1 Samweli 11 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 11 (Swahili) 1st Samuel 11 (English)

Ikawa, kama baada ya mwezi mmoja, Nahashi, Mwamoni ,akakwea na kupanga marago juu ya Yabesh-gileadi;na watu wote wa Yabeshi wakamwambia Nahashi, Fanya mapatano nasi,na sisi tutakutumikia. 1 Samweli 11:1

Then Nahash the Ammonite came up, and encamped against Jabesh Gilead: and all the men of Jabesh said to Nahash, Make a covenant with us, and we will serve you.

Huyo Nahashi, Mwamoni, akawaambia, Kwa sharti hii mimi nitapatana nanyi, kila mtu ang'olewe jicho la kuume; na kwa jambo hilo nitawashutumu Waisraeli wote pia. 1 Samweli 11:2

Nahash the Ammonite said to them, On this condition will I make it with you, that all your right eyes be put out; and I will lay it for a reproach on all Israel.

Basi wazee wa Yabeshi wakamjibu, Tuachie siku saba, ili tutume wajumbe waende mipakani mwote mwa Israeli; kisha, ikiwa hakuna atakayetuokoa, tutakutokea. 1 Samweli 11:3

The elders of Jabesh said to him, Give us seven days' respite, that we may send messengers to all the borders of Israel; and then, if there be none to save us, we will come out to you.

Hivyo wajumbe wakafika Gibea ya Sauli, wakasema maneno hayo masikioni mwa watu; na watu wote wakainua sauti zao wakalia. 1 Samweli 11:4

Then came the messengers to Gibeah of Saul, and spoke these words in the ears of the people: and all the people lifted up their voice, and wept.

Na tazama, Sauli akaja akifuata ng'ombe kutoka kondeni; naye Sauli akauliza, Watu hawa wana nini, hata wakalia? Wakamwambia maneno ya watu wale wa Yabeshi. 1 Samweli 11:5

Behold, Saul came following the oxen out of the field; and Saul said, What ails the people that they weep? They told him the words of the men of Jabesh.

Na roho ya Mungu ikamjilia Sauli kwa nguvu, hapo alipoyasikia maneno yale, na hasira yake ikawaka sana. 1 Samweli 11:6

The Spirit of God came mightily on Saul when he heard those words, and his anger was kindled greatly.

Naye akatwaa jozi ya ng'ombe, akawakata-kata vipande, kisha akavipeleka vile vipande mipakani mwote mwa Israeli kwa mikono ya wajumbe, kusema, Ye yote asiyetoka nyuma ya Sauli na Samweli, ng'ombe zake watatendwa vivi hivi. Basi utisho wa Bwana ukawaangukia wale watu, wakatoka kama mtu mmoja. 1 Samweli 11:7

He took a yoke of oxen, and cut them in pieces, and sent them throughout all the borders of Israel by the hand of messengers, saying, Whoever doesn't come forth after Saul and after Samuel, so shall it be done to his oxen. The dread of Yahweh fell on the people, and they came out as one man.

Naye akawahesabu huko Bezeki; Waisraeli walikuwa mia tatu elfu, na Wayuda thelathini elfu. 1 Samweli 11:8

He numbered them in Bezek; and the children of Israel were three hundred thousand, and the men of Judah thirty thousand.

Nao wakawaambia hao wajumbe waliokuja, Waambieni watu wa Yabesh-gileadi, Kesho, wakati wa jua kali, mtapata wokovu. Basi wale wajumbe wakaenda, wakawaarifu watu wa Yabeshi; nao walifurahiwa. 1 Samweli 11:9

They said to the messengers who came, Thus shall you tell the men of Jabesh Gilead, Tomorrow, by the time the sun is hot, you shall have deliverance. The messengers came and told the men of Jabesh; and they were glad.

Kwa hiyo watu wa Yabeshi walisema, Kesho tutawatokea, nanyi mtatufanyia yote myaonayo kuwa ni mema. 1 Samweli 11:10

Therefore the men of Jabesh said, Tomorrow we will come out to you, and you shall do with us all that seems good to you.

Ikawa, kesho yake, Sauli akawapanga watu katika vikosi vitatu; nao wakaingia katikati ya marago kwenye zamu ya asubuhi, wakawapiga Waamoni hata wakati wa jua kali; kisha ikawa wale waliosalia wakatawanyika, hata wasiachwe wawili wao pamoja. 1 Samweli 11:11

It was so on the next day, that Saul put the people in three companies; and they came into the midst of the camp in the morning watch, and struck the Ammonites until the heat of the day: and it happened, that those who remained were scattered, so that no two of them were left together.

Ndipo watu walipomwambia Samweli, Ni nani yule aliyesema, Je! Huyo Sauli atatutawala? Walete watu hao, ili tuwaue. 1 Samweli 11:12

The people said to Samuel, Who is he who said, Shall Saul reign over us? bring the men, that we may put them to death.

Lakini Sauli akasema, Hakuna mtu atakayeuawa leo, maana leo Bwana amefanya wokovu katika Israeli. 1 Samweli 11:13

Saul said, There shall not a man be put to death this day; for today Yahweh has worked deliverance in Israel.

Kisha Samweli akawaambia watu, Haya! Na twendeni mpaka Gilgali, ili tuuimarishe ufalme huko mara ya pili. 1 Samweli 11:14

Then said Samuel to the people, Come, and let us go to Gilgal, and renew the kingdom there.

Nao watu wote wakaenda Gilgali; wakamtawaza Sauli mbele za Bwana huko Gilgali; wakachinja sadaka za amani mbele za Bwana; na huko Sauli na watu wote wa Israeli wakafurahi sana. 1 Samweli 11:15

All the people went to Gilgal; and there they made Saul king before Yahweh in Gilgal; and there they offered sacrifices of peace-offerings before Yahweh; and there Saul and all the men of Israel rejoiced greatly.