Sifa Lyrics

Mungu Wa Ibada by Ambwene Mwasongwe cover art

Ambwene Mwasongwe - Mungu Wa Ibada Lyrics

Artist:
Ambwene Mwasongwe

Lyrics

Wewe ni wengu, wewe ndiwe
Ulikuweko kabla ya mwanzo
Ulikuweko kabla ya miaka
Ndiwe uliweka mbingu za mbingu
Ulimweka kerubi 
Akuabudu akafunika kiti 
Kwa mbawa zake mlima wa moto
Wenye mawe ya moto akaabudu 
Utukufu ukaonekana 
Ila ukatazama moyo wa kerubi 
Akajichuuza akajivuna
Uovu  ukaone kana ndani yake 
Akang’olewa akafukuzwa ibada ikaendelea
Maana wewe ni mungu mungu wa ibada


Ndipo ukaumba mtu kwa mfano wako, na sura yako
Ndipo ukamweka bustani ya edeni ukamtembelea
Ukaongea naye akakuabudu 
Mungu wa ibada, wewe ni mungu
Mungu wa ibada


Wewe ni mungu chanzo cha vyote
Wewe ni bwana, injini ya vitu/vyote
Ndio maana wewe haulali
Ndio sababu, wewe husinzii
Siku ukilala itakuwa kasheshe 
Maana  vilivyolala vyote vitaamka
Vilivyo macho naamini vitalala
Itakuwa kasheshe na mtikisiko
Dude la baharini ndipo litaamka 
Nani atalifunga joka lewithani ?
Bahari itakiuka sharia iliyowekewa nchi itakiuka
Amri uliyoipa vitu vyote vitakwenda 
Bila sheria maana mweny sheria
Utakuwa umelala, asante maana hulali
Asante maana husinzii wewe ni injini
Ya kuendesha vitu vyote bwana unaweza
Bwana una nguvu 


Wewe ni mungu wa ibada
Wewe ni bwana muumbaji 
Sheria zote umeweka 
Wewe ni bwana wa vitu vyote
Aaah aaaah aaah aaaah
Aaah aaaah aaah aaaah


Wewe ni mungu usiyeshindwa 
Huhitaji jeshi kushinda vita
Huhitaji vingi kushibisha watu
Huhitaji mawe magumu kushinda
Daudi na mawe yake yale matano
Alitumia moja kwa jina la bwana
Chupa ya mafuta ilikuwa ndogo
Ila ilitosha kujaza mapipa
Watu wanne, tena wakoma na visigino vyao
Wakasikizisha vishindo, kwa jina la bwana
Jeshi likakimbia likaachia nyara
Huhitaji mapanga mengi, kuwapiga watu jeuri
Kwa malaika mmoja, wazaliwa wa kwanza walikufa
Farao alikoma, akamwambia musa nendeni
Kwawabudu Jehova, maana yeye peke yake ni mungu
Aaah wewe ni mungu, mungu wa ibada


Bwana tubaariki utulinde sote
Utupe roho wako, atuogeze kwa Yesu
Amen amen aameh
Kweli atukuzwe 
Yesu ndiye bwana tu yeye utubariki 


Wewe ni mungu wa ibada
Wewe ni bwana muumbaji 
Sheria zote umeweka 
Wewe ni bwana wa vitu vyote
Aaah aaaah aaah aaaah
Aaah aaaah aaah aaaah


Video