Yoshua 10 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yoshua 10 (Swahili) Joshua 10 (English)

Basi ikawa hapo Adoni-sedeki, mfalme wa Yerusalemu, aliposikia jinsi Yoshua alivyoushika mji wa Ai na kuuharibu kabisa; kama alivyoufanyia mji wa Yeriko na mfalme wake, akaufanya vivyo Ai na mfalme wake; na jinsi wenyeji waliokaa Gibeoni walivyofanya amani na Israeli, na ya kwamba walikuwa kati yao; Yoshua 10:1

Now it happened, when Adoni-zedek king of Jerusalem heard how Joshua had taken Ai, and had utterly destroyed it; as he had done to Jericho and her king, so he had done to Ai and her king; and how the inhabitants of Gibeon had made peace with Israel, and were among them;

ndipo wakacha mno, kwa sababu Gibeoni ulikuwa ni mji mkubwa, kama ilivyo miji ya kifalme mmojawapo, tena kwa sababu ulikuwa ni mji mkubwa kupita Ai, tena watu wake wote walikuwa ni mashujaa. Yoshua 10:2

that they feared greatly, because Gibeon was a great city, as one of the royal cities, and because it was greater than Ai, and all the men of it were mighty.

Basi kwa hiyo Adoni-sedeki, mfalme wa Yerusalemu, akatuma ujumbe kwa Hohamu, mfalme wa Hebroni, na kwa Piramu, mfalme wa Yarmuthi, na kwa Yafia, mfalme wa Lakishi, na kwa Debiri, mfalme wa Egloni, akiwaambia, Yoshua 10:3

Therefore Adoni-zedek king of Jerusalem sent to Hoham king of Hebron, and to Piram king of Jarmuth, and to Japhia king of Lachish, and to Debir king of Eglon, saying,

Haya, kweeni mje kwangu, mnisaidie, tuupige Gibeoni; kwa sababu umefanya mapatano ya amani pamoja na Yoshua na wana wa Israeli. Yoshua 10:4

Come up to me, and help me, and let us strike Gibeon; for it has made peace with Joshua and with the children of Israel.

Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, mfalme wa Yerusalemu, na mfalme wa Hebroni na mfalme wa Yarmuthi na mfalme wa Lakishi, na mfalme wa Egloni, wakakutana pamoja, kisha wakakwea, wao na jeshi zao zote, na kupanga marago yao kinyume cha Gibeoni, na kuupiga vita. Yoshua 10:5

Therefore the five kings of the Amorites, the king of Jerusalem, the king of Hebron, the king of Jarmuth, the king of Lachish, the king of Eglon, gathered themselves together, and went up, they and all their hosts, and encamped against Gibeon, and made war against it.

Ndipo watu wa Gibeoni wakatuma wajumbe kwenda kwa Yoshua huko Gilgali maragoni, wakamwambia, Usiulegeze mkono wako hata ukatuacha sisi watumishi wako; uje kwetu kwa upesi, utuokoe, na kutusaidia; kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao katika nchi ya vilima wamekutana pamoja juu yetu. Yoshua 10:6

The men of Gibeon sent to Joshua to the camp to Gilgal, saying, Don't slack your hand from your servants; come up to us quickly, and save us, and help us: for all the kings of the Amorites that dwell in the hill-country are gathered together against us.

Basi Yoshua akakwea kutoka Gilgali, yeye, na watu wa vita wote pamoja naye, na mashujaa wenye uwezo pia wote. Yoshua 10:7

So Joshua went up from Gilgal, he, and all the people of war with him, and all the mighty men of valor.

Bwana akamwambia Yoshua, Usiwache watu hao; kwa kuwa mimi nimekwisha kuwatia mikononi mwako; hapana mtu awaye yote miongoni mwao atakayesimama mbele yako. Yoshua 10:8

Yahweh said to Joshua, Don't fear them: for I have delivered them into your hands; there shall not a man of them stand before you.

Basi Yoshua akawafikilia ghafula; kwani alikwea kutoka Gilgali kwenda usiku kucha. Yoshua 10:9

Joshua therefore came on them suddenly; [for] he went up from Gilgal all the night.

