Yeremia 32 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yeremia 32 (Swahili) Jeremiah 32 (English)

Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, katika mwaka wa kumi wa Sedekia, mfalme wa Yuda, nao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa Nebukadreza. Yeremia 32:1

The word that came to Jeremiah from Yahweh in the tenth year of Zedekiah king of Judah, which was the eighteenth year of Nebuchadrezzar.

Basi, wakati huo jeshi la mfalme wa Babeli liliuzunguka Yerusalemu; na Yeremia, nabii, alikuwa amefungwa ndani ya uwanda wa walinzi, uliokuwa katika nyumba ya mfalme wa Yuda. Yeremia 32:2

Now at that time the king of Babylon's army was besieging Jerusalem; and Jeremiah the prophet was shut up in the court of the guard, which was in the king of Judah's house.

Kwa maana Sedekia, mfalme wa Yuda, alikuwa amemfunga, akisema, Kwa nini unatabiri, na kusema, Bwana asema hivi, Angalia, nitatia mji huu katika mikono ya mfalme wa Babeli, naye atautwaa; Yeremia 32:3

For Zedekiah king of Judah had shut him up, saying, Why do you prophesy, and say, Thus says Yahweh, Behold, I will give this city into the hand of the king of Babylon, and he shall take it;

tena, Sedekia, mfalme wa Yuda, hatapona kutoka katika mikono ya Wakaldayo, lakini hakika yake atatiwa katika mikono ya mfalme wa Babeli, atanena naye mdomo kwa mdomo, na macho yake yatatazama macho yake; Yeremia 32:4

and Zedekiah king of Judah shall not escape out of the hand of the Chaldeans, but shall surely be delivered into the hand of the king of Babylon, and shall speak with him mouth to mouth, and his eyes shall see his eyes;

naye atamchukua Sedekia mpaka Babeli, naye atakuwako huko hata nitakapomjilia, asema Bwana; mjapopigana na Wakaldayo hamtafanikiwa. Yeremia 32:5

and he shall bring Zedekiah to Babylon, and there shall he be until I visit him, says Yahweh: though you fight with the Chaldeans, you shall not prosper?

Yeremia akasema, Neno la Bwana limenijia, kusema, Yeremia 32:6

Jeremiah said, The word of Yahweh came to me, saying,

Tazama, Hanameli, mwana wa Shalumu, mjomba wako, atakujia, akisema, Jinunulie shamba langu lililoko Anathothi; maana haki ya ukombozi ni yako, ulinunue. Yeremia 32:7

Behold, Hanamel the son of Shallum your uncle shall come to you, saying, Buy you my field that is in Anathoth; for the right of redemption is yours to buy it.

Basi Hanameli, mwana wa mjomba wangu, akanijia ndani ya uwanda wa walinzi, sawasawa na lile neno la Bwana, akaniambia, Tafadhali, ulinunue shamba langu lililoko Anathothi, katika nchi ya Benyamini; maana haki ya urithi ni yako, na haki ya ukombozi ni yako; ujinunulie. Ndipo nikajua kama neno hili ni neno la Bwana. Yeremia 32:8

So Hanamel my uncle's son came to me in the court of the guard according to the word of Yahweh, and said to me, Please buy my field that is in Anathoth, which is in the land of Benjamin; for the right of inheritance is yours, and the redemption is yours; buy it for yourself. Then I knew that this was the word of Yahweh.

Basi nikalinunua shamba lile lililoko Anathothi kwa Hanameli, mwana wa mjomba wangu, nikampimia fedha yake, shekeli kumi na saba za fedha. Yeremia 32:9

I bought the field that was in Anathoth of Hanamel my uncle's son, and weighed him the money, even seventeen shekels of silver.

Nami nikaitia sahihi ile hati, na kuipiga muhuri, nikawaita mashahidi, nikampimia ile fedha katika mizani. Yeremia 32:10

I subscribed the deed, and sealed it, and called witnesses, and weighed him the money in the balances.

