Yeremia 48 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yeremia 48 (Swahili) Jeremiah 48 (English)

Habari za Moabu. Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Ole wake Nebo! Kwa maana umeharibika; Kiriathaimu umeaibishwa, umetwaliwa; Misgabu umeaibishwa, nao umebomolewa. Yeremia 48:1

Of Moab. Thus says Yahweh of Hosts, the God of Israel: Woe to Nebo! for it is laid waste; Kiriathaim is disappointed, it is taken; Misgab is put to shame and broken down.

Sifa za Moabu haziko tena; katika Heshboni wameazimia mabaya juu yake, Haya! Njoni, na tumkatilie mbali asiwe taifa. Wewe nawe, Ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia. Yeremia 48:2

The praise of Moab is no more; in Heshbon they have devised evil against her: Come, and let us cut her off from being a nation. You also, Madmen, shall be brought to silence: the sword shall pursue you.

Sauti ya kilio toka Horonaimu, Ya kutekwa na uharibifu mkuu. Yeremia 48:3

The sound of a cry from Horonaim, desolation and great destruction!

Moabu umeharibika; Wadogo wake wamewasikiza watu kilio. Yeremia 48:4

Moab is destroyed; her little ones have caused a cry to be heard.

Kwa maana watu wapandapo huko Luhithi Watapanda wasiache kulia; Nao watu watelemkapo huko Horonaimu Wameisikia huzuni ya kilio cha uharibifu. Yeremia 48:5

For by the ascent of Luhith with continual weeping shall they go up; for at the descent of Horonaim they have heard the distress of the cry of destruction.

Haya! Kimbieni! Jiokoeni nafsi zenu! Mkawe kama mtu aliye mkiwa. Yeremia 48:6

Flee, save your lives, and be like the heath in the wilderness.

Maana, kwa kuwa umeyatumainia matendo yako, na hazina zako, wewe nawe utatwaliwa; na Kemoshi atatoka aende katika uhamisho, makuhani wake na wakuu wake pamoja. Yeremia 48:7

For, because you have trusted in your works and in your treasures, you also shall be taken: and Chemosh shall go forth into captivity, his priests and his princes together.

Naye mwenye kuteka nyara atakuja juu ya kila mji, wala hapana mji utakaookoka; bonde nalo litaangamia, nayo nchi tambarare itaharibiwa; kama Bwana alivyosema. Yeremia 48:8

The destroyer shall come on every city, and no city shall escape; the valley also shall perish, and the plain shall be destroyed; as Yahweh has spoken.

Mpe Moabu mabawa, apate kuruka na kwenda zake; na miji yake itakuwa ukiwa, isiwe na mtu wa kukaa ndani yake. Yeremia 48:9

Give wings to Moab, that she may fly and get her away: and her cities shall become a desolation, without any to dwell therein.

Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu; na alaaniwe auzuiaye upanga wake usimwage damu. Yeremia 48:10

Cursed be he who does the work of Yahweh negligently; and cursed be he who keeps back his sword from blood.

Moabu amestarehe tangu ujana wake, naye ametulia juu ya sira zake, wala hakumiminwa kutoka chombo kimoja kutiwa chombo kingine, wala hakwenda kufungwa; kwa hiyo ladha yake anakaa nayo, wala harufu yake haikubadilika. Yeremia 48:11

Moab has been at ease from his youth, and he has settled on his lees, and has not been emptied from vessel to vessel, neither has he gone into captivity: therefore his taste remains in him, and his scent is not changed.

Basi, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo nitampelekea wamiminao, nao watammimina, nao watamwaga vyote vilivyomo vyomboni mwake, na kuzivunja chupa zake vipande vipande. Yeremia 48:12

Therefore, behold, the days come, says Yahweh, that I will send to him those who pour off, and they shall pour him off; and they shall empty his vessels, and break their bottles in pieces.

Na Moabu ataona haya kwa ajili ya Kemoshi, kama nyumba ya Israeli ilivyoona haya kwa ajili ya Betheli, matumaini yao. Yeremia 48:13

Moab shall be ashamed of Chemosh, as the house of Israel was ashamed of Bethel their confidence.

Mwasemaje ninyi, Sisi tu mashujaa, watu hodari wa vita. Yeremia 48:14

How say you, We are mighty men, and valiant men for the war?

Moabu ameharibika, na moshi wa miji yake umepanda; na vijana wake wateule wametelemka kwenda kuchinjwa, asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana wa majeshi. Yeremia 48:15

Moab is laid waste, and they are gone up into his cities, and his chosen young men are gone down to the slaughter, says the King, whose name is Yahweh of Hosts.

Msiba wa Moabu umefika karibu, Na mateso yake yanafanya haraka. Yeremia 48:16

The calamity of Moab is near to come, and his affliction hurries fast.

