Yeremia 22 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yeremia 22 (Swahili) Jeremiah 22 (English)

Bwana akasema hivi, Shuka nyumbani kwa mfalme wa Yuda, ukaseme neno hili huko, Yeremia 22:1

Thus said Yahweh: Go down to the house of the king of Judah, and speak there this word,

ya kwamba, Sikia neno la Bwana, Ee mfalme wa Yuda; wewe uketiye katika kiti cha enzi cha Daudi, wewe, na watumishi wako, na watu wako wote waingiao kwa malango haya; Yeremia 22:2

Say, Hear the word of Yahweh, king of Judah, who sits on the throne of David, you, and your servants, and your people who enter in by these gates.

Bwana asema hivi, Fanyeni hukumu na haki, mkamtoe yeye aliyetekwa katika mikono ya mdhalimu; wala msiwatende mabaya mgeni, wala yatima, wala mjane, wala kuwadhulumu, wala msimwage damu ya mtu asiye na hatia katika mahali hapa. Yeremia 22:3

Thus says Yahweh: Execute you justice and righteousness, and deliver him who is robbed out of the hand of the oppressor: and do no wrong, do no violence, to the foreigner, the fatherless, nor the widow; neither shed innocent blood in this place.

Kwa maana mkifanya haya kweli kweli, ndipo watakapoingia kwa malango ya nyumba hii wafalme wenye kuketi katika kiti cha enzi cha Daudi, wanakwenda kwa magari, na wamepanda farasi yeye, na watumishi wake, na watu wake. Yeremia 22:4

For if you do this thing indeed, then shall there enter in by the gates of this house kings sitting on the throne of David, riding in chariots and on horses, he, and his servants, and his people.

Lakini kama hamtaki kusikia maneno haya, mimi naapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, ya kuwa nyumba hii itakuwa ukiwa. Yeremia 22:5

But if you will not hear these words, I swear by myself, says Yahweh, that this house shall become a desolation.

Kwa maana Bwana asema hivi, katika habari ya nyumba ya mfalme wa Yuda; Wewe u Gileadi kwangu, na kichwa cha Lebanoni; Ila hakika nitakufanya kuwa jangwa, na miji isiyokaliwa na watu. Yeremia 22:6

For thus says Yahweh concerning the house of the king of Judah: You are Gilead to me, [and] the head of Lebanon; [yet] surely I will make you a wilderness, [and] cities which are not inhabited.

Nami nitakufanyia tayari watu wenye kuharibu, kila mtu na silaha zake; Nao watakata mierezi miteule yako, na kuitupa motoni. Yeremia 22:7

I will prepare destroyers against you, everyone with his weapons; and they shall cut down your choice cedars, and cast them into the fire.

Na mataifa mengi watapita karibu na mji huu, nao watasema kila mtu na jirani yake, Nini maana yake Bwana kuutenda hivi mji huu mkubwa? Yeremia 22:8

Many nations shall pass by this city, and they shall say every man to his neighbor, Why has Yahweh done thus to this great city?

Ndipo watakapojibu, Ni kwa sababu waliliacha agano la Bwana, Mungu wao, wakaabudu miungu mingine, na kuitumikia. Yeremia 22:9

Then they shall answer, Because they forsook the covenant of Yahweh their God, and worshiped other gods, and served them.

Msimlilie aliyekufa, wala msimwombolezee, Bali mlilieni huyo aendaye zake mbali; Kwa maana yeye hatarudi tena, Wala hataiona nchi aliyozaliwa. Yeremia 22:10

Don't you weep for the dead, neither bemoan him; but weep sore for him who goes away; for he shall return no more, nor see his native country.

Maana Bwana asema hivi, katika habari za Shalumu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda; aliyemiliki badala ya Yosia, baba yake, yeye aliyetoka mahali hapa; Hatarudi huku tena; Yeremia 22:11

For thus says Yahweh touching Shallum the son of Josiah, king of Judah, who reigned instead of Josiah his father, [and] who went forth out of this place: He shall not return there any more.

bali katika mahali pale walipomchukua mateka ndipo atakapokufa, wala hataiona nchi hii tena kamwe. Yeremia 22:12

But in the place where they have led him captive, there shall he die, and he shall see this land no more.

Ole wake aijengaye nyumba yake kwa uovu! Na vyumba vyake kwa udhalimu! Atumiaye utumishi wa mwenzake bila ujira, Wala hampi mshahara wake; Yeremia 22:13

Woe to him who builds his house by unrighteousness, and his chambers by injustice; who uses his neighbor's service without wages, and doesn't give him his hire;

Asemaye, Nitajijengea nyumba pana na vyumba vipana; Naye hujikatia madirisha; Na kuta zake zimefunikwa kwa mierezi, Na kupakwa rangi nyekundu. Yeremia 22:14

who says, I will build me a wide house and spacious chambers, and cuts him out windows; and it is ceiling with cedar, and painted with vermilion.