Bwana naye akawatapanya mbele ya Israeli, naye Israeli akawaua uuaji ulio mkuu hapo Gibeoni, akawafukuza waikimbilie hiyo njia ya kukwelea kwenda Beth-horoni, na kuwapiga hata kufikilia Azeka, tena hata kufikilia Makeda. Yoshua 10:10

Yahweh confused them before Israel, and he killed them with a great slaughter at Gibeon, and chased them by the way of the ascent of Beth Horon, and struck them to Azekah, and to Makkedah.

Kisha ikawa, hapo walipokuwa wakimbia mbele ya Israeli, hapo walipokuwa katika kutelemkia Beth-horoni, ndipo Bwana alipowatupia mawe makubwa kutoka mbinguni juu yao hata kufikilia Azeka, nao wakafa; hao waliokufa kwa kuuawa na hayo mawe ya barafu walikuwa ni wengi kuliko hao waliouawa na wana wa Israeli kwa upanga. Yoshua 10:11

It happened, as they fled from before Israel, while they were at the descent of Beth Horon, that Yahweh cast down great stones from the sky on them to Azekah, and they died: they were more who died with the hailstones than they whom the children of Israel killed with the sword.

Ndipo Yoshua akanena na Bwana katika siku hiyo ambayo Bwana aliwatoa Waamori mbele ya wana wa Israeli; akasema mbele ya macho ya Israeli, Wewe Jua, simama kimya juu ya Gibeoni; Na wewe Mwezi, simama katika bonde la Aiyaloni. Yoshua 10:12

Then spoke Joshua to Yahweh in the day when Yahweh delivered up the Amorites before the children of Israel; and he said in the sight of Israel, Sun, stand you still on Gibeon; You, Moon, in the valley of Aijalon.

Ndipo jua likasimama, na mwezi ukatulia, Hata hilo taifa lilipokuwa limekwisha jipatiliza juu ya adui zao. Yoshua 10:13

The sun stood still, and the moon stayed, Until the nation had avenged themselves of their enemies. Isn't this written in the book of Jashar? The sun stayed in the midst of the sky, and didn't hurry to go down about a whole day.

Haikuwapo siku nyingine mfano wa siku hiyo katika siku zilizotangulia mbele yake wala katika hizo zilizoandama baada yake, hata ikawa yeye Bwana kuisikia sauti ya binadamu; kwa kuwa Bwana alipiga vita kwa ajili ya Israeli. Yoshua 10:14

There was no day like that before it or after it, that Yahweh listened to the voice of a man: for Yahweh fought for Israel.

Basi Yoshua akarudi, na Israeli wote wakarudi pamoja naye, mpaka maragoni hapo Gilgali. Yoshua 10:15

Joshua returned, and all Israel with him, to the camp to Gilgal.

Na hawa wafalme watano wakakimbia, wakajificha ndani ya pango la Makeda. Yoshua 10:16

These five kings fled, and hid themselves in the cave at Makkedah.

Kisha Yoshua aliambiwa habari hiyo, ya kwamba, Hao wafalme watano wameonekana, nao wa hali ya kujificha ndani ya pango la Makeda Yoshua 10:17

It was told Joshua, saying, The five kings are found, hidden in the cave at Makkedah.

Basi Yoshua akasema, Haya, vingirisheni mawe makubwa mdomoni mwa lile pango, kisha wekeni watu hapo ili kuwalinda; Yoshua 10:18

Joshua said, Roll great stones to the mouth of the cave, and set men by it to keep them:

lakini msikae ninyi; wafuatieni adui zenu, mwapige hao walio nyuma; msiwaache wakaingia ndani ya miji yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, amewatia mikononi mwenu. Yoshua 10:19

but don't stay; pursue after your enemies, and strike the hindmost of them; don't allow them to enter into their cities: for Yahweh your God has delivered them into your hand.

Kisha ikawa, hapo Yoshua, na wana wa Israeli, walipokuwa wamekwisha kuwaua watu wengi mno, hata wakaangamizwa, na hayo mabaki yao yaliyowasalia walipokuwa wamekwisha ingia katika miji yao yenye boma, Yoshua 10:20

It happened, when Joshua and the children of Israel had made an end of killing them with a very great slaughter, until they were consumed, and the remnant which remained of them had entered into the fortified cities,

ndipo hao watu wote wakamrudia Yoshua maragoni huko Makeda salama; hakuna mtu awaye yote aliyetoa ulimi kinyume cha hao wana wa Israeli hata mmojawapo. Yoshua 10:21

that all the people returned to the camp to Joshua at Makkedah in peace: none moved his tongue against any of the children of Israel.