Ninyi nyote mnaomzunguka, mlilieni, Nanyi nyote mlijuao jina lake, semeni, Jinsi ilivyovunjika fimbo ya enzi, Fimbo ile iliyokuwa nzuri! Yeremia 48:17

All you who are round about him, bemoan him, and all you who know his name; say, How is the strong staff broken, the beautiful rod!

Ee binti ukaaye Diboni, Shuka toka utukufu wako, ukae katika kiu; Maana atekaye Moabu amepanda juu yako, Ameziharibu ngome zako. Yeremia 48:18

You daughter who dwells in Dibon, come down from your glory, and sit in thirst; for the destroyer of Moab is come up against you, he has destroyed your strongholds.

Wewe ukaaye Aroeri, Simama kando ya njia upeleleze; Mwulize mwanamume akimbiaye na mwanamke atorokaye, Sema, Imetendeka nini? Yeremia 48:19

Inhabitant of Aroer, stand by the way, and watch: ask him who flees, and her who escapes; say, What has been done?

Moabu ameaibishwa, kwa maana amevunjika; Pigeni yowe na kulia; Tangazeni habari hii katika Arnoni, Ya kuwa Moabu ameharibika. Yeremia 48:20

Moab is disappointed; for it is broken down: wail and cry; tell you it by the Arnon, that Moab is laid waste.

Na hukumu imeifikilia nchi tambarare; juu ya Holoni, na juu ya Yasa, na juu ya Mefaathi; Yeremia 48:21

Judgment is come on the plain country, on Holon, and on Jahzah, and on Mephaath,

na juu ya Diboni, na juu ya Nebo, na juu ya Beth-diblathaimu; Yeremia 48:22

and on Dibon, and on Nebo, and on Beth Diblathaim,

na juu ya Kiriathaimu, na juu ya Beth-gamuli, na juu ya Beth-meoni; Yeremia 48:23

and on Kiriathaim, and on Beth Gamul, and on Beth Meon,

na juu ya Keriothi, na juu ya Bozra, na juu ya miji yote ya nchi ya Moabu, iliyo mbali na iliyo karibu. Yeremia 48:24

and on Kerioth, and on Bozrah, and on all the cities of the land of Moab, far or near.

Pembe ya Moabu imekatika, na mkono wake umevunjika, asema Bwana. Mlevyeni; kwa maana alijitukuza juu ya Bwana Yeremia 48:25

The horn of Moab is cut off, and his arm is broken, says Yahweh.

na Moabu atagaa-gaa katika matapiko yake, naye atadhihakiwa. Kwa maana Israeli, je! Hakuwa dhihaka kwako? Yeremia 48:26

Make you him drunken; for he magnified himself against Yahweh: and Moab shall wallow in his vomit, and he also shall be in derision.

Alionekana kati ya wevi? Maana kila umtajapo watikisa kichwa chako. Yeremia 48:27

For wasn't Israel a derision to you? was he found among thieves? for as often as you speak of him, you wag the head.

Enyi mkaao Moabu, iacheni miji, Enendeni kukaa majabalini; Mkawe kama njiwa afanyaye kioto chake Katika ubavu wa mdomo wa shimo. Yeremia 48:28

You inhabitants of Moab, leave the cities, and dwell in the rock; and be like the dove that makes her nest over the mouth of the abyss.

Tumesikia habari za kiburi cha Moabu; Ya kuwa ana kiburi kingi; Jeuri yake, na kiburi chake, na majivuno yake, Na jinsi alivyotakabari moyoni mwake. Yeremia 48:29

We have heard of the pride of Moab, [that] he is very proud; his loftiness, and his pride, and his arrogance, and the haughtiness of his heart.

Najua ghadhabu yake, asema Bwana, ya kuwa si kitu; majisifu yake hayakutenda neno lo lote. Yeremia 48:30

I know his wrath, says Yahweh, that it is nothing; his boastings have worked nothing.

Kwa sababu hiyo nitampigia yowe Moabu, naam, nitapiga kelele kwa ajili ya Moabu yote; nitawaombolezea watu wa Kir-heresi. Yeremia 48:31

Therefore will I wail for Moab; yes, I will cry out for all Moab: for the men of Kir Heres shall they mourn.

Nitakulilia, Ee mzabibu wa Sibma, kwa vilio vipitavyo vilio vya Yazeri; matawi yako yalipita juu ya bahari, yalifika hata bahari ya Yazeri; atekaye nyara ameyaangukia matunda yako ya wakati wa jua, na mavuno yako ya zabibu. Yeremia 48:32

With more than the weeping of Jazer will I weep for you, vine of Sibmah: your branches passed over the sea, they reached even to the sea of Jazer: on your summer fruits and on your vintage the destroyer is fallen.

Furaha na shangwe zimeondoshwa, katika shamba lizaalo sana, na katika nchi ya Moabu; nami nimeikomesha divai katika mashinikizo; hapana mtu atakayekanyaga zabibu kwa shangwe; shangwe ile itakuwa si shangwe. Yeremia 48:33

Gladness and joy is taken away from the fruitful field and from the land of Moab; and I have caused wine to cease from the wine presses: none shall tread with shouting; the shouting shall be no shouting.

