1 Wafalme 18 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Wafalme 18 (Swahili) 1st Kings 18 (English)

Ikawa baada ya siku nyingi, neno la Bwana likamjia Eliya, katika mwaka wa tatu, kusema, Enenda, ukajionyeshe kwa Ahabu; nami nitaleta mvua juu ya nchi. 1 Wafalme 18:1

It happened after many days, that the word of Yahweh came to Elijah, in the third year, saying, Go, show yourself to Ahab; and I will send rain on the earth.

Basi Eliya akaenda ili ajionyeshe kwa Ahabu. Na njaa ilikuwa nzito katika Samaria. 1 Wafalme 18:2

Elijah went to show himself to Ahab. The famine was sore in Samaria.

Ahabu akamwita Obadia, aliyekuwa juu ya nyumba yake; (na huyu Obadia alikuwa mwenye kumcha Bwana sana; 1 Wafalme 18:3

Ahab called Obadiah, who was over the household. (Now Obadiah feared Yahweh greatly:

kwa kuwa ikawa, Yezebeli alipowaua manabii wa Bwana, Obadia akatwaa manabii mia, akawaficha hamsini hamsini katika pango, akawalisha chakula na kuwapa maji). 1 Wafalme 18:4

for it was so, when Jezebel cut off the prophets of Yahweh, that Obadiah took one hundred prophets, and hid them by fifty in a cave, and fed them with bread and water.)

Ahabu akamwambia Obadia, Pita katika nchi, kwenye chemchemi zote za maji, na vijito vyote; labda tutapata majani, tuwahifadhi hai farasi na nyumbu, tusipate hasara ya hao wanyama wote. 1 Wafalme 18:5

Ahab said to Obadiah, Go through the land, to all the springs of water, and to all the brooks: peradventure we may find grass and save the horses and mules alive, that we not lose all the animals.

Basi wakaigawanya nchi, ili wapite katika nchi yote; Ahabu akaenda zake njia moja peke yake, na Obadia akaenda zake njia nyingine peke yake. 1 Wafalme 18:6

So they divided the land between them to pass throughout it: Ahab went one way by himself, and Obadiah went another way by himself.

Na Obadia alipokuwa njiani, kumbe! Eliya akakutana naye. Akamtambua, akaanguka kifudifudi, akanena, Je! Ni wewe, bwana wangu Eliya? 1 Wafalme 18:7

As Obadiah was in the way, behold, Elijah met him: and he knew him, and fell on his face, and said, Is it you, my lord Elijah?

Akamjibu, Ni mimi. Enenda, umwambie bwana wako, Tazama, Eliya yupo. 1 Wafalme 18:8

He answered him, It is I: go, tell your lord, Behold, Elijah [is here].

Akamwambia, Nimekosa nini, hata unitie mimi mtumishi wako mkononi mwa Ahabu, aniue? 1 Wafalme 18:9

He said, Wherein have I sinned, that you would deliver your servant into the hand of Ahab, to kill me?

Kama Bwana, Mungu wako, aishivyo, hakuna taifa wala ufalme ambao bwana wangu hakutuma watu wakutafute; na waliposema, Hayupo, akawaapisha ule ufalme, na taifa, ya kwamba hawakukuona. 1 Wafalme 18:10

As Yahweh your God lives, there is no nation or kingdom, where my lord has not sent to seek you: and when they said, He is not here, he took an oath of the kingdom and nation, that they didn't find you.

Nawe sasa wasema, Enenda, umwambie bwana wako, Tazama, Eliya yupo. 1 Wafalme 18:11

Now you say, Go, tell your lord, Behold, Elijah [is here].

Na itakuwa, mara mimi nikiondoka kwako, roho ya Bwana atakuchukua uende nisikojua; nami nitakapokwenda kumwambia Ahabu, naye asipokuona, ataniua, lakini mimi mtumishi wako namcha Bwana tangu ujana wangu. 1 Wafalme 18:12

It will happen, as soon as I am gone from you, that the Spirit of Yahweh will carry you I don't know where; and so when I come and tell Ahab, and he can't find you, he will kill me: but I your servant fear Yahweh from my youth.

