa, aliyekuwa juu ya nyumba huko Tirza; 1 Wafalme 16:9

His servant Zimri, captain of half his chariots, conspired against him. Now he was in Tirzah, drinking himself drunk in the house of Arza, who was over the household in Tirzah:

Zimri akaingia akampiga, akamwua, katika mwaka wa ishirini na saba wa Asa mfalme wa Yuda, akatawala mahali pake. 1 Wafalme 16:10

and Zimri went in and struck him, and killed him, in the twenty-seventh year of Asa king of Judah, and reigned in his place.

Ikawa, alipoanza kutawala, mara alipoketi juu ya kiti chake cha enzi, akawaua nyumba yote ya Baasha; hakumwachia mwanamume ye yote, wa jamaa zake, wala wa rafiki zake. 1 Wafalme 16:11

It happened, when he began to reign, as soon as he sat on his throne, that he struck all the house of Baasha: he didn't leave him a single man-child, neither of his relatives, nor of his friends.

Hivyo Zimri akaiharibu nyumba yote ya Baasha, sawasawa na neno la Bwana, alilolinena juu ya Baasha kwa Yehu nabii, 1 Wafalme 16:12

Thus did Zimri destroy all the house of Baasha, according to the word of Yahweh, which he spoke against Baasha by Jehu the prophet,

kwa sababu ya makosa yake Baasha, na makosa yote ya Ela mwanawe, waliyoyakosa, na kuwakosesha Israeli, wakimghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kwa matendo yao ya ubatili. 1 Wafalme 16:13

for all the sins of Baasha, and the sins of Elah his son, which they sinned, and with which they made Israel to sin, to provoke Yahweh, the God of Israel, to anger with their vanities.

Na mambo yote ya Ela yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli? 1 Wafalme 16:14

Now the rest of the acts of Elah, and all that he did, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Israel?

Katika mwaka wa ishirini na saba wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala muda wa siku saba huko Tirza. Basi, watu walikuwa wametua maragoni kupigana na Gibethoni, ulio wa Wafilisti. 1 Wafalme 16:15

In the twenty-seventh year of Asa king of Judah did Zimri reign seven days in Tirzah. Now the people were encamped against Gibbethon, which belonged to the Philistines.

Na hao watu waliokuwako maragoni wakasikia habari ya kwamba Zimri amefanya fitina, tena amempiga mfalme; kwa hiyo Israeli wote wakamfanya Omri, jemadari wa jeshi, awe mfalme juu ya Israeli siku ile maragoni. 1 Wafalme 16:16

The people who were encamped heard say, Zimri has conspired, and has also struck the king: therefore all Israel made Omri, the captain of the host, king over Israel that day in the camp.

Omri akapanda kutoka Gibethoni, na Israeli wote pamoja naye, wakauhusuru Tirza. 1 Wafalme 16:17

Omri went up from Gibbethon, and all Israel with him, and they besieged Tirzah.

Ikawa Zimri alipoona ya kuwa mji umetwaliwa, akaingia ngomeni mwa nyumba ya mfalme, akaiteketeza nyumba ya mfalme juu yake kwa moto, akafa; 1 Wafalme 16:18

It happened, when Zimri saw that the city was taken, that he went into the castle of the king's house, and burnt the king's house over him with fire, and died,

kwa sababu ya makosa aliyoyakosa, akifanya mabaya machoni pa Bwana, kwa kuiendea njia ya Yeroboamu na makosa yake aliyoyafanya akiwakosesha Israeli. 1 Wafalme 16:19

for his sins which he sinned in doing that which was evil in the sight of Yahweh, in walking in the way of Jeroboam, and in his sin which he did, to make Israel to sin.

Na mambo yote ya Zimri yaliyosalia na fitina yake aliyoifanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli? 1 Wafalme 16:20

Now the rest of the acts of Zimri, and his treason that he did, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Israel?

Ndipo watu wa Israeli wakatengwa sehemu mbili; nusu ya watu wakamfuata Tibni mwana wa Ginathi, ili wamfanye mfalme; nusu wakamfuata Omri. 1 Wafalme 16:21

Then were the people of Israel divided into two parts: half of the people followed Tibni the son of Ginath, to make him king; and half followed Omri.

