Mathayo 27

Matthew Chapter 27

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua;
Now when morning had come, all the chief priests and the elders of the people took counsel against Jesus to put him to death:
2
wakamfunga, wakamchukua, wakampeleka kwa Pilato aliyekuwa liwali.
and they bound him, and led him away, and delivered him up to Pontius Pilate, the governor.
3
Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia.
Then Judas, who betrayed him, when he saw that Jesus was condemned, felt remorse, and brought back the thirty pieces of silver to the chief priests and elders,
4
Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.
saying, "I have sinned in that I betrayed innocent blood." But they said, "What is that to us? You see to it."
5
Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga.
He threw down the pieces of silver in the sanctuary, and departed. He went away and hanged himself.
6
Wakuu wa makuhani wakavitwaa vile vipande vya fedha, wakasema, Si halali kuviweka katika sanduku ya sadaka, kwa kuwa ni kima cha damu.
The chief priests took the pieces of silver, and said, "It's not lawful to put them into the treasury, since it is the price of blood."
7
Wakafanya shauri, wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
They took counsel, and bought the potter's field with them, to bury strangers in.
8
Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo.
Therefore that field was called "The Field of Blood" to this day.
9
Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima;
Then that which was spoken through Jeremiah the prophet was fulfilled, saying, "They took the thirty pieces of silver, The price of him upon whom a price had been set, Whom some of the children of Israel priced,
10
wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.
And they gave them for the potter's field, As the Lord commanded me."
11
Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, Wewe wasema.
Now Jesus stood before the governor: and the governor asked him, saying, "Are you the King of the Jews?" Jesus said to him, "So you say."
12
Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno.
When he was accused by the chief priests and elders, he answered nothing.
13
Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?
Then Pilate said to him, "Don't you hear how many things they testify against you?"
14
Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana.
He gave him no answer, not even one word, so that the governor marveled greatly.
15
Basi wakati wa siku kuu, liwali desturi yake huwafungulia mkutano mfungwa mmoja waliyemtaka.
Now at the feast the governor was accustomed to release to the multitude one prisoner, whom they desired.
16
Basi palikuwa na mfungwa mashuhuri siku zile, aitwaye Baraba.
They had then a notable prisoner, called Barabbas.
17
Basi walipokutanika, Pilato akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi? Yule Baraba, au Yesu aitwaye Kristo?
When therefore they were gathered together, Pilate said to them, "Whom do you want me to release to you? Barabbas, or Jesus, who is called Christ?"
18
Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda.
For he knew that because of envy they had delivered him up.
19
Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.
While he was sitting on the judgment seat, his wife sent to him, saying, "Have nothing to do with that righteous man, for I have suffered many things this day in a dream because of him."
20
Nao wakuu wa makuhani na wazee wakawashawishi makutano ili wamtake Baraba, na kumwangamiza Yesu.
Now the chief priests and the elders persuaded the multitudes to ask for Barabbas, and destroy Jesus.
21
Basi liwali akajibu, akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi katika hawa wawili? Wakasema, Baraba.
But the governor answered them, "Which of the two do you want me to release to you?" They said, "Barabbas!"
22
Pilato akawaambia, Basi, nimtendeje Yesu aitwaye Kristo? Wakasema wote, Asulibiwe.
Pilate said to them, "What then shall I do to Jesus, who is called Christ?" They all said to him, "Let him be crucified!"
23
Akasema, Kwani? Ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, wakisema, Na asulibiwe.
But the governor said, "Why? What evil has he done?" But they cried out exceedingly, saying, "Let him be crucified!"
24
Basi Pilato alipoona ya kuwa hafai lo lote, bali ghasia inazidi tu, akatwaa maji, akanawa mikono yake mbele ya mkutano, akasema, Mimi sina hatia katika damu ya mtu huyu mwenye haki; yaangalieni haya ninyi wenyewe.
So when Pilate saw that nothing was being gained, but rather that a disturbance was starting, he took water, and washed his hands before the multitude, saying, "I am innocent of the blood of this righteous person. You see to it."
25
Watu wote wakajibu wakasema, Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu.
All the people answered, "May his blood be on us, and on our children!"
26
Ndipo akawafungulia Baraba; na baada ya kumpiga Yesu mijeledi, akamtoa ili asulibiwe.
Then he released to them Barabbas, but Jesus he flogged and delivered to be crucified.
27
Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima.
Then the governor's soldiers took Jesus into the Praetorium, and gathered the whole garrison together against him.
28
Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu.
They stripped him, and put a scarlet robe on him.
29
Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!
They braided a crown of thorns and put it on his head, and a reed in his right hand; and they kneeled down before him, and mocked him, saying, "Hail, King of the Jews!"
30
Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani.
They spat on him, and took the reed and struck him on the head.
31
Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha.
When they had mocked him, they took the robe off of him, and put his clothes on him, and led him away to crucify him.
32
Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake.
As they came out, they found a man of Cyrene, Simon by name, and they compelled him to go with them, that he might carry his cross.
33
Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa,
They came to a place called "Golgotha," that is to say, "The place of a skull."
34
wakampa kunywa divai iliyochanganyika na nyongo; lakini yeye alipoionja hakutaka kunywa.
They gave him sour wine to drink mixed with gall. When he had tasted it, he would not drink.
35
Walipokwisha kumsulibisha, waligawa mavazi yake, wakipiga kura; [ili litimie neno lililonenwa na nabii, Waligawa nguo zangu kati yao, na juu ya vazi langu walipiga kura.]