Je! Bwana wangu hakuambiwa nilivyofanya hapo Yezebeli alipowaua manabii wa Bwana? Jinsi nilivyowaficha manabii wa Bwana, watu mia, hamsini hamsini katika pango, nikawalisha chakula na kuwapa maji? 1 Wafalme 18:13

Wasn't it told my lord what I did when Jezebel killed the prophets of Yahweh, how I hid one hundred men of Yahweh's prophets by fifty in a cave, and fed them with bread and water?

Nawe sasa wasema, Enenda umwambie bwana wako, Tazama, Eliya yupo; basi, ataniua. 1 Wafalme 18:14

Now you say, Go, tell your lord, Behold, Elijah [is here]; and he will kill me.

Eliya akasema, Kama Bwana wa majeshi aishivyo ambaye ninasimama mbele zake, hakika nitajionyesha kwake leo. 1 Wafalme 18:15

Elijah said, As Yahweh of Hosts lives, before whom I stand, I will surely show myself to him today.

Basi, Obadia akaenda zake amwone Ahabu, akamwambia; naye Ahabu akaenda kumlaki Eliya. 1 Wafalme 18:16

So Obadiah went to meet Ahab, and told him; and Ahab went to meet Elijah.

Ikawa, Ahabu alipomwona Eliya, Ahabu akamwambia, Je! Ni wewe, Ewe mtaabishaji wa Israeli? 1 Wafalme 18:17

It happened, when Ahab saw Elijah, that Ahab said to him, Is it you, you troubler of Israel?

Naye akajibu, Si mimi niliyewataabisha Israeli; bali ni wewe, na nyumba ya baba yako, kwa kuwa mmeziacha amri za Bwana; nawe umewafuata mabaali. 1 Wafalme 18:18

He answered, I have not troubled Israel; but you, and your father's house, in that you have forsaken the commandments of Yahweh, and you have followed the Baals.

Basi sasa upeleke watu, unikusanyie jamii ya Israeli katika mlima wa Karmeli, na wale manabii wa Baali mia nne na hamsini, na wale manabii wa Ashera mia nne, walao chakula mezani pa Yezebeli. 1 Wafalme 18:19

Now therefore send, and gather to me all Israel to Mount Carmel, and the prophets of Baal four hundred fifty, and the prophets of the Asherah four hundred, who eat at Jezebel's table.

Basi, Ahabu akapeleka watu kwa wana wa Israeli wote, akawakusanya manabii pamoja katika mlima wa Karmeli. 1 Wafalme 18:20

So Ahab sent to all the children of Israel, and gathered the prophets together to Mount Carmel.

Naye Eliya akawakaribia watu wote, akanena, Mtasita-sita katikati ya mawazo mawili hata lini? Bwana akiwa ndiye Mungu, mfuateni; bali ikiwa Baali ni Mungu, haya! Mfuateni yeye. Wale watu hawakumjibu neno. 1 Wafalme 18:21

Elijah came near to all the people, and said, "How long will you waver between the two sides? If Yahweh is God, follow him; but if Baal, then follow him." The people answered him not a word.

Ndipo Eliya akawaambia watu, Mimi nimesalia, mimi peke yangu, nabii wa Bwana; lakini manabii wa Baali ni watu mia nne na hamsini. 1 Wafalme 18:22

Then Elijah said to the people, "I, even I only, am left a prophet of Yahweh; but Baal's prophets are four hundred fifty men.

Kwa hiyo na watutolee ng'ombe wawili; wao na wajichagulie ng'ombe mmoja, wamkate-kate na kumweka juu ya kuni, wasitie moto chini; nami nitamtengeza huyo ng'ombe wa pili, na kumweka juu ya kuni, wala sitatia moto chini. 1 Wafalme 18:23

Let them therefore give us two bulls; and let them choose one bull for themselves, and cut it in pieces, and lay it on the wood, and put no fire under; and I will dress the other bull, and lay it on the wood, and put no fire under.

