Yeremia 30 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yeremia 30 (Swahili) Jeremiah 30 (English)

Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema, Yeremia 30:1

The word that came to Jeremiah from Yahweh, saying,

Bwana Mungu wa Israeli, asema hivi, ya kwamba, Uyaandike kitabuni maneno hayo yote niliyokuambia. Yeremia 30:2

Thus speaks Yahweh, the God of Israel, saying, Write you all the words that I have spoken to you in a book.

Kwa maana, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapowarejeza watu wangu wa Israeli na Yuda waliofungwa, asema Bwana; nami nitawarudisha hata nchi niliyowapa baba zao, nao wataimiliki. Yeremia 30:3

For, behold, the days come, says Yahweh, that I will turn again the captivity of my people Israel and Judah, says Yahweh; and I will cause them to return to the land that I gave to their fathers, and they shall possess it.

Na haya ndiyo maneno aliyosema Bwana, katika habari za Israeli, na katika habari za Yuda. Yeremia 30:4

These are the words that Yahweh spoke concerning Israel and concerning Judah.

Maana Bwana asema hivi, Tumesikia sauti ya tetemeko, na ya hofu, wala si ya amani. Yeremia 30:5

For thus says Yahweh: We have heard a voice of trembling, of fear, and not of peace.

Ulizeni sasa, mkaone kwamba mwanamume aona utungu wa uzazi; mbona, basi, ninaona kila mtu anaweka mikono yake viunoni, kama mwanamke aliye na utungu, na nyuso zote zimegeuka rangi. Yeremia 30:6

Ask now, and see whether a man does travail with child: why do I see every man with his hands on his loins, as a woman in travail, and all faces are turned into paleness?

Ole! Maana siku ile ni kuu, hata hapana inayofanana nayo, maana ni wakati wa taabu yake Yakobo; lakini ataokolewa nayo. Yeremia 30:7

Alas! for that day is great, so that none is like it: it is even the time of Jacob's trouble; but he shall be saved out of it.

Na itakuwa katika siku ile, asema Bwana wa majeshi, nitaivunja nira yake itoke shingoni mwako, nami nitavipasua vifungo vyako; wala wageni hawatamtumikisha tena; Yeremia 30:8

It shall come to pass in that day, says Yahweh of Hosts, that I will break his yoke from off your neck, and will burst your bonds; and strangers shall no more make him their bondservant;

bali watamtumikia Bwana, Mungu wao, na Daudi, mfalme wao, nitakayemwinua kwa ajili yao. Yeremia 30:9

but they shall serve Yahweh their God, and David their king, whom I will raise up to them.

Kwa sababu hiyo usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu, asema Bwana; wala usifadhaike, Ee Israeli; kwa maana, tazama, nitakuokoa toka mbali, na wazao wako toka nchi ya uhamisho wao; na Yakobo atarudi, naye atatulia na kustarehe, wala hapana mtu atakayemtia hofu. Yeremia 30:10

Therefore don't you be afraid, O Jacob my servant, says Yahweh; neither be dismayed, Israel: for, behold, I will save you from afar, and your seed from the land of their captivity; and Jacob shall return, and shall be quiet and at ease, and none shall make him afraid.

Maana mimi ni pamoja nawe, asema Bwana, nikuokoe; maana nitawakomesha kabisa mataifa yote huko nilikokutawanya, bali sitakukomesha wewe kabisa; lakini nitakurudi kwa hukumu, wala sitakuacha bila adhabu. Yeremia 30:11

For I am with you, says Yahweh, to save you: for I will make a full end of all the nations where I have scattered you, but I will not make a full end of you; but I will correct you in measure, and will in no way leave you unpunished.

Maana Bwana asema hivi, Maumivu yako hayaponyekani, na jeraha yako ni kubwa. Yeremia 30:12

For thus says Yahweh, Your hurt is incurable, and your wound grievous.

Hapana mtu wa kukutetea; kwa jeraha yako huna dawa ziponyazo. Yeremia 30:13

There is none to plead your cause, that you may be bound up: you have no healing medicines.

Wote wakupendao wamekusahau; hawakutafuti; maana nimekujeruhi kwa jeraha ya adui, kwa adhabu ya mtu mkatili; kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zilikuwa zimeongezeka. Yeremia 30:14

All your lovers have forgotten you; they don't seek you: for I have wounded you with the wound of an enemy, with the chastisement of a cruel one, for the greatness of your iniquity, because your sins were increased.

Mbona unalilia maumivu yako? Hayaponyeki maumivu yako; kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zimeongezeka, nimekutenda haya. Yeremia 30:15

Why cry you for your hurt? your pain is incurable: for the greatness of your iniquity, because your sins were increased, I have done these things to you.

Basi, watu wote wakulao wataliwa; na adui zako wote watakwenda kufungwa; kila mmoja wao; na hao waliokuteka nyara watatekwa; na wote waliokuwinda nitawafanya kuwa mawindo. Yeremia 30:16

Therefore all those who devour you shall be devoured; and all your adversaries, everyone of them, shall go into captivity; and those who despoil you shall be a spoil, and all who prey on you will I give for a prey.

Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye. Yeremia 30:17

For I will restore health to you, and I will heal you of your wounds, says Yahweh; because they have called you an outcast, [saying], It is Zion, whom no man seeks after.

Bwana asema hivi, Tazama, nitarudisha tena hema za Yakobo zilizohamishwa, na kuyahurumia makao yake; nao mji huo utajengwa juu ya magofu yake wenyewe, nalo jumba litakaliwa, kama ilivyokuwa desturi yake. Yeremia 30:18

Thus says Yahweh: Behold, I will turn again the captivity of Jacob's tents, and have compassion on his dwelling-places; and the city shall be built on its own hill, and the palace shall be inhabited after its own manner.

Tena kwao itasikiwa shukrani, na sauti yao wachangamkao; nami nitawazidisha, wala hawatakuwa wachache; tena nitawatukuza, wala hawatakuwa wanyonge. Yeremia 30:19

Out of them shall proceed thanksgiving and the voice of those who make merry: and I will multiply them, and they shall not be few; I will also glorify them, and they shall not be small.

Watoto wao nao watakuwa kama zamani, na kusanyiko lao litathibitika mbele zangu, nami nitawaadhibu wote wawaoneao. Yeremia 30:20

Their children also shall be as before, and their congregation shall be established before me; and I will punish all who oppress them.

Na mkuu wao atakuwa mtu wa kwao wenyewe, naye mwenye kuwatawala atakuwa mtu wa jamaa yao; nami nitamkaribisha, naye atanikaribia; maana ni nani aliye na moyo wa kuthubutu kunikaribia? Asema Bwana. Yeremia 30:21

Their prince shall be of themselves, and their ruler shall proceed from the midst of them; and I will cause him to draw near, and he shall approach to me: for who is he who has had boldness to approach to me? says Yahweh.

Nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Yeremia 30:22

You shall be my people, and I will be your God.

Tazama, tufani ya Bwana, yaani, ghadhabu yake, imetokea tufani ya kudumu; itawaangukia waovu vichwani. Yeremia 30:23

Behold, the tempest of Yahweh, [even his] wrath, is gone forth, a sweeping tempest: it shall burst on the head of the wicked.

Hasira kali ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha kutenda, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtayafahamu haya. Yeremia 30:24

The fierce anger of Yahweh shall not return, until he has executed, and until he have performed the intents of his heart: in the latter days you shall understand it.