Yoshua 19 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yoshua 19 (Swahili) Joshua 19 (English)

Kisha kura ya pili ilitokea kwa ajili ya Simeoni, maana, kwa ajili ya hiyo kabila ya wana wa Simeoni, kwa kuandama jamaa zao; na urithi wao ulikuwa katikati ya urithi wa wana wa Yuda. Yoshua 19:1

The second lot came out for Simeon, even for the tribe of the children of Simeon according to their families: and their inheritance was in the midst of the inheritance of the children of Judah.

Miji waliyokuwa nayo katika urithi wao ni Beer-sheba, na Sheba, na Molada; Yoshua 19:2

They had for their inheritance Beersheba, or Sheba, and Moladah,

na Hasarshuali, na Bala, na Esemu; Yoshua 19:3

and Hazar Shual, and Balah, and Ezem,

na Eltoladi, na Bethuli, na Horma; Yoshua 19:4

and Eltolad, and Bethul, and Hormah,

na Siklagi, na Bethmarkabothi, na Hasarsusa; Yoshua 19:5

and Ziklag, and Beth Marcaboth, and Hazar Susah,

na Bethlebaothi, na Sharuheni; miji kumi na mitatu, pamoja na vijiji vyake; Yoshua 19:6

and Beth Lebaoth, and Sharuhen; thirteen cities with their villages:

na Aini, na Rimoni, na Etheri, na Ashani; miji minne, pamoja na vijiji vyake; Yoshua 19:7

Ain, Rimmon, and Ether, and Ashan; four cities with their villages:

tena vijiji vyote vilivyozunguka miji hiyo kote kote mpaka Baalath-beeri, Rama wa Kusini. Huo ndio urithi wa kabila ya wana wa Simeoni kwa kuandama jamaa zao. Yoshua 19:8

and all the villages that were round about these cities to Baalath Beer, Ramah of the South. This is the inheritance of the tribe of the children of Simeon according to their families.

Huo urithi wa hao wana wa Simeoni ulitoka katika fungu la wana wa Yuda; kwa maana hilo fungu la wana wa Yuda lilikuwa ni kubwa mno kwao; kwa hiyo wana wa Simeoni walikuwa na urithi katikati ya urithi wao. Yoshua 19:9

Out of the part of the children of Judah was the inheritance of the children of Simeon; for the portion of the children of Judah was too much for them: therefore the children of Simeon had inheritance in the midst of their inheritance.

Kisha kura ya tatu ilitokea kwa ajili ya wana wa Zabuloni kwa kuandama jamaa zao; na mpaka wa urithi wao ulifikilia hata Saridi; Yoshua 19:10

The third lot came up for the children of Zebulun according to their families; and the border of their inheritance was to Sarid;

kisha mpaka wao ukakwea kwendelea upande wa magharibi, hata kufikilia Marala, nao ukafikilia hata Dabeshethi; nao ukafikilia kijito cha maji kilicho mkabala wa Yokneamu; Yoshua 19:11

and their border went up westward, even to Maralah, and reached to Dabbesheth; and it reached to the brook that is before Jokneam;

kisha ukazunguka kutoka Saridi kwendelea upande wa mashariki kwa kuelekea maawio ya jua hata kufikilia mpaka wa Kisiloth-ubori; kisha ukatokea hata Daberathi, kisha ukakwea kwendelea Yafia; Yoshua 19:12

and it turned from Sarid eastward toward the sunrise to the border of Chisloth Tabor; and it went out to Daberath, and went up to Japhia;

kutoka hapo ukaendelea kuelekea mashariki mpaka Gath-heferi, hata kufikilia Ethkasini; kisha ukatokea huko Rimoni ufikiliao hata Nea; Yoshua 19:13

and from there it passed along eastward to Gath Hepher, to Eth-kazin; and it went out at Rimmon which stretches to Neah;

kisha mpaka uliizunguka nchi hiyo kwa upande wa kaskazini hata Hanathoni; kisha matokeo yake yalikuwa katika bonde la Iftaeli; Yoshua 19:14

and the border turned about it on the north to Hannathon; and the goings out of it were at the valley of Iphtah El;

na Katathi, na Nahalali, na Shimroni, na Idala, na Bethlehemu; miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake. Yoshua 19:15

and Kattath, and Nahalal, and Shimron, and Idalah, and Bethlehem: twelve cities with their villages.

Huu ndio urithi wa wana wa Zabuloni kwa kuandama jamaa zao; miji hii pamoja na vijiji vyake. Yoshua 19:16

This is the inheritance of the children of Zebulun according to their families, these cities with their villages.