Nanyi ombeni kwa jina la mungu wenu, nami nitaomba kwa jina la Bwana; na Mungu yule ajibuye kwa moto, na awe ndiye Mungu. Watu wote wakajibu wakasema, Maneno haya ni mazuri. 1 Wafalme 18:24

You call on the name of your god, and I will call on the name of Yahweh; and the God who answers by fire, let him be God." All the people answered, "It is well said."

Eliya akawaambia manabii wa Baali, Jichagulieni ng'ombe mmoja, mkamtengeze kwanza; maana ninyi ndio wengi; mkaliitie jina la mungu wenu, wala msitie moto chini. 1 Wafalme 18:25

Elijah said to the prophets of Baal, "Choose one bull for yourselves, and dress it first; for you are many; and call on the name of your god, but put no fire under it."

Wakamtwaa yule ng'ombe waliyepewa, wakamtengeza, wakaliitia jina la Baali tangu asubuhi hata adhuhuri, wakisema, Ee Baali, utusikie. Lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu. Nao wakaruka-ruka juu ya madhabahu waliyoifanya. 1 Wafalme 18:26

They took the bull which was given them, and they dressed it, and called on the name of Baal from morning even until noon, saying, Baal, hear us. But there was no voice, nor any who answered. They leaped about the altar which was made.

Ikawa, wakati wa adhuhuri, Eliya akawafanyia dhihaka, akasema, Mwiteni kwa sauti kuu; maana ni mungu huyo; labda anazungumza, au ana shughuli, au anasafiri, au labda amelala, sharti aamshwe. 1 Wafalme 18:27

It happened at noon, that Elijah mocked them, and said, Cry aloud; for he is a god: either he is musing, or he is gone aside, or he is on a journey, or peradventure he sleeps and must be awakened.

Wakapiga kelele, wakajikata-kata kwa visu na vyembe kama ilivyo desturi yao, hata damu ikawachuruzika. 1 Wafalme 18:28

They cried aloud, and cut themselves after their manner with knives and lances, until the blood gushed out on them.

Ikawa, wakati wa adhuhuri ulipopita, walitabiri hata wakati wa kutoa dhabihu ya jioni; lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu, wala aliyeangalia. 1 Wafalme 18:29

It was so, when midday was past, that they prophesied until the time of the offering of the [evening] offering; but there was neither voice, nor any to answer, nor any who regarded.

Kisha Eliya akawaambia watu wote, Nikaribieni mimi. Watu wote wakamkaribia. Akaitengeneza madhabahu ya Bwana iliyovunjika. 1 Wafalme 18:30

Elijah said to all the people, Come near to me; and all the people came near to him. He repaired the altar of Yahweh that was thrown down.

Eliya akatwaa mawe kumi na mawili, kwa hesabu ya kabila za wana wa Yakobo, aliyejiliwa na neno la Bwana na kuambiwa, Jina lako litakuwa Israeli. 1 Wafalme 18:31

Elijah took twelve stones, according to the number of the tribes of the sons of Jacob, to whom the word of Yahweh came, saying, Israel shall be your name.

Naye akaijenga madhabahu kwa mawe hayo katika jina la Bwana; akafanya mfereji, kama wa vipimo viwili vya mbegu, ukiizunguka madhabahu. 1 Wafalme 18:32

With the stones he built an altar in the name of Yahweh; and he made a trench about the altar, as great as would contain two measures of seed.

Kisha akazipanga zile kuni, akamkata yule ng'ombe vipande vipande, akaviweka juu ya kuni. Akasema, Jazeni mapipa manne maji, mkayamwage juu ya sadaka ya kuteketezwa, na juu ya kuni. 1 Wafalme 18:33

He put the wood in order, and cut the bull in pieces, and laid it on the wood. He said, Fill four jars with water, and pour it on the burnt offering, and on the wood.

Akasema, Fanyeni mara ya pili. Wakafanya mara ya pili. Akasema, Fanyeni mara ya tatu. Wakafanya mara ya tatu. 1 Wafalme 18:34

He said, Do it the second time; and they did it the second time. He said, Do it the third time; and they did it the third time.

