Yeremia 23 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yeremia 23 (Swahili) Jeremiah 23 (English)

Ole wao wachungaji, wanaoharibu kondoo za malisho yangu na kuwatawanya! Asema Bwana. Yeremia 23:1

Woe to the shepherds who destroy and scatter the sheep of my pasture! says Yahweh.

Kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, juu ya wachungaji wanaowalisha watu wangu, Mmetawanya kundi langu, na kuwafukuza, wala hamkwenda kuwatazama; angalieni, nitawapatiliza uovu wa matendo yenu, asema Bwana. Yeremia 23:2

Therefore thus says Yahweh, the God of Israel, against the shepherds who feed my people: You have scattered my flock, and driven them away, and have not visited them; behold, I will visit on you the evil of your doings, says Yahweh.

Nami nitakusanya mabaki ya kundi langu, katika nchi zile zote nilizowafukuza, nami nitawaleta tena mazizini mwao; nao watazaa na kuongezeka. Yeremia 23:3

I will gather the remnant of my flock out of all the countries where I have driven them, and will bring them again to their folds; and they shall be fruitful and multiply.

Nami nitaweka juu yao wachungaji watakaowalisha; wala hawataona hofu tena, wala kufadhaika, wala hatapotea hata mmoja wao, asema Bwana. Yeremia 23:4

I will set up shepherds over them, who shall feed them; and they shall fear no more, nor be dismayed, neither shall any be lacking, says Yahweh.

Tazama siku zinakuja, asema Bwana, nitakapomchipushia Daudi Chipukizi la haki; naye atamiliki mfalme, atatenda kwa hekima, naye atafanya hukumu na haki katika nchi. Yeremia 23:5

Behold, the days come, says Yahweh, that I will raise to David a righteous Branch, and he shall reign as king and deal wisely, and shall execute justice and righteousness in the land.

Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli atakaa salama, na jina lake atakaloitwa ni hili, Bwana ni haki yetu. Yeremia 23:6

In his days Judah shall be saved, and Israel shall dwell safely; and this is his name by which he shall be called: Yahweh our righteousness.

Kwa hiyo, angalia, siku zinakuja, asema Bwana, ambapo hawatasema tena, Aishivyo Bwana, aliyewatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri; Yeremia 23:7

Therefore, behold, the days come, says Yahweh, that they shall no more say, As Yahweh lives, who brought up the children of Israel out of the land of Egypt;

lakini, Aishivyo Bwana, aliyewapandisha na kuwaongoza wazao wa nyumba ya Israeli kutoka nchi ya kaskazini, na kutoka nchi zote nilikowafukuza; nao watakaa katika nchi yao wenyewe. Yeremia 23:8

but, As Yahweh lives, who brought up and who led the seed of the house of Israel out of the north country, and from all the countries where I had driven them. They shall dwell in their own land.

Katika habari za manabii. Moyo wangu ndani yangu umevunjika, Mifupa yangu yote inatikisika. Nimekuwa kama mtu aliye mlevi, Na kama mtu aliyeshindwa na divai;kwa ajili ya Bwana,na kwa ajili ya maneno yake matakatifu. Yeremia 23:9

Concerning the prophets. My heart within me is broken, all my bones shake; I am like a drunken man, and like a man whom wine has overcome, because of Yahweh, and because of his holy words.

Maana nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya kuapa nchi inaomboleza; malisho ya nyikani yamekauka; mwenendo wao ni mbaya, na nguvu zao si za haki. Yeremia 23:10

For the land is full of adulterers; for because of swearing the land mourns; the pastures of the wilderness are dried up. Their course is evil, and their might is not right;

Maana nabii, na kuhani, wote wawili wanakufuru; naam, katika nyumba yangu nimeuona uovu wao, asema Bwana. Yeremia 23:11

for both prophet and priest are profane; yes, in my house have I found their wickedness, says Yahweh.

Kwa ajili ya hayo njia yao itakuwa kwao kama mahali pa kuteleza gizani; watatelemshwa na kuanguka hapo; kwa maana nitaleta uovu juu yao, naam, mwaka wa kujiliwa kwao, asema Bwana. Yeremia 23:12

Therefore their way shall be to them as slippery places in the darkness: they shall be driven on, and fall therein; for I will bring evil on them, even the year of their visitation, says Yahweh.

