Yeremia 11 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yeremia 11 (Swahili) Jeremiah 11 (English)

Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema, Yeremia 11:1

The word that came to Jeremiah from Yahweh, saying,

Yasikieni maneno ya maagano haya; ukaseme na watu wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu; Yeremia 11:2

Hear you the words of this covenant, and speak to the men of Judah, and to the inhabitants of Jerusalem;

ukawaambie, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Na alaaniwe mtu asiyeyasikia maneno ya maagano haya, Yeremia 11:3

and say you to them, Thus says Yahweh, the God of Israel: Cursed be the man who doesn't hear the words of this covenant,

niliyowaamuru baba zenu, siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri, katika tanuru ya chuma, nikisema, Itiini sauti yangu, mkafanye sawasawa na yote niwaagizayo ninyi; ndivyo mtakavyokuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu; Yeremia 11:4

which I commanded your fathers in the day that I brought them forth out of the land of Egypt, out of the iron furnace, saying, Obey my voice, and do them, according to all which I command you: so shall you be my people, and I will be your God;

ili nipate kukitimiza kiapo nilichowaapia baba zenu, kuwapa nchi ijaayo maziwa na asali, kama ilivyo leo hivi. Ndipo nikajibu, nikasema, Amina, Ee Bwana. Yeremia 11:5

that I may establish the oath which I swore to your fathers, to give them a land flowing with milk and honey, as at this day. Then answered I, and said, Amen, Yahweh.

Naye Bwana akaniambia, Hubiri maneno haya yote katika miji ya Yuda, na katika njia kuu za Yerusalemu, ukisema, Yasikieni maneno ya maagano haya, mkayafanye. Yeremia 11:6

Yahweh said to me, Proclaim all these words in the cities of Judah, and in the streets of Jerusalem, saying, Hear you the words of this covenant, and do them.

Kwa maana naliwashuhudia sana baba zenu, siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri, hata leo, nikiamka mapema na kuwashuhudia, nikisema, Itiini sauti yangu. Yeremia 11:7

For I earnestly protested to your fathers in the day that I brought them up out of the land of Egypt, even to this day, rising early and protesting, saying, Obey my voice.

Lakini hawakutii, wala kutega masikio yao, bali walikwenda kila mtu katika ushupavu wa moyo wake mbaya; kwa hiyo nimeleta juu yao maneno yote ya maagano haya, niliyowaamuru wayafanye; lakini hawakuyafanya. Yeremia 11:8

Yet they didn't obey, nor turn their ear, but walked everyone in the stubbornness of their evil heart: therefore I brought on them all the words of this covenant, which I commanded them to do, but they didn't do them.

Naye Bwana akaniambia, Fitina imeonekana katika watu wa Yuda, na katika wenyeji wa Yerusalemu. Yeremia 11:9

Yahweh said to me, A conspiracy is found among the men of Judah, and among the inhabitants of Jerusalem.

Wameyarudia maovu ya baba zao, waliokataa kusikia maneno yangu; wamewafuata miungu mingine na kuwatumikia; nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, wameyavunja maagano yangu niliyoyafanya na baba zao. Yeremia 11:10

They are turned back to the iniquities of their forefathers, who refused to hear my words; and they are gone after other gods to serve them: the house of Israel and the house of Judah have broken my covenant which I made with their fathers.

Basi, Bwana asema hivi, Tazama, nitaleta mabaya juu yao, ambayo hawataweza kuyakimbia; nao watanililia, walakini sitawasikiliza. Yeremia 11:11

Therefore thus says Yahweh, Behold, I will bring evil on them, which they shall not be able to escape; and they shall cry to me, but I will not listen to them.

Ndipo miji ya Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu, watakwenda na kuwalilia miungu wawafukiziao uvumba; lakini hawatawaokoa hata kidogo wakati wa taabu yao. Yeremia 11:12

Then shall the cities of Judah and the inhabitants of Jerusalem go and cry to the gods to which they offer incense: but they will not save them at all in the time of their trouble.

