Yoshua 14 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yoshua 14 (Swahili) Joshua 14 (English)

Kisha hizi ndizo nchi ambazo wana wa Israeli walizitwaa katika nchi ya Kanaani, ambazo Eleazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na vichwa vya nyumba za mababa wa kabila za Israeli, waliwagawanyia, Yoshua 14:1

These are the inheritances which the children of Israel took in the land of Canaan, which Eleazar the priest, and Joshua the son of Nun, and the heads of the fathers' [houses] of the tribes of the children of Israel, distributed to them,

kwa kuandama hiyo kura ya urithi wao, vile vile kama Bwana alivyoamuru kwa mkono wa Musa, kwa ajili ya hizo kabila kenda, na hiyo nusu ya kabila. Yoshua 14:2

by the lot of their inheritance, as Yahweh commanded by Moses, for the nine tribes, and for the half-tribe.

Kwa kuwa Musa alikuwa amekwisha kuwapa urithi hizo kabila mbili na nusu, ng'ambo ya pili ya Yordani; lakini hakuwapa Walawi urithi uwao wote kati yao. Yoshua 14:3

For Moses had given the inheritance of the two tribes and the half-tribe beyond the Jordan: but to the Levites he gave no inheritance among them.

Kwa kuwa wana wa Yusufu walikuwa kabila mbili, Manase na Efraimu; nao hawakuwapa Walawi sehemu katika hiyo nchi, isipokuwa waliwapa miji wapate kuikaa, pamoja na viunga vyake kwa ajili ya wanyama wao wa mifugo, na kwa ajili ya riziki zao. Yoshua 14:4

For the children of Joseph were two tribes, Manasseh and Ephraim: and they gave no portion to the Levites in the land, save cities to dwell in, with the suburbs of it for their cattle and for their substance.

Vile vile kama Bwana alivyomwamuru Musa, hao wana wa Israeli walifanya vivyo, nao wakaigawanya hiyo nchi. Yoshua 14:5

As Yahweh commanded Moses, so the children of Israel did; and they divided the land.

Wakati huo wana wa Yuda walimkaribia Yoshua hapo Gilgali; na Kalebu, mwana wa Yefune, huyo Mkenizi, akamwambia, Wewe wajua hilo neno Bwana alilomwambia Musa, huyo mtu wa Mungu, katika habari zangu, na katika habari zako wewe, tulipokuwa katika Kadesh-barnea. Yoshua 14:6

Then the children of Judah drew near to Joshua in Gilgal: and Caleb the son of Jephunneh the Kenizzite said to him, You know the thing that Yahweh spoke to Moses the man of God concerning me and concerning you in Kadesh-barnea.

Mimi nilikuwa mtu wa miaka arobaini umri wangu, hapo Musa mtumishi wa Bwana aliponituma niende kutoka Kadesh-barnea ili kuipeleleza hiyo nchi; nami nilimletea habari tena, kama ilivyokuwa ndani ya moyo wangu. Yoshua 14:7

Forty years old was I when Moses the servant of Yahweh sent me from Kadesh-barnea to spy out the land; and I brought him word again as it was in my heart.

Lakini wale ndugu zangu waliokwea kwenda pamoja nami waliiyeyusha mioyo ya watu; ila mimi nilimfuata Bwana, Mungu wangu, kwa utimilifu. Yoshua 14:8

Nevertheless my brothers who went up with me made the heart of the people melt; but I wholly followed Yahweh my God.

Kisha Musa akaniapia siku hiyo, akasema, Hakika hiyo nchi ambayo miguu yako imekanyaga itakuwa ni urithi kwako wewe, na kwa watoto wako milele, kwa sababu wewe umemfuata Bwana, Mungu wako, kwa utimilifu. Yoshua 14:9

Moses swore on that day, saying, Surely the land whereon your foot has trodden shall be an inheritance to you and to your children forever, because you have wholly followed Yahweh my God.

Sasa basi, angalia, yeye Bwana ameniweka hai, kama alivyosema, miaka hii arobaini na mitano, tangu wakati huo Bwana alipomwambia Musa neno hilo, wakati Israeli waliokuwa wakienenda barani; na sasa tazama, hivi leo nimepata miaka themanini na mitano umri wangu. Yoshua 14:10

Now, behold, Yahweh has kept me alive, as he spoke, these forty-five years, from the time that Yahweh spoke this word to Moses, while Israel walked in the wilderness: and now, behold, I am this day eighty-five years old.

Hata sasa mimi nina nguvu zangu hivi leo kama nilivyokuwa siku hiyo Musa aliyonituma; kama nguvu zangu zilivyokuwa wakati huo, na nguvu zangu ndivyo zilivyo sasa, kwa vita na kwa kutoka nje na kuingia ndani. Yoshua 14:11

As yet I am as strong this day as I as in the day that Moses sent me: as my strength was then, even so is my strength now, for war, and to go out and to come in.

Basi sasa unipe mlima huu, ambao Bwana alinena habari zake siku hiyo; kwani wewe ulisikia siku hiyo jinsi Waanaki walivyokuwa huko, na miji ilivyokuwa mikubwa yenye boma; yumkini yeye Bwana atakuwa pamoja nami, nami nitawafukuza watoke nje, kama Bwana alivyonena. Yoshua 14:12

Now therefore give me this hill-country, of which Yahweh spoke in that day; for you heard in that day how the Anakim were there, and cities great and fortified: it may be that Yahweh will be with me, and I shall drive them out, as Yahweh spoke.

Yoshua akambarikia, akampa Kalebu, huyo mwana wa Yefune, Hebroni kuwa urithi wake. Yoshua 14:13

Joshua blessed him; and he gave Hebron to Caleb the son of Jephunneh for an inheritance.

Kwa hiyo Hebroni ukawa urithi wa Kalebu, mwana wa Yefune, Mkenizi, hata leo; kwa sababu alimwandama Bwana, Mungu wa Israeli, kwa utimilifu. Yoshua 14:14

Therefore Hebron became the inheritance of Caleb the son of Jephunneh the Kenizzite to this day; because that he wholly followed Yahweh, the God of Israel.

Basi jina la Hebroni hapo kwanza uliitwa Kiriath-arba; huyo Arba alikuwa ni mtu mkubwa kupita wenziwe wote katika hao Waanaki. Hiyo nchi nayo ikatulia, vita vikakoma.

Yoshua 14:15

Now the name of Hebron before was Kiriath Arba; [which Arba was] the greatest man among the Anakim. The land had rest from war.