Nimeachilia Lyrics - Ambwene Mwasongwe
Ambwene Mwasongwe swahili
Chorus:
Eeh
Nimeachilia
jifunze kuambia moyo wako
Nimeachilia
hatakama inauma sana jifunze kusema
Nimeachilia
Nimesamehe Mungu anaona mimi
Nimeachilia
Nimeachilia Video
Nimeachilia Lyrics
Ulipanda mti mzuri ukategemea kuvuna matunda
ila mti wenyewe umezaa miiba na michongoma
Uliwekeza muda na mali,ukamwagilia ukitarajia
matarajio yamekuwa sio sasa umebaki na maumivu
japokuwa uliiona miiba,ulijipa muda ukapogolea
ukitarajia mabadiliko,labda kesho mti utazaa
sasa imekuwa kinyume,mti wako mwenyewe unakuchoma
Unalia
Aaah ah
ukikumbuka Mbegu
Aaah ah
Unalia
Aaah ah
ukikumbuka maji
Unalia
Aaah ah
ukikumbuka kazi
Aaah ah
Sio kila kinachokuja kwako ni chako
na si kiondokacho kwako ni chako
hata kama unavipenda sio vyako
vingine mungu huviondoa, ili wewe ubaki salama
iwe kazi,nafsi,mahusiano au cheo
japo vyaondoka kwa maumivu ili jifunze kuacha viende
nafasi ya moyo wako mpe mungu
Chochote kile kikuumizacho kufikia hatua ya kukuua
jua ulikikalisha mahali pa mungu
jifunze kukiacha kiende,jifunze kusema Bye Bye
maana sio vyote vya kwako
Walitoka kwetu hawakuwa wa kwetu
maana wangelikuwa wetu wangelikaa nasi
walitoka ili wafunuliwe sio wote wa kwetu
Walitoka kwetu hawakuwa wa kwetu
maana wangelikuwa wetu wangelikaa nasi
wafunuliwa ili tujue sio wote wa kwetu
Eeh
Nimeachilia
jifunze kuambia moyo wako
Nimeachilia
hatakama inauma sana jifunze kusema
Nimeachilia
Nimesamehe Mungu anaona mimi
Nimeachilia
Tafuta mahali kaa pekee Yako Mahali Hakuna akuonaye
Mahali pa siri pa utulivu,mahali hakuna akusikiaye
ukakumbuke machungu yako,maumivu yako na machozi yako
kayakumbuke maneno yote yakuumizayo moyo wako
kayakumbuke vitu ulivyopoteza,kayakumbuke muda na watu wa karibu
kakumbuke hasara uliyopata,usiyasahau machungu yote
Lia usibakishe machozi
lia usiyameze yeyote
toa yanayousibu moyo
toa yasibakiye yeyote
Aaaah ah ah ah aaah ah
toa usibaki na machungu
hakikisha umetuliza moyo,umesahau yote yaliyopita
achilia yote uloshikilia waache waende sio Riziki yako
hakikisha umekuwa mwepesi ji-edit,moyo ubaki salama
Inuka sema kwa ujasiri
Nimeachilia ninaanza upya
Inuka jikung'ute mavumbi ya kale
yamepita sasa ni mapya
Nimeachilia sema
Nimeachilia
Nimesamehe yote
Nimeachilia
Nimejinyonyoa manyoya ya kale sasa ni mwepesi
Nimeachilia
Sasa niko Huru
Aah ah aah aaah aah
Nimeachilia
Nimesamehea sasa ninayo amani Ooh oh o
maumivu ya kale nimeacha nyuma
Nimeachilia