Nami nimeona upumbavu katika manabii wa Samaria; walitabiri kwa Baali, wakawakosesha watu wangu Israeli. Yeremia 23:13

I have seen folly in the prophets of Samaria; they prophesied by Baal, and caused my people Israel to err.

Katika manabii wa Yerusalemu nimeona neno linalochukiza sana; hufanya zinaa; huenenda katika maneno ya uongo, hutia nguvu mikono ya watendao maovu, hata ikawa hapana mtu arejeaye na kuuacha uovu wake; wote pia wamekuwa kama Sodoma kwangu, na wenyeji wake kama Gomora. Yeremia 23:14

In the prophets of Jerusalem also I have seen a horrible thing: they commit adultery, and walk in lies; and they strengthen the hands of evil-doers, so that none does return from his wickedness: they are all of them become to me as Sodom, and the inhabitants of it as Gomorrah.

Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, Tazama, nitawalisha pakanga, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote. Yeremia 23:15

Therefore thus says Yahweh of Hosts concerning the prophets: Behold, I will feed them with wormwood, and make them drink the water of gall; for from the prophets of Jerusalem is ungodliness gone forth into all the land.

Bwana wa majeshi asema hivi, Msisikilize maneno ya manabii wakiwatabiria; huwafundisha ubatili; hunena maono ya mioyo yao wenyewe; hayakutoka katika kinywa cha Bwana. Yeremia 23:16

Thus says Yahweh of Hosts, Don't listen to the words of the prophets who prophesy to you: they teach you vanity; they speak a vision of their own heart, and not out of the mouth of Yahweh.

Daima huwaambia wao wanaonidharau, Bwana amesema, Mtakuwa na amani; nao humwambia kila mtu aendaye kwa ukaidi wa moyo wake, Hamtapatwa na ubaya wo wote. Yeremia 23:17

They say continually to those who despise me, Yahweh has said, You shall have peace; and to everyone who walks in the stubbornness of his own heart they say, No evil shall come on you.

Maana, ni nani aliyesimama katika baraza la Bwana, hata akalifahamu neno lake na kulisikia? Ni nani aliyelitia moyoni neno langu, na kulisikia? Yeremia 23:18

For who has stood in the council of Yahweh, that he should perceive and hear his word? who has marked my word, and heard it?

Tazama, tufani ya Bwana, yaani, ghadhabu yake, imetokea; ni dhoruba ya kisulisuli; itapasuka, na kuwaangukia waovu vichwani. Yeremia 23:19

Behold, the tempest of Yahweh, [even his] wrath, is gone forth, yes, a whirling tempest: it shall burst on the head of the wicked.

Hasira ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtalifahamu neno hili kabisa. Yeremia 23:20

The anger of Yahweh shall not return, until he has executed, and until he have performed the intents of his heart: in the latter days you shall understand it perfectly.

Mimi sikuwatuma manabii hao, lakini walikwenda mbio; sikusema nao, lakini walitabiri. Yeremia 23:21

I sent not these prophets, yet they ran: I didn't speak to them, yet they prophesied.

Lakini kama wangalisimama katika baraza yangu, ndipo wangaliwasikizisha watu wangu maneno yangu, na kuwageuza waziache njia zao mbaya, na uovu wa matendo yao. Yeremia 23:22

But if they had stood in my council, then had they caused my people to hear my words, and had turned them from their evil way, and from the evil of their doings.

Mimi ni Mungu aliye karibu, asema Bwana, mimi si Mungu aliye mbali. Yeremia 23:23

Am I a God at hand, says Yahweh, and not a God afar off?

Je, mtu ye yote aweza kujificha mahali pa siri, nisimwone? Asema Bwana. Je! Mbingu na nchi hazikujawa nami? Asema Bwana. Yeremia 23:24

Can any hide himself in secret places so that I shall not see him? says Yahweh. Don't I fill heaven and earth? says Yahweh.

Nimesikia waliyoyasema manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema, Nimeota ndoto; nimeota ndoto. Yeremia 23:25

I have heard what the prophets have said, who prophesy lies in my name, saying, I have dreamed, I have dreamed.

Je! Mambo hayo yatakuwa katika mioyo ya manabii wanaotabiri uongo hata lini, manabii hao wenye udanganyifu katika mioyo yao wenyewe? Yeremia 23:26

How long shall this be in the heart of the prophets who prophesy lies, even the prophets of the deceit of their own heart?