Toka kilio cha Heshboni mpaka Eleale, naam, mpaka Yahasa, wametoa sauti zao, toka Soari mpaka Horonaimu, hata Eglath-shelishia; maana maji ya Nimrimu nayo yatakuwa ukiwa. Yeremia 48:34

From the cry of Heshbon even to Elealeh, even to Jahaz have they uttered their voice, from Zoar even to Horonaim, to Eglath Shelishiyah: for the waters of Nimrim also shall become desolate.

Pamoja na hayo, asema Bwana, nitamkomesha katika Moabu mtu atoaye sadaka katika mahali pa juu, naye awafukiziaye uvumba miungu yake. Yeremia 48:35

Moreover I will cause to cease in Moab, says Yahweh, him who offers in the high place, and him who burns incense to his gods.

Kwa sababu hiyo moyo wangu watoa sauti kama filimbi kwa ajili ya Moabu, na kwa ajili ya watu wa Kir-heresi, moyo wangu watoa sauti kama filimbi; kwa kuwa wingi aliojipatia umepotea. Yeremia 48:36

Therefore my heart sounds for Moab like pipes, and my heart sounds like pipes for the men of Kir Heres: therefore the abundance that he has gotten is perished.

Maana kila kichwa kina upaa, na ndevu zote zimenyolewa; mikono yote ina alama za chale, na viuno vyote vimevikwa nguo za magunia. Yeremia 48:37

For every head is bald, and every beard clipped: on all the hands are cuttings, and on the loins sackcloth.

Juu ya dari zote za nyumba za Moabu, na katika njia kuu zake, pana maombolezo, kila mahali; kwa maana nimevunja Moabu kama chombo kisichopendeza, asema Bwana. Yeremia 48:38

On all the housetops of Moab and in the streets of it there is lamentation every where; for I have broken Moab like a vessel in which none delights, says Yahweh.

Jinsi alivyovunjika! Pigeni yowe! Jinsi Moabu alivyogeuza kisogo kwa haya! Hivyo ndivyo Moabu atakavyokuwa dhihaka, na sababu ya kuwashangaza watu wote wamzungukao. Yeremia 48:39

How is it broken down! [how] do they wail! how has Moab turned the back with shame! so shall Moab become a derision and a terror to all who are round about him.

Maana Bwana asema hivi, Tazama, ataruka kama tai, na kutandaza mabawa yake juu ya Moabu. Yeremia 48:40

For thus says Yahweh: Behold, he shall fly as an eagle, and shall spread out his wings against Moab.

Miji imetwaliwa, ngome zimeshambuliwa, na mioyo ya mashujaa wa Moabu siku hiyo itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wake. Yeremia 48:41

Kerioth is taken, and the strongholds are seized, and the heart of the mighty men of Moab at that day shall be as the heart of a woman in her pangs.

Na Moabu ataangamizwa, asiwe taifa tena, kwa sababu alijitukuza juu ya Bwana. Yeremia 48:42

Moab shall be destroyed from being a people, because he has magnified himself against Yahweh.

Hofu, na shimo, na mtego, zaja juu yako, Ee mwenyeji wa Moabu, asema Bwana. Yeremia 48:43

Fear, and the pit, and the snare, are on you, inhabitant of Moab, says Yahweh.

Aikimbiaye hofu ataanguka shimoni; na yeye atokaye shimoni atanaswa kwa mtego; maana nitaleta juu yake, yaani, juu ya Moabu, mwaka wa kujiliwa kwake, asema Bwana. Yeremia 48:44

He who flees from the fear shall fall into the pit; and he who gets up out of the pit shall be taken in the snare: for I will bring on him, even on Moab, the year of their visitation, says Yahweh.

Wamekimbia, wasio na nguvu Wanasimama chini ya kivuli cha Heshboni; Ila moto umetoka katika Heshboni, Na mwali wa moto toka kati ya Sihoni Nao umekula pembe ya Moabu, Na utosi wa kichwa wa watu wapigao kelele. Yeremia 48:45

Those who fled stand without strength under the shadow of Heshbon; for a fire is gone forth out of Heshbon, and a flame from the midst of Sihon, and has devoured the corner of Moab, and the crown of the head of the tumultuous ones.

Ole wako! Ee Moabu, Watu wa Kemoshi wamepotea; Maana wana wako wamechukuliwa mateka, Na binti zako wamekwenda utumwani. Yeremia 48:46

Woe to you, O Moab! the people of Chemosh is undone; for your sons are taken away captive, and your daughters into captivity.

Lakini nitawarudisha watu wa Moabu walio utumwani, siku za mwisho, asema Bwana. Hukumu ya Moabu imefikilia hapa. Yeremia 48:47

Yet will I bring back the captivity of Moab in the latter days, says Yahweh. Thus far is the judgment of Moab.