Mathayo 25

Matthew Chapter 25

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.
"Then the Kingdom of Heaven will be like ten virgins, who took their lamps, and went out to meet the bridegroom.
2
Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.
Five of them were foolish, and five were wise.
3
Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao;
Those who were foolish, when they took their lamps, took no oil with them,
4
bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.
but the wise took oil in their vessels with their lamps.
5
Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.
Now while the bridegroom delayed, they all slumbered and slept.
6
Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.
But at midnight there was a cry, 'Behold! The bridegroom is coming! Come out to meet him!'
7
Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.
Then all those virgins arose, and trimmed their lamps.
8
Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.
The foolish said to the wise, 'Give us some of your oil, for our lamps are going out.'
9
Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.
But the wise answered, saying, 'What if there isn't enough for us and you? You go rather to those who sell, and buy for yourselves.'
10
Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
While they went away to buy, the bridegroom came, and those who were ready went in with him to the marriage feast, and the door was shut.
11
Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.
Afterward the other virgins also came, saying, 'Lord, Lord, open to us.'
12
Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.
But he answered, 'Most assuredly I tell you, I don't know you.'
13
Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.
Watch therefore, for you don't know the day nor the hour in which the Son of Man is coming.
14
Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake.
"For it is like a man, going into another country, who called his own servants, and entrusted his goods to them.
15
Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri.
To one he gave five talents, to another two, to another one; to each according to his own ability. Then he went on his journey.
16
Mara yule aliyepokea talanta tano akaenda, akafanya biashara nazo, akachuma faida talanta nyingine tano.
Immediately he who received the five talents went and traded with them, and made another five talents.
17
Vile vile na yule mwenye mbili, yeye naye akachuma nyingine mbili faida.
In like manner he also who got the two gained another two.
18
Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake.
But he who received the one went away and dug in the earth, and hid his lord's money.
19
Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.
"Now after a long time the lord of those servants came, and reconciled accounts with them.
20
Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida.
He who received the five talents came and brought another five talents, saying, 'Lord, you delivered to me five talents. Behold, I have gained another five talents besides them.'
21
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.
"His lord said to him, 'Well done, good and faithful servant. You have been faithful over a few things, I will set you over many things. Enter into the joy of your lord.'
22
Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida.
"He also who got the two talents came and said, 'Lord, you delivered to me two talents. Behold, I have gained another two talents besides them.'
23
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.
"His lord said to him, 'Well done, good and faithful servant. You have been faithful over a few things, I will set you over many things. Enter into the joy of your lord.'
24
Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;
"He also who had received the one talent came and said, 'Lord, I knew you that you are a hard man, reaping where you did not sow, and gathering where you did not scatter.
25
basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako.
I was afraid, and went away and hid your talent in the earth. Behold, you have what is yours.'
26
Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;
"But his lord answered him, 'You wicked and slothful servant. You knew that I reap where I didn't sow, and gather where I didn't scatter.
27
basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.
You ought therefore to have deposited my money with the bankers, and at my coming I should have received back my own with interest.
28
Basi, mnyang'anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.
Take away therefore the talent from him, and give it to him who has the ten talents.
29
Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa.
For to everyone who has will be given, and he will have abundance, but from him who has not, even that which he has will be taken away.
30
Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Throw out the unprofitable servant into the outer darkness, where there will be weeping and gnashing of teeth.'
31
Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;
"But when the Son of Man comes in his glory, and all the holy angels with him, then he will sit on the throne of his glory.
32
na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;
Before him all the nations will be gathered, and he will separate them one from another, as a shepherd separates the sheep from the goats.
33
atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.
He will set the sheep on his right hand, but the goats on the left.
34
Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;
Then the King will tell those on his right hand, 'Come, blessed of my Father, inherit the Kingdom prepared for you from the foundation of the world;
35
kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;
for I was hungry, and you gave me food to eat; I was thirsty, and you gave me drink; I was a stranger, and you took me in;
36
nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.
naked, and you clothed me; I was sick, and you visited me; I was in prison, and you came to me.'
37
Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?
"Then the righteous will answer him, saying, 'Lord, when did we see you hungry, and feed you; or thirsty, and give you a drink?
38
Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?
When did we see you as a stranger, and take you in; or naked, and clothe you?
39
Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?
When did we see you sick, or in prison, and come to you?'
40
Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.
"The King will answer them, 'Most assuredly I tell you, inasmuch as you did it to one of the least of these my brothers{The word for "brothers" here may be also correctly translated "brothers and sisters" or "siblings."}, you did it to me.'
41
Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;
Then he will say also to those on the left hand, 'Depart from me, you cursed, into the eternal fire which is prepared for the devil and his angels;
42
kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;
for I was hungry, and you didn't give me food to eat; I was thirsty, and you gave me no drink;
43
nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.
I was a stranger, and you didn't take me in; naked, and you didn't clothe me; sick, and in prison, and you didn't visit me.'
44
Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?
"Then they will also answer, saying, 'Lord, when did we see you hungry, or thirsty, or a stranger, or naked, or sick, or in prison, and didn't help you?'
45
Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.
"Then he will answer them, saying, 'Most assuredly I tell you, inasmuch as you didn't do it to one of the least of these, you didn't do it to me.'
46
Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.
These will go away into eternal punishment, but the righteous into eternal life."
« 24 26 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)