Sifaeli Mwabuka - Utukufu ni Wako Lyrics
Lyrics
Acha mimi nikushukuru wewe Mungu Uliyenitunza toka utoto wangu Ukanichagua tumboni mwa mama Umeniweka kwenye kusudi lako nisimame
Acha mimi nikushukuru wewe Mungu Uliyenitunza toka utoto wangu Ukanichagua tumboni mwa mama Umeniweka kwenye kusudi lako nisimame
Mimi ni nani kwa yote uliyonitendea? Nimekulipa nini kwa uhai huu nilio nao Mimi ni nani kwa yote uliyonitendea? Nimekulipa nini kwa uhai huu nilio nao
Niseme ni akili zangu baba sio kweli Niseme ni elimu yangu baba sio kweli Niseme ni uzuri wangu baba sio kweli Niseme ni utajiri wangu baba sio kweli
Acha mimi niseme, utukufu nakurudishia wewe Nasema ni asante Mungu wangu, utukufu nakurudishia wewe Mimi ni nani hata naishi leo, utukufu nakurudishia wewe Niliomba mke ukanipa kutoka kwako, utukufu nakurudishia wewe Maombi yangu ukajibu Mungu wangu, utukufu nakurudishia wewe Niliomba kazi ukanipa kazi nzuri, utukufu nakurudishia wewe Ooh Mungu, ee Mungu wangu
Niende kwa nani nikuache wewe Mungu Hatua zangu zaongozwa na wewe Maisha yangu yako mikononi mwako Hata nipitie magumu najua Mungu yuko
Niende kwa nani nikuache wewe Mungu Hatua zangu zaongozwa na wewe Maisha yangu yako mikononi mwako Hata nipitie magumu najua Mungu yuko
Jeuri yangu kwa sababu Mungu unanipenda Ujasiri wangu kwa sababu Mungu unanilinda Jeuri yangu kwa sababu Mungu unanipenda Ujasiri wangu kwa sababu Mungu unanilinda
Niende kwa nani kama si wewe Nimwite nani kama si wewe Yote umefanya baba acha niseme baba asante
Utukufu nakurudishia wewe Nasema ni asante Mungu wangu, utukufu nakurudishia wewe Mimi ni nani hata naishi leo, utukufu nakurudishia wewe Niliomba mke ukanipa kutoka kwako, utukufu nakurudishia wewe Maombi yangu ukajibu Mungu wangu, utukufu nakurudishia wewe Niliomba kazi ukanipa kazi nzuri, utukufu nakurudishia wewe Ooh Mungu, ee Mungu wangu
Video
UTUKUFU NI WAKO-OFFICIAL VIDEO BY SIFAELI MWABUKA 2021