Kisha Yoshua akasema, Haya, funua mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano hapa nje ya pango. Yoshua 10:22

Then said Joshua, Open the mouth of the cave, and bring forth those five kings to me out of the cave.

Nao wakafanya, wakamletea hao wafalme watano hapo nje ya pango, yaani, mfalme wa Yerusalemu, na mfalme wa Hebroni, na mfalme wa Yarmuthi, na mfalme wa Lakishi, na mfalme wa Egloni. Yoshua 10:23

They did so, and brought forth those five kings to him out of the cave, the king of Jerusalem, the king of Hebron, the king of Jarmuth, the king of Lachish, the king of Eglon.

Kisha ikawa hapo walipomletea Yoshua hao wafalme watano hapo nje, Yoshua akawaita wanaume wote wa Israeli, akawaambia majemadari wa watu wa vita waliokwenda naye, Haya, jongeeni karibu, mweke nyayo za miguu yenu katika shingo za wafalme hawa. Nao wakajongea karibu, wakatia nyayo zao katika shingo zao. Yoshua 10:24

It happened, when they brought forth those kings to Joshua, that Joshua called for all the men of Israel, and said to the chiefs of the men of war who went with him, Come near, put your feet on the necks of these kings. They came near, and put their feet on the necks of them.

Yoshua akawaambia, Msiche, wala msifadhaike; iweni hodari na wa mioyo ya ushujaa; kwa kuwa ndivyo Bwana atakavyowafanyia adui zenu wote ambao mwapigana nao. Yoshua 10:25

Joshua said to them, Don't be afraid, nor be dismayed; be strong and of good courage: for thus shall Yahweh do to all your enemies against whom you fight.

Baadaye Yoshua akawapiga, na kuwaua, akawatundika katika miti mitano; nao wakawa wakitundikwa katika hiyo miti hata jioni. Yoshua 10:26

Afterward Joshua struck them, and put them to death, and hanged them on five trees: and they were hanging on the trees until the evening.

Kisha wakati wa kuchwa jua, Yoshua akatoa amri, nao wakawatelemsha katika hiyo miti, na kuwatupa katika lile pango ambamo walikuwa walijificha kisha wakatia mawe makubwa mdomoni mwa pango, hata hivi leo. Yoshua 10:27

It happened at the time of the going down of the sun, that Joshua commanded, and they took them down off the trees, and cast them into the cave in which they had hidden themselves, and laid great stones on the mouth of the cave, to this very day.

Siku hiyo Yoshua akautwaa mji wa Makeda, akaupiga kwa makali ya upanga, na mfalme wake; akawaangamiza kabisa na wote pia waliokuwamo ndani yake, hakumwacha hata mmoja aliyesalia; naye akamfanyia huyo mfalme wa Makeda kama alivyomfanyia huyo mfalme wa Yeriko. Yoshua 10:28

Joshua took Makkedah on that day, and struck it with the edge of the sword, and the king of it: he utterly destroyed them and all the souls who were therein; he left none remaining; and he did to the king of Makkedah as he had done to the king of Jericho.

Kisha Yoshua akapita kutoka hapo Makeda, mpaka Libna, na Israeli wote pamoja naye, nao wakapiga Libna; Yoshua 10:29

Joshua passed from Makkedah, and all Israel with him, to Libnah, and fought against Libnah:

Bwana akautia na mji huo pia pamoja na mfalme wake mkononi mwa Israeli; naye akaupiga kwa makali ya upanga, na wote pia waliokuwamo ndani yake; hakumwacha hata mmoja aliyesalia ndani yake; naye akamtenda mfalme wake kama alivyomtenda huyo mfalme wa Yeriko. Yoshua 10:30

and Yahweh delivered it also, and the king of it, into the hand of Israel; and he struck it with the edge of the sword, and all the souls who were therein; he left none remaining in it; and he did to the king of it as he had done to the king of Jericho.

Kisha Yoshua akapita kutoka hapo Libna, na Israeli wote pamoja naye, wakafika Lakishi, wakapanga marago mbele yake na kupigana nao; Yoshua 10:31

Joshua passed from Libnah, and all Israel with him, to Lachish, and encamped against it, and fought against it:

Bwana akautia huo mji wa Lakishi mkononi mwa Israeli, naye akautwaa siku ya pili, akaupiga kwa makali ya upanga, na wote pia waliokuwamo ndani yake, sawasawa na hayo yote aliyoutenda Libna. Yoshua 10:32

and Yahweh delivered Lachish into the hand of Israel; and he took it on the second day, and struck it with the edge of the sword, and all the souls who were therein, according to all that he had done to Libnah.

