Mathayo 27 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mathayo 27 (Swahili) Matthew 27 (English)

Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua; Mathayo 27:1

Now when morning had come, all the chief priests and the elders of the people took counsel against Jesus to put him to death:

wakamfunga, wakamchukua, wakampeleka kwa Pilato aliyekuwa liwali. Mathayo 27:2

and they bound him, and led him away, and delivered him up to Pontius Pilate, the governor.

Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia. Mathayo 27:3

Then Judas, who betrayed him, when he saw that Jesus was condemned, felt remorse, and brought back the thirty pieces of silver to the chief priests and elders,

Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe. Mathayo 27:4

saying, "I have sinned in that I betrayed innocent blood." But they said, "What is that to us? You see to it."

Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga. Mathayo 27:5

He threw down the pieces of silver in the sanctuary, and departed. He went away and hanged himself.

Wakuu wa makuhani wakavitwaa vile vipande vya fedha, wakasema, Si halali kuviweka katika sanduku ya sadaka, kwa kuwa ni kima cha damu. Mathayo 27:6

The chief priests took the pieces of silver, and said, "It's not lawful to put them into the treasury, since it is the price of blood."

Wakafanya shauri, wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni. Mathayo 27:7

They took counsel, and bought the potter's field with them, to bury strangers in.

Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo. Mathayo 27:8

Therefore that field was called "The Field of Blood" to this day.

Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima; Mathayo 27:9

Then that which was spoken through Jeremiah the prophet was fulfilled, saying, "They took the thirty pieces of silver, The price of him upon whom a price had been set, Whom some of the children of Israel priced,

wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza. Mathayo 27:10

And they gave them for the potter's field, As the Lord commanded me."

Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, Wewe wasema. Mathayo 27:11

Now Jesus stood before the governor: and the governor asked him, saying, "Are you the King of the Jews?" Jesus said to him, "So you say."

Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno. Mathayo 27:12

When he was accused by the chief priests and elders, he answered nothing.

Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia? Mathayo 27:13

Then Pilate said to him, "Don't you hear how many things they testify against you?"

Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana. Mathayo 27:14

He gave him no answer, not even one word, so that the governor marveled greatly.

Basi wakati wa siku kuu, liwali desturi yake huwafungulia mkutano mfungwa mmoja waliyemtaka. Mathayo 27:15

Now at the feast the governor was accustomed to release to the multitude one prisoner, whom they desired.

Basi palikuwa na mfungwa mashuhuri siku zile, aitwaye Baraba. Mathayo 27:16

They had then a notable prisoner, called Barabbas.

Basi walipokutanika, Pilato akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi? Yule Baraba, au Yesu aitwaye Kristo? Mathayo 27:17

When therefore they were gathered together, Pilate said to them, "Whom do you want me to release to you? Barabbas, or Jesus, who is called Christ?"

Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda. Mathayo 27:18

For he knew that because of envy they had delivered him up.

Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake. Mathayo 27:19

While he was sitting on the judgment seat, his wife sent to him, saying, "Have nothing to do with that righteous man, for I have suffered many things this day in a dream because of him."

Nao wakuu wa makuhani na wazee wakawashawishi makutano ili wamtake Baraba, na kumwangamiza Yesu. Mathayo 27:20

Now the chief priests and the elders persuaded the multitudes to ask for Barabbas, and destroy Jesus.

Basi liwali akajibu, akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi katika hawa wawili? Wakasema, Baraba. Mathayo 27:21

But the governor answered them, "Which of the two do you want me to release to you?" They said, "Barabbas!"

Pilato akawaambia, Basi, nimtendeje Yesu aitwaye Kristo? Wakasema wote, Asulibiwe. Mathayo 27:22

Pilate said to them, "What then shall I do to Jesus, who is called Christ?" They all said to him, "Let him be crucified!"

Akasema, Kwani? Ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, wakisema, Na asulibiwe. Mathayo 27:23

But the governor said, "Why? What evil has he done?" But they cried out exceedingly, saying, "Let him be crucified!"