Lakini hao watu waliomfuata Omri wakawashinda watu waliomfuata Tibni mwana wa Ginathi; basi akafa Tibni, akatawala Omri. 1 Wafalme 16:22

But the people who followed Omri prevailed against the people who followed Tibni the son of Ginath: so Tibni died, and Omri reigned.

Katika mwaka wa thelathini na moja wa Asa, mfalme wa Yuda, Omri alianza kutawala juu ya Israeli, akatawala miaka kumi na miwili. Akatawala huko Tirza miaka sita. 1 Wafalme 16:23

In the thirty-first year of Asa king of Judah began Omri to reign over Israel, [and reigned] twelve years: six years reigned he in Tirzah.

Kisha akanunua kilima cha Samaria kwa Shemeri kwa talanta mbili za fedha; akajenga juu ya kilima kile, akauita mji alioujenga Samaria, kwa kuliandama jina lake Shemeri, aliyekuwa mwenye kilima. 1 Wafalme 16:24

He bought the hill Samaria of Shemer for two talents of silver; and he built on the hill, and called the name of the city which he built, after the name of Shemer, the owner of the hill, Samaria.

Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, akatenda maovu kuliko wote waliomtangulia; 1 Wafalme 16:25

Omri did that which was evil in the sight of Yahweh, and dealt wickedly above all who were before him.

kwa kuwa aliiendea njia yote ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na makosa yake, aliyowakosesha Israeli, ili kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kwa matendo yao ya ubatili. 1 Wafalme 16:26

For he walked in all the way of Jeroboam the son of Nebat, and in his sins with which he made Israel to sin, to provoke Yahweh, the God of Israel, to anger with their vanities.

Nayo mambo yote ya Omri yaliyosalia aliyoyatenda, na uthabiti alioufanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli? 1 Wafalme 16:27

Now the rest of the acts of Omri which he did, and his might that he shown, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Israel?

Omri akalala na babaze, akazikwa huko Samaria; na Ahabu mwanawe akatawala mahali pake. 1 Wafalme 16:28

So Omri slept with his fathers, and was buried in Samaria; and Ahab his son reigned in his place.

Ahabu mwana wa Omri alianza kutawala juu ya Israeli katika mwaka wa thelathini na nane wa Asa mfalme wa Yuda; akatawala Ahabu mwana wa Omri juu ya Israeli katika Samaria miaka ishirini na miwili. 1 Wafalme 16:29

In the thirty-eighth year of Asa king of Judah began Ahab the son of Omri to reign over Israel: and Ahab the son of Omri reigned over Israel in Samaria twenty-two years.

Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana kuliko wote waliomtangulia. 1 Wafalme 16:30

Ahab the son of Omri did that which was evil in the sight of Yahweh above all that were before him.

Ikawa, kama ingalikuwa neno dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia. 1 Wafalme 16:31

It happened, as if it had been a light thing for him to walk in the sins of Jeroboam the son of Nebat, that he took as wife Jezebel the daughter of Ethbaal king of the Sidonians, and went and served Baal, and worshiped him.

Akamjengea Baali madhabahu katika nyumba ya Baali, aliyoijenga huko Samaria. 1 Wafalme 16:32

He reared up an altar for Baal in the house of Baal, which he had built in Samaria.

Ahabu akaifanya Ashera; Ahabu akazidi kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko wafalme wote wa Israeli waliomtangulia. 1 Wafalme 16:33

Ahab made the Asherah; and Ahab did yet more to provoke Yahweh, the God of Israel, to anger than all the kings of Israel who were before him.

Katika siku zake, Hieli Mbetheli akajenga Yeriko; akatia misingi yake kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa kwanza, na kuyaweka malango yake kwa kufiwa na mwana wake mdogo Segubu; sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa Yoshua mwana wa Nuni.

1 Wafalme 16:34

In his days did Hiel the Bethelite build Jericho: he laid the foundation of it with the loss of Abiram his firstborn, and set up the gates of it with the loss of his youngest son Segub, according to the word of Yahweh, which he spoke by Joshua the son of Nun.