Yeremia 1 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yeremia 1 (Swahili) Jeremiah 1 (English)

Maneno ya Yeremia, mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani waliokuwa katika Anathothi, katika nchi ya Benyamini; Yeremia 1:1

The words of Jeremiah the son of Hilkiah, of the priests who were in Anathoth in the land of Benjamin:

ambaye neno la Bwana lilimjia katika siku za Yosia, mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na tatu wa kumiliki kwake. Yeremia 1:2

to whom the word of Yahweh came in the days of Josiah the son of Amon, king of Judah, in the thirteenth year of his reign.

Tena lilikuja siku za Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, hata mwisho wa mwaka wa kumi na mmoja wa Sedekia, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda; hata wakati ulipochukuliwa mateka Yerusalemu, katika mwezi wa tano. Yeremia 1:3

It came also in the days of Jehoiakim the son of Josiah, king of Judah, to the end of the eleventh year of Zedekiah, the son of Josiah, king of Judah, to the carrying away of Jerusalem captive in the fifth month.

Neno la Bwana lilinijia, kusema, Yeremia 1:4

Now the word of Yahweh came to me, saying,

Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. Yeremia 1:5

Before I formed you in the belly I knew you, and before you came forth out of the womb I sanctified you; I have appointed you a prophet to the nations.

Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto. Yeremia 1:6

Then said I, Ah, Lord Yahweh! behold, I don't know how to speak; for I am a child.

Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru. Yeremia 1:7

But Yahweh said to me, Don't say, I am a child; for to whoever I shall send you, you shall go, and whatever I shall command you, you shall speak.

Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana. Yeremia 1:8

Don't be afraid because of them; for I am with you to deliver you, says Yahweh.

Ndipo Bwana akaunyosha mkono wake, akanigusa kinywa changu; Bwana akaniambia, Tazama, nimetia maneno yangu kinywani mwako; Yeremia 1:9

Then Yahweh put forth his hand, and touched my mouth; and Yahweh said to me, Behold, I have put my words in your mouth:

angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung'oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda. Yeremia 1:10

behold, I have this day set you over the nations and over the kingdoms, to pluck up and to break down and to destroy and to overthrow, to build and to plant.

Tena neno la Bwana likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema, Naona ufito wa mlozi. Yeremia 1:11

Moreover the word of Yahweh came to me, saying, Jeremiah, what see you? I said, I see a rod of an almond tree.

Ndipo Bwana akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize. Yeremia 1:12

Then said Yahweh to me, You have well seen: for I watch over my word to perform it.

Neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema, Waona nini? Nikasema, Naona sufuria lenye maji yatokotayo, na mdomo wake unaelekea toka upande wa kaskazini. Yeremia 1:13

The word of Yahweh came to me the second time, saying, What see you? I said, I see a boiling caldron; and the face of it is from the north.

Ndipo Bwana akaniambia, Toka kaskazini mabaya yatatokea, na kuwapata watu wote wakaao katika nchi hii. Yeremia 1:14

Then Yahweh said to me, Out of the north evil shall break forth on all the inhabitants of the land.

Kwa kuwa, tazama, nitaziita jamaa zote za falme za kaskazini, asema Bwana; nao watakuja, na kuweka kila mtu kiti chake cha enzi mbele ya mahali pa kuingilia malango ya Yerusalemu, na kuzielekea kuta zake pande zote, na kuielekea miji yote ya Yuda. Yeremia 1:15

For, behold, I will call all the families of the kingdoms of the north, says Yahweh; and they shall come, and they shall set everyone his throne at the entrance of the gates of Jerusalem, and against all the walls of it round about, and against all the cities of Judah.

Nami nitatamka hukumu zangu juu yao kwa habari ya uovu wao wote; kwa kuwa wameniacha mimi, wakaifukizia uvumba miungu mingine, wakaziabudu kazi za mikono yao wenyewe. Yeremia 1:16

I will utter my judgments against them touching all their wickedness, in that they have forsaken me, and have burned incense to other gods, and worshiped the works of their own hands.

Haya basi, wewe jifunge viuno, ukaondoke ukawaambie maneno yote niliyokuamuru; usifadhaike kwa ajili yao, nisije nikakufadhaisha wewe mbele yao. Yeremia 1:17

You therefore gird up your loins, and arise, and speak to them all that I command you: don't be dismayed at them, lest I dismay you before them.

Maana, tazama, nimekufanya leo kuwa mji wenye boma, na nguzo ya chuma, na kuta za shaba, juu ya nchi yote; juu ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wa nchi hii. Yeremia 1:18

For, behold, I have made you this day a fortified city, and an iron pillar, and brazen walls, against the whole land, against the kings of Judah, against the princes of it, against the priests of it, and against the people of the land.

Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe. Yeremia 1:19

They shall fight against you; but they shall not prevail against you: for I am with you, says Yahweh, to deliver you.