Yoshua 23 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yoshua 23 (Swahili) Joshua 23 (English)

Hata ikawa baada ya siku nyingi, Bwana alipokuwa amekwisha kuwapa Israeli raha mbele ya adui zao pande zote, naye Yoshua alipokuwa mzee, mwenye miaka mingi sana, Yoshua 23:1

It happened after many days, when Yahweh had given rest to Israel from all their enemies round about, and Joshua was old and well stricken in years;

Yoshua akawaita Israeli wote, wazee wao, na wakuu wao, na makadhi yao, na maakida yao, akawaambia, Mimi ni mzee, nami nimekwendelea sana katika miaka yangu; Yoshua 23:2

that Joshua called for all Israel, for their elders and for their heads, and for their judges and for their officers, and said to them, I am old and well stricken in years:

nanyi mmeona mambo yote ambayo Bwana, Mungu wenu, amewatenda mataifa haya yote kwa ajili yenu; kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye aliyewapigania ninyi. Yoshua 23:3

and you have seen all that Yahweh your God has done to all these nations because of you; for Yahweh your God, he it is that has fought for you.

Tazama, nimewagawieni kwa kura mataifa haya yaliyobaki, yawe urithi kwa kabila zenu, toka mto wa Yordani, pamoja na mataifa yote niliyowakatilia mbali, mpaka bahari kubwa upande wa machweo ya jua. Yoshua 23:4

Behold, I have allotted to you these nations that remain, to be an inheritance for your tribes, from the Jordan, with all the nations that I have cut off, even to the great sea toward the going down of the sun.

Yeye Bwana, Mungu wenu, atawatoa kwa nguvu mbele yenu, atawafukuza wasiwe mbele ya macho yenu tena; nanyi mtaimiliki nchi yao, kama Bwana Mungu wenu, alivyowaambia. Yoshua 23:5

Yahweh your God, he will thrust them out from before you, and drive them from out of your sight; and you shall possess their land, as Yahweh your God spoke to you.

Basi, iweni mashujaa sana kuyashika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati ya Musa, na kuyatenda, msiyaache kwa kugeukia upande wa kuume wala upande wa kushoto. Yoshua 23:6

Therefore be you very courageous to keep and to do all that is written in the book of the law of Moses, that you not turn aside from it to the right hand or to the left;

Msiingie kati ya mataifa haya, yaani, haya yaliyobaki kati yenu; wala msitaje majina ya miungu yao, wala kuwaapisha watu kwa majina hayo, wala kuitumikia, wala kujiinamisha mbele yao; Yoshua 23:7

that you not come among these nations, these that remain among you; neither make mention of the name of their gods, nor cause to swear [by them], neither serve them, nor bow down yourselves to them;

bali shikamaneni na Bwana, Mungu wenu, kama mlivyotenda hata hivi leo. Yoshua 23:8

but cleave to Yahweh your God, as you have done to this day.

Maana Bwana amefukuza mbele yenu mataifa walio hodari, kisha wenye nguvu, lakini kwenu ninyi hapana mtu aliyesimama mbele yenu hata leo. Yoshua 23:9

For Yahweh has driven out from before you great nations and strong: but as for you, no man has stood before you to this day.

Mtu mmoja miongoni mwenu atafukuza watu elfu; maana Bwana, Mungu wenu, ndiye anayewapigania, kama alivyowaambia. Yoshua 23:10

One man of you shall chase a thousand; for Yahweh your God, he it is who fights for you, as he spoke to you.

Jihadharini nafsi zenu, basi, ili mmpende Bwana, Mungu wenu. Yoshua 23:11

Take good heed therefore to yourselves, that you love Yahweh your God.

Lakini mkirudi nyuma kwa njia yo yote na kushikamana na mabaki ya mataifa, yaani, mataifa haya yaliyobaki kati yenu, na kuoana nao, na kuingia kwao, nao kuingia kwenu; Yoshua 23:12

Else if you do at all go back, and cleave to the remnant of these nations, even these who remain among you, and make marriages with them, and go in to them, and they to you;

jueni hakika ya kuwa Bwana, Mungu wenu, hatawafukuza tena mataifa haya mbele ya macho yenu, bali watakuwa mtego kwenu na tanzi, na mjeledi mbavuni mwenu, na miiba machoni mwenu, hata mtakapoangamia na kutoka katika nchi hii njema, ambayo Bwana, Mungu wenu, amewapa ninyi. Yoshua 23:13

know for a certainty that Yahweh your God will no more drive these nations from out of your sight; but they shall be a snare and a trap to you, and a scourge in your sides, and thorns in your eyes, until you perish from off this good land which Yahweh your God has given you.

Angalieni, mimi leo ninakwenda njia ile waendayo watu wote wa ulimwengu; nanyi nyote mnajua mioyoni mwenu, na rohoni mwenu, ya kuwa halikuwapungukia ninyi hata neno moja katika mambo hayo mema yote aliyoyanena Bwana, Mungu wenu, katika habari zenu; yote yametimia kwenu hapana neno lo lote mlilopungukiwa. Yoshua 23:14

Behold, this day I am going the way of all the earth: and you know in all your hearts and in all your souls, that not one thing has failed of all the good things which Yahweh your God spoke concerning you; all are happen to you, not one thing has failed of it.

Kisha itakuwa, kama yalivyowafikilia yale mambo mema yote, Bwana, Mungu wenu, aliyowaahidia ninyi, kadhalika Bwana atawafikilizia mabaya yote, hata atakapokuwa amewaangamiza katika nchi hii njema, Bwana Mungu wenu, aliyowapa. Yoshua 23:15

It shall happen, that as all the good things are come on you of which Yahweh your God spoke to you, so will Yahweh bring on you all the evil things, until he have destroyed you from off this good land which Yahweh your God has given you.

Hapo mtakapolivunja agano la Bwana, Mungu wenu, alilowaamuru, na kwenda kuitumikia miungu mingine, na kujiinamisha mbele yao, ndipo hasira ya Bwana itakapowaka juu yenu, nanyi mtaangamia upesi katika nchi hii njema aliyowapa. Yoshua 23:16

When you disobey the covenant of Yahweh your God, which he commanded you, and go and serve other gods, and bow down yourselves to them; then will the anger of Yahweh be kindled against you, and you shall perish quickly from off the good land which he has given to you.