Wanaodhania ya kuwa watawasahaulisha watu wangu jina langu kwa ndoto zao, wanazomhadithia kila mtu jirani yake, kama vile baba zao walivyolisahau jina langu, kwa ajili ya Baali. Yeremia 23:27

who think to cause my people to forget my name by their dreams which they tell every man to his neighbor, as their fathers forgot my name for Baal.

Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye aliye na neno langu, na aseme neno langu kwa uaminifu. Makapi ni kitu gani kuliko ngano? Asema Bwana. Yeremia 23:28

The prophet who has a dream, let him tell a dream; and he who has my word, let him speak my word faithfully. What is the straw to the wheat? says Yahweh.

Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande? Yeremia 23:29

Isn't my word like fire? says Yahweh; and like a hammer that breaks the rock in pieces?

Basi kwa sababu hiyo mimi ni juu ya manabii hao, asema Bwana, wanaompokonya kila mtu jirani yake maneno yangu. Yeremia 23:30

Therefore, behold, I am against the prophets, says Yahweh, who steal my words everyone from his neighbor.

Tazama, mimi ni juu ya manabii, asema Bwana, wanaotumia ndimi zao na kusema, Yeye asema, Yeremia 23:31

Behold, I am against the prophets, says Yahweh, who use their tongues, and say, He says.

Tazama, mimi ni juu ya hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema Bwana, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi sikuwatuma, wala sikuwapa amri; wala hawatawafaidia watu hawa hata kidogo, asema Bwana. Yeremia 23:32

Behold, I am against those who prophesy lying dreams, says Yahweh, and do tell them, and cause my people to err by their lies, and by their vain boasting: yet I didn't send them, nor commanded them; neither do they profit this people at all, says Yahweh.

Na watu hawa, au nabii au kuhani, atakapokuuliza, akisema, Mzigo wa Bwana ni nini? Ndipo utawaambia, Mzigo gani? Bwana asema, Nitawatupilia mbali. Yeremia 23:33

When this people, or the prophet, or a priest, shall ask you, saying, What is the burden of Yahweh? then shall you tell them, What burden! I will cast you off, says Yahweh.

Na katika habari ya nabii, na kuhani, na watu, watakaosema, Mzigo wa Bwana, mimi nitamwadhibu mtu yule, na nyumba yake. Yeremia 23:34

As for the prophet, and the priest, and the people, who shall say, The burden of Yahweh, I will even punish that man and his house.

Mtasema hivi kila mtu na jirani yake, na kila mtu na ndugu yake, Bwana amejibu mtu? Na, Bwana amesemaje? Yeremia 23:35

Thus shall you say everyone to his neighbor, and everyone to his brother, What has Yahweh answered? and, What has Yahweh spoken?

Na mzigo wa Bwana hamtautaja tena; maana neno la kila mtu ndilo litakalokuwa mzigo wake; maana ninyi mmeyapotosha maneno ya Mungu aliye hai, ya Bwana wa majeshi, Mungu wetu. Yeremia 23:36

The burden of Yahweh shall you mention no more: for every man's own word shall be his burden; for you have perverted the words of the living God, of Yahweh of Hosts our God.

Nawe utamwambia nabii hivi, Bwana amekujibu nini? Na, Bwana amesemaje? Yeremia 23:37

Thus shall you say to the prophet, What has Yahweh answered you? and, What has Yahweh spoken?

Lakini mkisema, Mzigo wa Bwana, basi, Bwana asema hivi, Kwa sababu mwasema neno hili, ; nami nimemtuma mtu kwenu kusema, Msiseme, ; Yeremia 23:38

But if you say, The burden of Yahweh; therefore thus says Yahweh: Because you say this word, The burden of Yahweh, and I have sent to you, saying, You shall not say, The burden of Yahweh;

basi, kwa hiyo angalieni, nitawasahau ninyi kabisa, nami nitawatupilia mbali, pamoja na mji huu niliowapa ninyi na baba zenu, mtoke mbele za uso wangu; Yeremia 23:39

therefore, behold, I will utterly forget you, and I will cast you off, and the city that I gave to you and to your fathers, away from my presence:

nami nitaleta juu yenu aibu ya milele, na fedheha ya daima, ambayo haitasahauliwa. Yeremia 23:40

and I will bring an everlasting reproach on you, and a perpetual shame, which shall not be forgotten.