Je! Utatawala kwa sababu unashindana na watu kwa mierezi? Baba yako, je! Hakula na kunywa, na kufanya hukumu na haki? Hapo ndipo alipofanikiwa. Yeremia 22:15

Shall you reign, because you strive to excel in cedar? Didn't your father eat and drink, and do justice and righteousness? then it was well with him.

Alihukumu maneno ya maskini na mhitaji; hapo ndipo alipofanikiwa. Je! Huku siko kunijua, asema Bwana? Yeremia 22:16

He judged the cause of the poor and needy; then it was well. Wasn't this to know me? says Yahweh.

Bali macho yako na moyo wako hauna utakalo ila kutamani, na kumwaga damu isiyo na hatia, na kudhulumu, na kutenda jeuri. Yeremia 22:17

But your eyes and your heart are not but for your covetousness, and for shedding innocent blood, and for oppression, and for violence, to do it.

Basi, Bwana asema hivi, katika habari ya Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda; Hawatamwombolezea, wakisema, Aa! Ndugu yangu; au, Aa! Dada yangu; wala hawatamlilia, wakisema, Aa! Bwana wangu; au, Aa! Utukufu wake. Yeremia 22:18

Therefore thus says Yahweh concerning Jehoiakim the son of Josiah, king of Judah: they shall not lament for him, [saying], Ah my brother! or, Ah sister! They shall not lament for him, [saying] Ah lord! or, Ah his glory!

Atazikwa maziko ya punda, akibururwa, na kutupwa nje ya malango ya Yerusalemu. Yeremia 22:19

He shall be buried with the burial of a donkey, drawn and cast forth beyond the gates of Jerusalem.

Haya panda Lebanoni, ukalie Upalize sauti yako katika Bashani; Ukalie kutoka Abarimu; Maana wapenzi wako wote wameangamia. Yeremia 22:20

Go up to Lebanon, and cry; and lift up your voice in Bashan, and cry from Abarim; for all your lovers are destroyed.

Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako tangu ujana wako, kutokuitii sauti yangu. Yeremia 22:21

I spoke to you in your prosperity; but you said, I will not hear. This has been your manner from your youth, that you didn't obey my voice.

Upepo utawalisha wachungaji wako wote, na wapenzi wako watakwenda kufungwa; hakika wakati huo utatahayarika, na kufadhaika kwa sababu ya uovu wako wote. Yeremia 22:22

The wind shall feed all your shepherds, and your lovers shall go into captivity: surely then shall you be ashamed and confounded for all your wickedness.

Wewe ukaaye Lebanoni, Ufanyaye kioto chako katika mierezi, Utakuwa na hali ya kuhurumiwa sana, Upatapo utungu kama wa mwanamke azaaye. Yeremia 22:23

Inhabitant of Lebanon, who makes your nest in the cedars, how greatly to be pitied shall you be when pangs come on you, the pain as of a woman in travail!

Kama niishivyo mimi, asema Bwana, hata Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, angekuwa pete yenye muhuri katika mkono wangu wa kuume, ningekung'oa wewe hapo; Yeremia 22:24

As I live, says Yahweh, though Coniah the son of Jehoiakim king of Judah were the signet on my right hand, yet would I pluck you there;

nami nitakutia katika mikono ya watu wale wakutafutao roho yako, na katika mikono yao unaowaogopa, naam, katika mikono ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, na katika mikono ya Wakaldayo. Yeremia 22:25

and I will give you into the hand of those who seek your life, and into the hand of them of whom you are afraid, even into the hand of Nebuchadrezzar king of Babylon, and into the hand of the Chaldeans.

Nami nitakutupa nje, wewe na mama yako aliyekuzaa, mwende nchi nyingine ambayo hamkuzaliwa huko, nanyi mtakufa huko. Yeremia 22:26

I will cast you out, and your mother who bore you, into another country, where you were not born; and there shall you die.

Lakini nchi ile ambayo wanatamani kuirudia, hawatairudia kamwe. Yeremia 22:27

But to the land whereunto their soul longs to return, there shall they not return.

Je! Mtu huyu, Konia, ni chombo kilichodharauliwa, na kuvunjika? Ni chombo kisichopendeza? Mbona wametupwa, yeye na wazao wake, na kutupwa katika nchi wasiyoijua? Yeremia 22:28

Is this man Coniah a despised broken vessel? is he a vessel in which none delights? why are they cast out, he and his seed, and are cast into the land which they don't know?

Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana. Yeremia 22:29

O earth, earth, earth, hear the word of Yahweh.

Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda. Yeremia 22:30

Thus says Yahweh, Write you this man childless, a man who shall not prosper in his days; for no more shall a man of his seed prosper, sitting on the throne of David, and ruling in Judah.