Maana hesabu ya miungu yako, Ee Yuda, ni sawasawa na hesabu ya miji yako; na kama ilivyo hesabu ya njia za Yerusalemu, ndivyo mlivyosimamisha madhabahu za kitu kile cha aibu, madhabahu za kumfukizia Baali uvumba. Yeremia 11:13

For according to the number of your cities are your gods, Judah; and according to the number of the streets of Jerusalem have you set up altars to the shameful thing, even altars to burn incense to Baal.

Basi, usiwaombee watu hawa, wala usipaze sauti yako, wala kuwaombea dua watu hawa; maana sitawasikia wakati watakaponililia kwa ajili ya taabu yao. Yeremia 11:14

Therefore don't you pray for this people, neither lift up cry nor prayer for them; for I will not hear them in the time that they cry to me because of their trouble.

Mpenzi wangu afanya nini nyumbani mwangu, ikiwa amefanya uasherati? Je! Nadhiri zako na nyama takatifu zitakuondolea hatia? Ufanyapo maovu, ndipo uonapo furaha. Yeremia 11:15

What has my beloved to do in my house, seeing she has worked lewdness [with] many, and the holy flesh is passed from you? when you do evil, then you rejoice.

Bwana alikuita jina lako, Mzeituni wenye majani mabichi, mzuri, wenye matunda mema; kwa kelele za mshindo mkuu amewasha moto juu yake, na matawi yake yamevunjika. Yeremia 11:16

Yahweh called your name, A green olive tree, beautiful with goodly fruit: with the noise of a great tumult he has kindled fire on it, and the branches of it are broken.

Kwa maana Bwana wa majeshi, aliyekupanda, ametamka mabaya juu yako, kwa sababu ya maovu ya nyumba ya Israeli, na ya nyumba ya Yuda, waliyoyatenda juu ya nafsi zao wenyewe kwa kunikasirisha, wakimfukizia Baali uvumba. Yeremia 11:17

For Yahweh of Hosts, who planted you, has pronounced evil against you, because of the evil of the house of Israel and of the house of Judah, which they have worked for themselves in provoking me to anger by offering incense to Baal.

Tena Bwana akanijulisha haya, nami nikayajua; ndipo uliponionyesha matendo yao. Yeremia 11:18

Yahweh gave me knowledge of it, and I knew it: then you shown me their doings.

Lakini mimi nalikuwa kama mwana-kondoo mpole, achukuliwaye kwenda kuchinjwa; wala sikujua ya kuwa wamefanya mashauri kinyume changu, wakisema, Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali atoke katika nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena. Yeremia 11:19

But I was like a gentle lamb that is led to the slaughter; and I didn't know that they had devised devices against me, [saying], Let us destroy the tree with the fruit of it, and let us cut him off from the land of the living, that his name may be no more remembered.

Lakini, Ee Bwana wa majeshi, uhukumuye haki, ujaribuye viuno na moyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu. Yeremia 11:20

But, Yahweh of Hosts, who judge righteously, who try the heart and the mind, I shall see your vengeance on them; for to you have I revealed my cause.

Basi, kwa hiyo, Bwana asema hivi, juu ya watu wa Anathothi, watakao uhai wako, wakisema, Hutafanya unabii kwa jina la Bwana, usije ukafa kwa mkono wetu. Yeremia 11:21

Therefore thus says Yahweh concerning the men of Anathoth, who seek your life, saying, You shall not prophesy in the name of Yahweh, that you not die by our hand;

Kwa sababu hiyo Bwana wa majeshi asema hivi, Tazama, nitawaadhibu watu hawa; vijana watakufa kwa upanga; wana wao na binti zao watakufa kwa njaa; Yeremia 11:22

therefore thus says Yahweh of hosts, Behold, I will punish them: the young men shall die by the sword; their sons and their daughters shall die by famine;

wala hapatakuwa na mtu atakayesalia kwao; maana nitaleta mabaya juu ya watu wa Anathothi, mwaka wa kujiliwa kwao. Yeremia 11:23

and there shall be no remnant to them: for I will bring evil on the men of Anathoth, even the year of their visitation.