Nikaitwaa ile hati ya kununua, ile iliyopigwa muhuri kama ilivyo sheria na ada, na ile nayo iliyokuwa wazi; Yeremia 32:11

So I took the deed of the purchase, both that which was sealed, containing the terms and conditions, and that which was open;

na ile hati ya kununua nikampa Baruku, mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, mbele ya uso wa Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na mbele ya mashahidi wale walioitia sahihi hati ya kununua, mbele ya Wayahudi wote walioketi katika uwanda wa walinzi. Yeremia 32:12

and I delivered the deed of the purchase to Baruch the son of Neriah, the son of Mahseiah, in the presence of Hanamel my uncle's son, and in the presence of the witnesses who subscribed the deed of the purchase, before all the Jews who sat in the court of the guard.

Nami nikamwagiza Baruku mbele yao, nikisema, Yeremia 32:13

I charged Baruch before them, saying,

Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Twaa hati hizi, hati hii ya kununua, hati hii iliyopigwa muhuri, na hii iliyo wazi pia, ukazitie katika chombo cha udongo, zipate kukaa siku nyingi. Yeremia 32:14

Thus says Yahweh of Hosts, the God of Israel: Take these deeds, this deed of the purchase which is sealed, and this deed which is open, and put them in an earthen vessel; that they may continue many days.

Maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nyumba na mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii. Yeremia 32:15

For thus says Yahweh of Hosts, the God of Israel: Houses and fields and vineyards shall yet again be bought in this land.

Hata nikiisha kumpa Baruku, mwana wa Neria, hati ile ya kununua, nalimwomba Bwana, nikisema, Yeremia 32:16

Now after I had delivered the deed of the purchase to Baruch the son of Neriah, I prayed to Yahweh, saying,

Aa! Bwana MUNGU, tazama, wewe umeziumba mbingu na nchi, kwa uweza wako mkuu na kwa mkono wako ulionyoshwa; hapana neno lililo gumu usiloliweza; Yeremia 32:17

Ah Lord Yahweh! behold, you have made the heavens and the earth by your great power and by your outstretched arm; there is nothing too hard for you,

wewe uwarehemuye watu elfu nyingi, uwalipaye baba za watu uovu wao vifuani mwa watoto wao baada yao; Mungu aliye mkuu, aliye hodari, Bwana wa majeshi ndilo jina lake; Yeremia 32:18

who show loving kindness to thousands, and recompense the iniquity of the fathers into the bosom of their children after them; the great, the mighty God, Yahweh of Hosts is his name;

mkuu wa mashauri, mweza katika kutenda; ambaye macho yake yamefumbuka juu ya njia zote za wanadamu, kumpa kila mtu kwa kadiri ya njia zake, na kwa kadiri ya matunda ya matendo yake, Yeremia 32:19

great in counsel, and mighty in work; whose eyes are open on all the ways of the sons of men, to give everyone according to his ways, and according to the fruit of his doings:

wewe uliyeweka ishara na ajabu katika nchi ya Misri hata siku hii ya leo, katika Israeli na kati ya watu wengine; na kujifanyia jina kama ilivyo leo; Yeremia 32:20

who performed signs and wonders in the land of Egypt, even to this day, both in Israel and among [other] men; and made you a name, as in this day;

ukawatoa watu wako, Israeli, katika nchi ya Misri, kwa ishara, na kwa ajabu, na kwa mkono hodari, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa utisho mkuu; Yeremia 32:21

and brought forth your people Israel out of the land of Egypt with signs, and with wonders, and with a strong hand, and with an outstretched arm, and with great terror;

ukawapa nchi hii, uliyowaapia baba zao kwamba utawapa, nchi iliyojaa maziwa na asali; Yeremia 32:22

and gave them this land, which you did swear to their fathers to give them, a land flowing with milk and honey;

nao wakaingia, wakaimiliki; lakini hawakuitii sauti yako, wala hawakuenda katika sheria yako; hawakutenda neno lo lote katika haya uliyowaagiza wayatende; basi, kwa sababu hii umeleta juu yao mabaya haya yote; Yeremia 32:23

and they came in, and possessed it, but they didn't obey your voice, neither walked in your law; they have done nothing of all that you commanded them to do: therefore you have caused all this evil to come on them.