Kisha kura ya nne ilitokea kwa ajili ya Isakari, maana, ni kwa ajili ya wana wa Isakari kwa kuandama jamaa zao. Yoshua 19:17

The fourth lot came out for Issachar, even for the children of Issachar according to their families.

Na mpaka wao ulifikilia Yezreeli, na Kesulothi, na Shunemu; Yoshua 19:18

Their border was to Jezreel, and Chesulloth, and Shunem,

na Hafaraimu, na Shioni, na Anaharathi; Yoshua 19:19

and Hapharaim, and Shion, and Anaharath,

na Rabithu, na Kishioni, na Ebesi; Yoshua 19:20

and Rabbith, and Kishion, and Ebez,

na Remethi, na Enganimu, na Enhada, na Bethpasesi; Yoshua 19:21

and Remeth, and Engannim, and En Haddah, and Beth Pazzez,

na mpaka ukafikilia hata Tabori, na Shahasuma na Bethshemeshi; na matokeo ya mpaka wao yalikuwa katika mto wa Yordani; miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake. Yoshua 19:22

and the border reached to Tabor, and Shahazumah, and Beth-shemesh; and the goings out of their border were at the Jordan: sixteen cities with their villages.

Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Isakari kwa kuandama jamaa zao; miji hiyo pamoja na vijiji vyake. Yoshua 19:23

This is the inheritance of the tribe of the children of Issachar according to their families, the cities with their villages.

Kisha kura ya tano ilitokea kwa ajili ya kabila ya wana wa Asheri kwa kuandama jamaa zao. Yoshua 19:24

The fifth lot came out for the tribe of the children of Asher according to their families.

Na mpaka wao ulikuwa ni Helkathi, na Hali, na Beteni, na Akishafu; Yoshua 19:25

Their border was Helkath, and Hali, and Beten, and Achshaph,

na Alameleki, na Amadi, na Mishali; nao ukafikilia hata Karmeli upande wa magharibi, tena ulifikilia hata Shihor-libnathi; Yoshua 19:26

and Allammelech, and Amad, and Mishal; and it reached to Carmel westward, and to Shihorlibnath;

kisha ukazunguka kuelekea maawio ya jua mpaka Beth-dagoni, nao ukafikilia hata Zabuloni, tena mpaka bonde la Iftaeli upande wa kaskazini hata Bethemeki na Neyeli; kisha ukatokea hata Kabuli upande wa kushoto; Yoshua 19:27

and it turned toward the sunrise to Beth Dagon, and reached to Zebulun, and to the valley of Iphtah El northward to Beth Emek and Neiel; and it went out to Cabul on the left hand,

na Ebroni, na Rehobu, na Hamoni, na Kana, hata kufikilia Sidoni mkuu; Yoshua 19:28

and Ebron, and Rehob, and Hammon, and Kanah, even to great Sidon;

kisha mpaka ulizunguka kuelekea Rama, na mji wa Tiro ulio na boma; kisha mpaka ulizunguka kuelekea Hosa; na matokeo yake yalikuwa baharini katika nchi ya Akzibu; Yoshua 19:29

and the border turned to Ramah, and to the fortified city of Tyre; and the border turned to Hosah; and the goings out of it were at the sea by the region of Achzib;

na Uma pia, na Afeka, na Rehobu; miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake. Yoshua 19:30

Ummah also, and Aphek, and Rehob: twenty-two cities with their villages.

Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Asheri kwa kuandama jamaa zao; miji hii pamoja na vijiji vyake. Yoshua 19:31

This is the inheritance of the tribe of the children of Asher according to their families, these cities with their villages.

Kisha kura ya sita ikatokea kwa ajili ya wana wa Naftali, maana, ni kwa ajili ya wana wa Naftali kwa kuandama jamaa zao. Yoshua 19:32

The sixth lot came out for the children of Naphtali, even for the children of Naphtali according to their families.

Na mpaka wao ulikuwa kutoka Helefu, tokea ule mwaloni ulio katika Saananimu, na Adami-nekebu, na Yabineeli, hata kufikilia Lakumu; na matokeo yake yalikuwa katika mto wa Yordani; Yoshua 19:33

Their border was from Heleph, from the oak in Zaanannim, and Adaminekeb, and Jabneel, to Lakkum; and the goings out of it were at the Jordan;

tena mpaka ulizunguka kwendelea upande wa magharibi hata Aznoth-tabori, tena kutoka hapo ukaendelea mpaka Hukoki; kisha ukafikilia hata Zabuloni upande wa kusini, tena ulifikilia hata Asheri upande wa magharibi, tena ulifikilia hata Yuda hapo katika mto wa Yordani kwa upande wa kuelekea maawio ya jua. Yoshua 19:34

and the border turned westward to Aznoth Tabor, and went out from there to Hukkok; and it reached to Zebulun on the south, and reached to Asher on the west, and to Judah at the Jordan toward the sunrise.