Yale maji yakaizunguka madhabahu; akaujaza mfereji maji. 1 Wafalme 18:35

The water ran round about the altar; and he filled the trench also with water.

Ikawa, wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, Eliya nabii akakaribia, akasema, Ee Bwana, Mungu wa Ibrahimu, na wa Isaka, na wa Israeli, na ijulikane leo ya kuwa wewe ndiwe Mungu katika Israeli, na ya kuwa mimi ni mtumishi wako, na ya kuwa nimefanya mambo haya yote kwa neno lako. 1 Wafalme 18:36

It happened at the time of the offering of the [evening] offering, that Elijah the prophet came near, and said, Yahweh, the God of Abraham, of Isaac, and of Israel, let it be known this day that you are God in Israel, and that I am your servant, and that I have done all these things at your word.

Unisikie, Ee Bwana, unisikie, ili watu hawa wajue ya kuwa wewe, Bwana, ndiwe Mungu, na ya kuwa wewe umewageuza moyo wakurudie. 1 Wafalme 18:37

Hear me, Yahweh, hear me, that this people may know that you, Yahweh, are God, and [that] you have turned their heart back again.

Ndipo moto wa Bwana ukashuka, ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa, na kuni, na mawe, na mavumbi, ukayaramba yale maji yaliyokuwamo katika mfereji. 1 Wafalme 18:38

Then the fire of Yahweh fell, and consumed the burnt offering, and the wood, and the stones, and the dust, and licked up the water that was in the trench.

Na watu wote walipoona, wakaanguka kifudifudi; wakasema, Bwana ndiye Mungu, Bwana ndiye Mungu. 1 Wafalme 18:39

When all the people saw it, they fell on their faces: and they said, Yahweh, he is God; Yahweh, he is God.

Eliya akawaambia, Wakamateni hao manabii wa Baali, asiokoke hata mmoja. Wakawakamata; na Eliya akawachukua mpaka kijito cha Kishoni, akawaua huko. 1 Wafalme 18:40

and Elijah said to them, Take the prophets of Baal; don't let one of them escape. They took them; and Elijah brought them down to the brook Kishon, and killed them there.

Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka, ule, unywe; kwani pana sauti ya mvua tele. 1 Wafalme 18:41

Elijah said to Ahab, Get you up, eat and drink; for there is the sound of abundance of rain.

Basi Ahabu akainuka ili ale na kunywa. Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi, akainama uso mpaka magotini. 1 Wafalme 18:42

So Ahab went up to eat and to drink. Elijah went up to the top of Carmel; and he bowed himself down on the earth, and put his face between his knees.

Akamwambia mtumishi wake, Kwea sasa, utazame upande wa bahari. Akakwea, akatazama, na kusema, Hakuna kitu. Naye akanena, Enenda tena mara saba. 1 Wafalme 18:43

He said to his servant, Go up now, look toward the sea. He went up, and looked, and said, There is nothing. He said, Go again seven times.

Ikawa mara ya saba akasema, Tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. Akanena, Enenda, umwambie Ahabu, Tandika, ushuke, mvua isikuzuie. 1 Wafalme 18:44

It happened at the seventh time, that he said, "Behold, a small cloud, like a man's hand, is rising out of the sea." He said, Go up, tell Ahab, Make ready [your chariot], and get you down, that the rain not stop you.

Ikawa, muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikanyesha mvua nyingi. Ahabu akapanda garini, akaenda zake Yezreeli. 1 Wafalme 18:45

It happened in a little while, that the sky grew black with clouds and wind, and there was a great rain. Ahab rode, and went to Jezreel:

Mkono wa Bwana ulikuwa juu ya Eliya; akajikaza viuno, akapiga mbio mbele ya Ahabu mpaka kuiingia Yezreeli. 1 Wafalme 18:46

and the hand of Yahweh was on Elijah; and he girded up his loins, and ran before Ahab to the entrance of Jezreel.