angalia maboma haya; wameujia mji huu ili kuutwaa; na mji huu umetiwa katika mikono ya Wakaldayo wanaopigana nao, kwa sababu ya upanga, na njaa, na tauni; na hayo uliyosema yamekuwa; na, tazama, wewe unayaona. Yeremia 32:24

Behold, the mounds, they are come to the city to take it; and the city is given into the hand of the Chaldeans who fight against it, because of the sword, and of the famine, and of the pestilence; and what you have spoken has happened; and, behold, you see it.

Nawe, Ee Bwana MUNGU, umeniambia, Jinunulie shamba lile kwa fedha, ukawaite mashahidi; iwapo mji huu umetiwa katika mikono ya Wakaldayo; je! Itakuwaje? Yeremia 32:25

You have said to me, Lord Yahweh, Buy you the field for money, and call witnesses; whereas the city is given into the hand of the Chaldeans.

Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia, kusema, Yeremia 32:26

Then came the word of Yahweh to Jeremiah, saying,

Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? Yeremia 32:27

Behold, I am Yahweh, the God of all flesh: is there anything too hard for me?

Basi, Bwana asema hivi, Tazama, nitautia mji huu katika mikono ya Wakaldayo, na katika mikono ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, naye atautwaa; Yeremia 32:28

Therefore thus says Yahweh: Behold, I will give this city into the hand of the Chaldeans, and into the hand of Nebuchadrezzar king of Babylon, and he shall take it:

na Wakaldayo, wanaopigana na mji huu, watakuja, na kuutia moto mji huu, na kuuteketeza, pamoja na nyumba zake, ambazo juu ya dari zake wamemfukizia Baali uvumba, na kuwamiminia miungu mingine vinywaji, ili kunikasirisha. Yeremia 32:29

and the Chaldeans, who fight against this city, shall come and set this city on fire, and burn it, with the houses, on whose roofs they have offered incense to Baal, and poured out drink-offerings to other gods, to provoke me to anger.

Maana wana wa Israeli, na wana wa Yuda, wametenda yaliyo mabaya tu mbele za uso wangu, tangu ujana wao; maana wana wa Israeli wamenichokoza tu kwa matendo ya mikono yao, asema Bwana. Yeremia 32:30

For the children of Israel and the children of Judah have done only that which was evil in my sight from their youth; for the children of Israel have only provoked me to anger with the work of their hands, says Yahweh.

Kwa kuwa mji huu umekuwa sababu ya kunitia hasira, na sababu ya ghadhabu yangu, tangu siku ile walipoujenga hata siku hii ya leo; ili niuondoe usiwe mbele za uso wangu; Yeremia 32:31

For this city has been to me a provocation of my anger and of my wrath from the day that they built it even to this day; that I should remove it from before my face,

kwa sababu ya mabaya yote ya wana wa Israeli, na ya wana wa Yuda, waliyoyatenda ili kunitia hasira, wao, na wafalme wao, na wakuu wao, na makuhani wao, na manabii wao, na watu wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu. Yeremia 32:32

because of all the evil of the children of Israel and of the children of Judah, which they have done to provoke me to anger, they, their kings, their princes, their priests, and their prophets, and the men of Judah, and the inhabitants of Jerusalem.

Tena wamenigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao; ingawa naliwafundisha, niliondoka mapema na kuwafundisha, lakini hawakusikiliza ili wapate mafundisho. Yeremia 32:33

They have turned to me the back, and not the face: and though I taught them, rising up early and teaching them, yet they have not listened to receive instruction.