Basi Pilato alipoona ya kuwa hafai lo lote, bali ghasia inazidi tu, akatwaa maji, akanawa mikono yake mbele ya mkutano, akasema, Mimi sina hatia katika damu ya mtu huyu mwenye haki; yaangalieni haya ninyi wenyewe. Mathayo 27:24

So when Pilate saw that nothing was being gained, but rather that a disturbance was starting, he took water, and washed his hands before the multitude, saying, "I am innocent of the blood of this righteous person. You see to it."

Watu wote wakajibu wakasema, Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu. Mathayo 27:25

All the people answered, "May his blood be on us, and on our children!"

Ndipo akawafungulia Baraba; na baada ya kumpiga Yesu mijeledi, akamtoa ili asulibiwe. Mathayo 27:26

Then he released to them Barabbas, but Jesus he flogged and delivered to be crucified.

Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima. Mathayo 27:27

Then the governor's soldiers took Jesus into the Praetorium, and gathered the whole garrison together against him.

Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu. Mathayo 27:28

They stripped him, and put a scarlet robe on him.

Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi! Mathayo 27:29

They braided a crown of thorns and put it on his head, and a reed in his right hand; and they kneeled down before him, and mocked him, saying, "Hail, King of the Jews!"

Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani. Mathayo 27:30

They spat on him, and took the reed and struck him on the head.

Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha. Mathayo 27:31

When they had mocked him, they took the robe off of him, and put his clothes on him, and led him away to crucify him.

Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake. Mathayo 27:32

As they came out, they found a man of Cyrene, Simon by name, and they compelled him to go with them, that he might carry his cross.

Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa, Mathayo 27:33

They came to a place called "Golgotha," that is to say, "The place of a skull."

wakampa kunywa divai iliyochanganyika na nyongo; lakini yeye alipoionja hakutaka kunywa. Mathayo 27:34

They gave him sour wine to drink mixed with gall. When he had tasted it, he would not drink.

Walipokwisha kumsulibisha, waligawa mavazi yake, wakipiga kura; [ili litimie neno lililonenwa na nabii, Waligawa nguo zangu kati yao, na juu ya vazi langu walipiga kura.] Mathayo 27:35

When they had crucified him, they divided his clothing among them, casting lots,{TR adds "that it might be fulfilled which was spoken by the prophet: 'They divided my garments among them, and for my clothing they cast lots;'" [see Psalm 22:18 and John 19:24]}

Wakaketi, wakamlinda huko. Mathayo 27:36

and they sat and watched him there.

Wakaweka juu ya kichwa chake mashitaka yake, yaliyoandikwa HUYU NI YESU, MFALME WA WAYAHUDI. Mathayo 27:37

They set up over his head the accusation against him written, "THIS IS JESUS, THE KING OF THE JEWS."

Wakati uo huo wanyang'anyi wawili wakasulibiwa pamoja naye, mmoja mkono wake wa kuume, na mmoja mkono wake wa kushoto. Mathayo 27:38

Then there were two robbers crucified with him, one on his right hand and one on the left.

Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakitikisa-tikisa vichwa vyao, wakisema, Mathayo 27:39

Those who passed by blasphemed him, wagging their heads,

Ewe mwenye kulivunja hekalu na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe nafsi yako; ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, shuka msalabani. Mathayo 27:40

and saying, "You who destroy the temple, and build it in three days, save yourself! If you are the Son of God, come down from the cross!"

Kadhalika na wale wakuu wa makuhani wakamdhihaki pamoja na waandishi na wazee, wakisema, Aliokoa wengine, hawezi kujiokoa mwenyewe. Mathayo 27:41

Likewise the chief priests also mocking, with the scribes, the Pharisees,{TR omits "the Pharisees"} and the elders, said,

Yeye ni mfalme wa Israeli; na ashuke sasa msalabani, nasi tutamwamini. Mathayo 27:42

"He saved others, but he can't save himself. If he is the King of Israel, let him come down from the cross now, and we will believe in him.

Amemtegemea Mungu; na amwokoe sasa, kama anamtaka; kwa maana alisema, Mimi ni Mwana wa Mungu. Mathayo 27:43

He trusts in God. Let God deliver him now, if he wants him; for he said, 'I am the Son of God.'"

Pia wale wanyang'anyi waliosulibiwa pamoja naye walimshutumu vile vile. Mathayo 27:44

The robbers also who were crucified with him cast on him the same reproach.

Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa. Mathayo 27:45

Now from the sixth hour{noon} there was darkness over all the land until the ninth hour.{3:00 P. M.}

Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Mathayo 27:46

About the ninth hour Jesus cried with a loud voice, saying, "Eli, Eli, lima{TR reads "lama" instead of "lima"} sabachthani?" That is, "My God, my God, why have you forsaken me?"

Na baadhi yao waliohudhuria, waliposikia, walisema, Huyu anamwita Eliya. Mathayo 27:47

Some of them who stood there, when they heard it, said, "This man is calling Elijah."

Mara mmoja wao akaenda mbio, akatwaa sifongo, akaijaza siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha. Mathayo 27:48

Immediately one of them ran, and took a sponge, and filled it with vinegar, and put it on a reed, and gave him a drink.

Wale wengine wakasema, Acha; na tuone kama Eliya anakuja kumwokoa. Mathayo 27:49

The rest said, "Let him be. Let's see whether Elijah comes to save him."

Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. Mathayo 27:50

Jesus cried again with a loud voice, and yielded up his spirit.

Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka; Mathayo 27:51

Behold, the veil of the temple was torn in two from the top to the bottom. The earth quaked and the rocks were split.

makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; Mathayo 27:52

The tombs were opened, and many bodies of the saints who had fallen asleep were raised;

nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi. Mathayo 27:53

and coming out of the tombs after his resurrection, they entered into the holy city and appeared to many.

Basi yule akida, na hao waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu, walipoliona tetemeko la nchi na mambo yaliyofanyika, wakaogopa sana, wakisema, Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu. Mathayo 27:54

Now the centurion, and those who were with him watching Jesus, when they saw the earthquake, and the things that were done, feared exceedingly, saying, "Truly this was the Son of God."

Palikuwa na wanawake wengi pale wakitazama kwa mbali, hao ndio waliomfuata Yesu toka Galilaya, na kumtumikia. Mathayo 27:55

Many women were there watching from afar, who had followed Jesus from Galilee, serving him.

Miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo na Yusufu, na mama yao wana wa Zebedayo. Mathayo 27:56

Among them were Mary Magdalene, Mary the mother of James and Joses, and the mother of the sons of Zebedee.

Hata ilipokuwa jioni akafika mtu tajiri wa Arimathaya, jina lake Yusufu, naye mwenyewe alikuwa mwanafunzi wa Yesu; Mathayo 27:57

When evening had come, a rich man from Arimathaea, named Joseph, who himself was also Jesus' disciple came.

mtu huyu alimwendea Pilato akauomba mwili wa Yesu. Ndipo Pilato akaamuru apewe. Mathayo 27:58

This man went to Pilate, and asked for Jesus' body. Then Pilate commanded the body to be given up.

Yusufu akautwaa mwili, akauzonga-zonga katika sanda ya kitani safi, Mathayo 27:59

Joseph took the body, and wrapped it in a clean linen cloth,

akauweka katika kaburi lake jipya, alilokuwa amelichonga mwambani; akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake. Mathayo 27:60

and laid it in his own new tomb, which he had hewn out in the rock, and he rolled a great stone to the door of the tomb, and departed.

Na pale walikuwapo Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, wameketi kulielekea kaburi. Mathayo 27:61

Mary Magdalene was there, and the other Mary, sitting opposite the tomb.

Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato, Mathayo 27:62

Now on the next day, which was the day after the Preparation Day, the chief priests and the Pharisees were gathered together to Pilate,

wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka. Mathayo 27:63

saying, "Sir, we remember what that deceiver said while he was still alive: 'After three days I will rise again.'

Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamwiba, na kuwaambia watu, Amefufuka katika wafu; na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza. Mathayo 27:64

Command therefore that the tomb be made secure until the third day, lest perhaps his disciples come at night and steal him away, and tell the people, 'He is risen from the dead;' and the last deception will be worse than the first."

Pilato akawaambia, Mna askari; nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo. Mathayo 27:65

Pilate said to them, "You have a guard. Go, make it as secure as you can."

Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi. Mathayo 27:66

So they went with the guard and made the tomb secure, sealing the stone.