Ambwene Mwasongwe - Unikumbuke Lyrics
Lyrics
Nimekuita uambie watu ushuhuda wangu Miaka tisa nimekaa jela Nilifungwa kwa kosa la kusingiziwa Namshukuru Mungu nimetoka
Usiku ule nilikamatwa kama mchezo Na mke wangu na mtoto mdogo Nikadhani labda walikuwa wanatania Labda ilikuwa siku ya wajinga
Hakuna mtu alielewa ukweli wa ushahidi wangu Wala sikuwa na wakumweleza akanielewa Mazingira ya kesi, ushahidi, sheria za kazi Siri ni ban, mpaka mke wangu kaniambia Kama umefanya kiri kosa tujue moja
Nikumbuke, kumbuka haki yangu, sikufanya ubaya Nikumbuke, nikumbuke, sikufanya ubaya Nikumbuke, namna walivyonishtaki kwa hila na wivu Nikumbuke, bwana unikumbuke nililia
Hey, kumbuka bwana haki yangu Hey, wakumbuke, walivyo kufanikiwa jela Uwakumbuke, Mungu wakumbuke washa mshumaa ndani ya nyumba Mkumbuke mtoto mchanga asiye na hatia Uwakumbuke, kama ningekuwepo angekonda Kumbuka Adam, aliyebaki, alikufanya kushtuka kwa ajili yako
Nilidhani Mungu kalisahau faili langu Nikadhani kwamba nitaaibika Sikuwa tena na tumaini lililobaki Haki yangu ilikuwa tumaini pekee
Waweza elewa shahidi wangu alikuwa Mungu Labda na wale walioua Mwisho wa siku Mungu alinitetea Na waliofanya kosa kunikana
Haki yangu ikasitana kama mtende na mwelezi Pale banoni, walinichimba wakuning'oa sababu ya Mungu Waliinamisha wakunivunja, walinitikisa sikupukutika Walinichuma ili niishe Wewe bwana ulinitetea na haki yangu
Nikumbuke, kumbuka maadui walivyonizunguka Nikumbuke, kumbuka ushahidi wa maneno yao Nikumbuke, kumbuka walivyonichafua jina langu Nikumbuke, kumbuka walivyoniona Mi ni mhalifu, hey ukalisafishe jina langu
Hey bwana, uwakumbuke! Uwakumbuke Ukarehemu makosa yao Uwakumbuke! Japo walifanya ubaya bwana na uwasamehe Uwakumbuke! Nilienda jela nikiwa bado sikujui Uwakumbuke! Nimetoka nimeokoka nimekujua Nikumbuke! Bwana unikumbuke usinisahau
Natengeza fadhili zako, niimbe Mungu baba Nimefurahi, niimbe Mungu bwana Nimefurahi, niimbe Mungu bwana Nimefurahi, niimbe Mungu bwana Nimefurahi, niimbe Mungu bwana
Video
Ambwene Mwasongwe - Unikumbuke (Official Music Video)