When they had crucified him, they divided his clothing among them, casting lots,{TR adds "that it might be fulfilled which was spoken by the prophet: 'They divided my garments among them, and for my clothing they cast lots;'" [see Psalm 22:18 and John 19:24]}
36
Wakaketi, wakamlinda huko.
and they sat and watched him there.
37
Wakaweka juu ya kichwa chake mashitaka yake, yaliyoandikwa HUYU NI YESU, MFALME WA WAYAHUDI.
They set up over his head the accusation against him written, "THIS IS JESUS, THE KING OF THE JEWS."
38
Wakati uo huo wanyang'anyi wawili wakasulibiwa pamoja naye, mmoja mkono wake wa kuume, na mmoja mkono wake wa kushoto.
Then there were two robbers crucified with him, one on his right hand and one on the left.
39
Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakitikisa-tikisa vichwa vyao, wakisema,
Those who passed by blasphemed him, wagging their heads,
40
Ewe mwenye kulivunja hekalu na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe nafsi yako; ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, shuka msalabani.
and saying, "You who destroy the temple, and build it in three days, save yourself! If you are the Son of God, come down from the cross!"
41
Kadhalika na wale wakuu wa makuhani wakamdhihaki pamoja na waandishi na wazee, wakisema, Aliokoa wengine, hawezi kujiokoa mwenyewe.
Likewise the chief priests also mocking, with the scribes, the Pharisees,{TR omits "the Pharisees"} and the elders, said,
42
Yeye ni mfalme wa Israeli; na ashuke sasa msalabani, nasi tutamwamini.
"He saved others, but he can't save himself. If he is the King of Israel, let him come down from the cross now, and we will believe in him.
43
Amemtegemea Mungu; na amwokoe sasa, kama anamtaka; kwa maana alisema, Mimi ni Mwana wa Mungu.
He trusts in God. Let God deliver him now, if he wants him; for he said, 'I am the Son of God.'"
44
Pia wale wanyang'anyi waliosulibiwa pamoja naye walimshutumu vile vile.
The robbers also who were crucified with him cast on him the same reproach.
45
Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa.
Now from the sixth hour{noon} there was darkness over all the land until the ninth hour.{3:00 P. M.}
46
Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
About the ninth hour Jesus cried with a loud voice, saying, "Eli, Eli, lima{TR reads "lama" instead of "lima"} sabachthani?" That is, "My God, my God, why have you forsaken me?"
47
Na baadhi yao waliohudhuria, waliposikia, walisema, Huyu anamwita Eliya.
Some of them who stood there, when they heard it, said, "This man is calling Elijah."
48
Mara mmoja wao akaenda mbio, akatwaa sifongo, akaijaza siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha.
Immediately one of them ran, and took a sponge, and filled it with vinegar, and put it on a reed, and gave him a drink.
49
Wale wengine wakasema, Acha; na tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.
The rest said, "Let him be. Let's see whether Elijah comes to save him."
50
Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.
Jesus cried again with a loud voice, and yielded up his spirit.
51
Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
Behold, the veil of the temple was torn in two from the top to the bottom. The earth quaked and the rocks were split.
52
makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;
The tombs were opened, and many bodies of the saints who had fallen asleep were raised;
53
nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.
and coming out of the tombs after his resurrection, they entered into the holy city and appeared to many.
54
Basi yule akida, na hao waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu, walipoliona tetemeko la nchi na mambo yaliyofanyika, wakaogopa sana, wakisema, Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.
Now the centurion, and those who were with him watching Jesus, when they saw the earthquake, and the things that were done, feared exceedingly, saying, "Truly this was the Son of God."
55
Palikuwa na wanawake wengi pale wakitazama kwa mbali, hao ndio waliomfuata Yesu toka Galilaya, na kumtumikia.
Many women were there watching from afar, who had followed Jesus from Galilee, serving him.
56
Miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo na Yusufu, na mama yao wana wa Zebedayo.
Among them were Mary Magdalene, Mary the mother of James and Joses, and the mother of the sons of Zebedee.
57
Hata ilipokuwa jioni akafika mtu tajiri wa Arimathaya, jina lake Yusufu, naye mwenyewe alikuwa mwanafunzi wa Yesu;
When evening had come, a rich man from Arimathaea, named Joseph, who himself was also Jesus' disciple came.
58
mtu huyu alimwendea Pilato akauomba mwili wa Yesu. Ndipo Pilato akaamuru apewe.
This man went to Pilate, and asked for Jesus' body. Then Pilate commanded the body to be given up.
59
Yusufu akautwaa mwili, akauzonga-zonga katika sanda ya kitani safi,
Joseph took the body, and wrapped it in a clean linen cloth,
60
akauweka katika kaburi lake jipya, alilokuwa amelichonga mwambani; akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
and laid it in his own new tomb, which he had hewn out in the rock, and he rolled a great stone to the door of the tomb, and departed.
61
Na pale walikuwapo Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, wameketi kulielekea kaburi.
Mary Magdalene was there, and the other Mary, sitting opposite the tomb.
62
Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato,
Now on the next day, which was the day after the Preparation Day, the chief priests and the Pharisees were gathered together to Pilate,
63
wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka.
saying, "Sir, we remember what that deceiver said while he was still alive: 'After three days I will rise again.'
64
Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamwiba, na kuwaambia watu, Amefufuka katika wafu; na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza.
Command therefore that the tomb be made secure until the third day, lest perhaps his disciples come at night and steal him away, and tell the people, 'He is risen from the dead;' and the last deception will be worse than the first."
65
Pilato akawaambia, Mna askari; nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo.
Pilate said to them, "You have a guard. Go, make it as secure as you can."
66
Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi.
So they went with the guard and made the tomb secure, sealing the stone.
« 26 28 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)