Yeremia 43 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yeremia 43 (Swahili) Jeremiah 43 (English)

Ikawa Yeremia alipokwisha kuwaambia watu wote maneno yote ya Bwana, Mungu wao, ambayo Bwana, Mungu wao, amemtuma kwao, yaani, maneno hayo yote, Yeremia 43:1

It happened that, when Jeremiah had made an end of speaking to all the people all the words of Yahweh their God, with which Yahweh their God had sent him to them, even all these words,

ndipo Azaria, mwana wa Hoshaya, na Yohana mwana wa Karea, na watu wote wenye kiburi wakanena, wakimwambia Yeremia, Unasema uongo; Bwana, Mungu wetu, hakukutuma useme, Msiende Misri kukaa huko; Yeremia 43:2

then spoke Azariah the son of Hoshaiah, and Johanan the son of Kareah, and all the proud men, saying to Jeremiah, You speak falsely: Yahweh our God has not sent you to say, You shall not go into Egypt to sojourn there;

bali Baruku, mwana wa Neria, akushawishi kinyume chetu, ili kututia katika mikono ya Wakaldayo, ili watuue, na kutuchukua mateka mpaka Babeli. Yeremia 43:3

but Baruch the son of Neriah sets you on against us, to deliver us into the hand of the Chaldeans, that they may put us to death, and carry us away captive to Babylon.

Basi Yohana, mwana wa Karea, na wakuu wote wa majeshi, na watu wote hawakuitii sauti ya Bwana, kwamba wakae katika nchi ya Yuda. Yeremia 43:4

So Johanan the son of Kareah, and all the captains of the forces, and all the people, didn't obey the voice of Yahweh, to dwell in the land of Judah.

Lakini Yohana, mwana wa Karea, na wakuu wote wa majeshi, wakawatwaa wote waliosalia wa Yuda, waliokuwa wamerudi kutoka taifa zote walikofukuzwa, wakae katika Yuda; Yeremia 43:5

But Johanan the son of Kareah, and all the captains of the forces, took all the remnant of Judah, who were returned from all the nations where they had been driven, to sojourn in the land of Judah;

wanaume, na wanawake, na watoto, na binti za mfalme, na kila mtu ambaye Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, amemwacha pamoja na Gedalia, mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, pia na Yeremia, nabii, na Baruku, mwana wa Neria; Yeremia 43:6

the men, and the women, and the children, and the king's daughters, and every person who Nebuzaradan the captain of the guard had left with Gedaliah the son of Ahikam, the son of Shaphan; and Jeremiah the prophet, and Baruch the son of Neriah;

wakaingia nchi ya Misri; maana hawakuitii sauti ya Bwana; wakafika hata Tahpanesi. Yeremia 43:7

and they came into the land of Egypt; for they didn't obey the voice of Yahweh: and they came to Tahpanhes.

Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia huko Tahpenesi, kusema, Yeremia 43:8

Then came the word of Yahweh to Jeremiah in Tahpanhes, saying,

Twaa mawe makubwa mikononi mwako, ukayafiche ndani ya chokaa ya kazi ya matofali, penye maingilio ya nyumba ya Farao huko Tahpanesi, machoni pa watu wa Yuda; Yeremia 43:9

Take great stones in your hand, and hide them in mortar in the brick work, which is at the entry of Pharaoh's house in Tahpanhes, in the sight of the men of Judah;

ukawaambie, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitatuma na kumtwaa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, mtumishi wangu, nami nitaweka kiti chake cha enzi juu ya mawe haya niliyoyaficha; naye atatandaza hema yake ya fahari juu yake. Yeremia 43:10

and tell them, Thus says Yahweh of Hosts, the God of Israel: Behold, I will send and take Nebuchadrezzar the king of Babylon, my servant, and will set his throne on these stones that I have hidden; and he shall spread his royal pavilion over them.

Naye atakuja, na kuipiga nchi ya Misri; watu walioandikiwa kufa watakufa, nao walioandikiwa kuwa mateka watakuwa mateka, nao walioandikiwa kupigwa kwa upanga watapigwa kwa upanga. Yeremia 43:11

He shall come, and shall strike the land of Egypt; such as are for death [shall be given] to death, and such as are for captivity to captivity, and such as are for the sword to the sword.

Nami nitawasha moto katika nyumba za miungu ya Misri, na kuziteketeza, na kuwachukua mateka; naye atajipamba kwa nchi ya Misri, kama vile mchungaji avaavyo nguo zake; naye atatoka huko na amani. Yeremia 43:12

I will kindle a fire in the houses of the gods of Egypt; and he shall burn them, and carry them away captive: and he shall array himself with the land of Egypt, as a shepherd puts on his garment; and he shall go forth from there in peace.

Naye atazivunja nguzo za Bethshemeshi, iliyoko huko katika nchi ya Misri, na nyumba za miungu ya Misri ataziteketeza. Yeremia 43:13

He shall also break the pillars of Beth-shemesh, that is in the land of Egypt; and the houses of the gods of Egypt shall he burn with fire.