Na miji yenye boma ilikuwa ni hii, Sidimu, na Seri, na Hamathi, na Rakathi, na Kinerethi; Yoshua 19:35

The fortified cities were Ziddim, Zer, and Hammath, Rakkath, and Chinnereth,

na Adama, na Rama, na Hazori; Yoshua 19:36

and Adamah, and Ramah, and Hazor,

na Kedeshi, na Edrei, na Enhasori; Yoshua 19:37

and Kedesh, and Edrei, and En Hazor,

na Ironi, na Migdal-eli, na Horemu, na Bethanathi, na Bethshemeshi; miji kumi na kenda, pamoja na vijiji vyake. Yoshua 19:38

Iron, and Migdal-el, Horem, and Beth Anath, and Beth-shemesh; nineteen cities with their villages.

Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Naftali kwa kuandama jamaa zao; miji hiyo pamoja na vijiji vyake. Yoshua 19:39

This is the inheritance of the tribe of the children of Naphtali according to their families, the cities with their villages.

Kisha kura ya saba ilitokea kwa ajili ya kabila ya wana wa Dani kwa kuandama jamaa zao. Yoshua 19:40

The seventh lot came out for the tribe of the children of Dan according to their families.

Na mpaka wa urithi wao ulikuwa ni Sora, na Eshtaoli, na Irishemeshi; Yoshua 19:41

The border of their inheritance was Zorah, and Eshtaol, and Irshemesh,

na Shaalabini, na Aiyaloni, na Ithla; Yoshua 19:42

and Shaalabbin, and Aijalon, and Ithlah,

na Eloni, na Timna, na Ekroni; Yoshua 19:43

and Elon, and Timnah, and Ekron,

na Elteka, na Gibethoni, na Baalathi; Yoshua 19:44

and Eltekeh, and Gibbethon, and Baalath,

na Yehudi, na Bene-beraki, na Gathrimoni; Yoshua 19:45

and Jehud, and Bene-berak, and Gath-rimmon,

na Meyarkoni, na Rakoni, pamoja na huo mpaka uliokuwa mkabala wa Yafa. Yoshua 19:46

and Me-jarkon, and Rakkon, with the border over against Joppa.

Kisha mpaka wa wana wa Dani ulitokea kuwapita wao; kwa kuwa hao wana wa Dani wakakwea na kupigana na Leshemu, na kuutwaa, na kuupiga kwa makali ya upanga, na kuumiliki, nao wakakaa humo, wakauita Dani, kwa kuliandama jina la huyo Dani mzee wao. Yoshua 19:47

The border of the children of Dan went out beyond them; for the children of Dan went up and fought against Leshem, and took it, and struck it with the edge of the sword, and possessed it, and lived therein, and called Leshem, Dan, after the name of Dan their father.

Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Dani kwa kuandama jamaa zao; miji hii pamoja na vijiji vyake. Yoshua 19:48

This is the inheritance of the tribe of the children of Dan according to their families, these cities with their villages.

Basi wakamaliza hiyo kazi yao ya kuigawanya nchi iwe urithi kwa kuandama mipaka yake; kisha wana wa Israeli wakampa Yoshua, mwana wa Nuni, urithi katikati yao; Yoshua 19:49

So they made an end of distributing the land for inheritance by the borders of it; and the children of Israel gave an inheritance to Joshua the son of Nun in the midst of them:

sawasawa na ile amri ya Bwana wakampa mji alioutaka, maana, ni Timnath-sera katika nchi ya vilima ya Efraimu; naye akaujenga huo mji na kukaa mumo. Yoshua 19:50

according to the commandment of Yahweh they gave him the city which he asked, even Timnathserah in the hill-country of Ephraim; and he built the city, and lived therein.

Hizi ndizo nchi, ambazo Eleazari kuhani, na Yoshua huyo mwana wa Nuni, pamoja na hao vichwa vya nyumba za mababa ya kabila za wana wa Israeli, walizigawanya kwa njia ya kupiga kura, ziwe urithi, huko Shilo mbele ya Bwana, hapo mlangoni mwa hema ya kukutania. Basi hivyo wakamaliza kazi ya kuigawanya hiyo nchi. Yoshua 19:51

These are the inheritances, which Eleazar the priest, and Joshua the son of Nun, and the heads of the fathers' [houses] of the tribes of the children of Israel, distributed for inheritance by lot in Shiloh before Yahweh, at the door of the tent of meeting. So they made an end of dividing the land.