Bali waliweka machukizo yao ndani ya nyumba iliyoitwa kwa jina langu, ili kuinajisi. Yeremia 32:34

But they set their abominations in the house which is called by my name, to defile it.

Tena walijenga mahali palipoinuka kwa Baali, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kuwapitisha wana wao na binti zao katika moto kwa ajili ya Moleki, jambo nisilowaagiza; wala halikuingia moyoni mwangu kwamba walitende chukizo hilo; wapate kumkosesha Yuda. Yeremia 32:35

They built the high places of Baal, which are in the valley of the son of Hinnom, to cause their sons and their daughters to pass through [the fire] to Molech; which I didn't command them, neither did it come into my mind, that they should do this abomination, to cause Judah to sin.

Basi sasa, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, katika habari za mji huu, ambao ninyi mnasema juu yake maneno haya, Umetiwa katika mikono ya mfalme wa Babeli, kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni; Yeremia 32:36

Now therefore thus says Yahweh, the God of Israel, concerning this city, about which you say, It is given into the hand of the king of Babylon by the sword, and by the famine, and by the pestilence:

Tazama, nitawakusanya, na kuwatoa katika nchi zote nilikowafukuza, katika hasira yangu, na uchungu wangu, na ghadhabu yangu nyingi; nami nitawaleta tena hata mahali hapa, nami nitawakalisha salama salimini; Yeremia 32:37

Behold, I will gather them out of all the countries, where I have driven them in my anger, and in my wrath, and in great indignation; and I will bring them again to this place, and I will cause them to dwell safely:

nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; Yeremia 32:38

and they shall be my people, and I will be their God:

nami nitawapa moyo mmoja na njia moja, wapate kunicha sikuzote; kwa mema yao, na ya watoto wao baada yao; Yeremia 32:39

and I will give them one heart and one way, that they may fear me forever, for the good of them, and of their children after them:

nami nitafanya agano la milele pamoja nao, kwamba sitageuka wala kuwaacha, ili niwatendee mema; nami nitatia kicho changu mioyoni mwao, ili wasiniache. Yeremia 32:40

and I will make an everlasting covenant with them, that I will not turn away from following them, to do them good; and I will put my fear in their hearts, that they may not depart from me.

Naam, nitafurahi juu yao niwatendee mema, nami nitawapanda katika nchi hii kweli kweli, kwa moyo wangu wote, na kwa roho yangu yote. Yeremia 32:41

Yes, I will rejoice over them to do them good, and I will plant them in this land assuredly with my whole heart and with my whole soul.

Maana Bwana asema hivi, Kama nilivyoleta mabaya makuu haya yote juu ya watu hawa, vivyo hivyo nitaleta juu yao mema hayo yote niliyowaahidia. Yeremia 32:42

For thus says Yahweh: Like as I have brought all this great evil on this people, so will I bring on them all the good that I have promised them.

Na mashamba yatanunuliwa katika nchi hii, mnayoitaja, mkisema, Ni ukiwa, haina mwanadamu wala mnyama; imetiwa katika mikono ya Wakaldayo. Yeremia 32:43

Fields shall be bought in this land, about which you say, It is desolate, without man or animal; it is given into the hand of the Chaldeans.

Watu watanunua mashamba kwa fedha, watazitia sahihi hati zake, na kuzipiga muhuri, na kuwaita mashahidi, katika nchi ya Benyamini, na katika mahali palipo pande zote za Yerusalemu, na katika miji ya Yuda, na katika miji ya nchi yenye vilima, na katika miji ya nchi tambarare, na katika miji ya Negebu; kwa maana nitawarudisha wafungwa wao, asema Bwana. Yeremia 32:44

Men shall buy fields for money, and subscribe the deeds, and seal them, and call witnesses, in the land of Benjamin, and in the places about Jerusalem, and in the cities of Judah, and in the cities of the hill-country, and in the cities of the lowland, and in the cities of the South: for I will cause their captivity to return, says Yahweh.