Wakati huo Horamu, mfalme wa Gezeri, akakwea ili kuusaidia Lakishi, lakini Yoshua akampiga yeye na watu wake, hata asimsazie hata mtu mmoja. Yoshua 10:33

Then Horam king of Gezer came up to help Lachish; and Joshua struck him and his people, until he had left him none remaining.

Kisha Yoshua akapita kutoka hapo Lakishi, na Israeli wote pamoja naye, hata wakafikilia Egloni; nao wakapanga marago mbele yake, na kupigana nao; Yoshua 10:34

Joshua passed from Lachish, and all Israel with him, to Eglon; and they encamped against it, and fought against it;

siku iyo hiyo wakautwaa, nao wakaupiga kwa makali ya upanga, na wote pia waliokuwamo ndani yake akawaangamiza kabisa siku hiyo, sawasawa na hayo yote aliyoufanyia mji wa Lakishi. Yoshua 10:35

and they took it on that day, and struck it with the edge of the sword; and all the souls who were therein he utterly destroyed that day, according to all that he had done to Lachish.

Kisha Yoshua akakwea kutoka hapo Egloni, na Israeli wote pamoja naye, hata wakafikilia Hebroni; nao wakapigana nao; Yoshua 10:36

Joshua went up from Eglon, and all Israel with him, to Hebron; and they fought against it:

wakautwaa, na kuupiga kwa makali ya upanga, na mfalme wake, na miji yake yote, na wote waliokuwamo ndani yake; hakumwacha aliyesalia hata mtu mmoja, sawasawa na hayo yote aliyoufanyia huo mji wa Egloni; lakini akauangamiza kabisa, na wote pia waliokuwamo ndani yake. Yoshua 10:37

and they took it, and struck it with the edge of the sword, and the king of it, and all the cities of it, and all the souls who were therein; he left none remaining, according to all that he had done to Eglon; but he utterly destroyed it, and all the souls who were therein.

Kisha Yoshua akarudi, na Israeli wote pamoja naye, hata Debiri; nao wakapigana nao; Yoshua 10:38

Joshua returned, and all Israel with him, to Debir, and fought against it:

kisha akautwaa, na mfalme wake, na miji yake yote; nao wakawapiga kwa makali ya upanga, wakawaangamiza kabisa wote pia waliokuwamo ndani yake; hakumwacha hata mmoja aliyesalia; kama alivyoufanyia Hebroni aliufanyia na Debiri vivyo, na mfalme wake; kama alivyoufanyia Libna, na mfalme wake. Yoshua 10:39

and he took it, and the king of it, and all the cities of it; and they struck them with the edge of the sword, and utterly destroyed all the souls who were therein; he left none remaining: as he had done to Hebron, so he did to Debir, and to the king of it; as he had done also to Libnah, and to the king of it.

Basi Yoshua akaipiga nchi hiyo yote, nchi ya vilima, na nchi ya Negebu, na nchi ya Shefela, na nchi ya matelemko, na wafalme wake wote; hakumwacha aliyesalia hata mmoja; lakini akawaharibu kabisa wote waliokuwa wavuta pumzi, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyoamuru. Yoshua 10:40

So Joshua struck all the land, the hill-country, and the South, and the lowland, and the slopes, and all their kings: he left none remaining, but he utterly destroyed all that breathed, as Yahweh, the God of Israel, commanded.

Yoshua akawapiga kutoka Kadesh-barnea mpaka Gaza, na nchi yote ya Gosheni, hata Gibeoni. Yoshua 10:41

Joshua struck them from Kadesh-barnea even to Gaza, and all the country of Goshen, even to Gibeon.

Na wafalme hao wote na nchi zao Yoshua akatwaa, wakati huo, kwa sababu yeye Bwana, Mungu wa Israeli, alipigana kwa ajili ya Israeli, Yoshua 10:42

All these kings and their land did Joshua take at one time, because Yahweh, the God of Israel, fought for Israel.

Kisha Yoshua akarudi, na Israeli wote pamoja naye, hata marago yao huko Gilgali. Yoshua 10:43

Joshua returned, and all Israel with him, to the camp to Gilgal.