1
Akapanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao.
Jesus got into a boat, crossed over, and came to His own town.
2
Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
Just then some men brought to Him a paralytic lying on a mat. When Jesus saw their faith, He said to the paralytic, “Take courage, son; your sins are forgiven.”
3
Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.
On seeing this, some of the scribes said to themselves, “This man is blaspheming!”
4
Naye Yesu, hali akijua mawazo yao, akasema, Mbona mnawaza maovu mioyoni mwenu?
But Jesus knew what they were thinking and said, “Why do you harbor evil in your hearts?
5
Kwa maana rahisi ni lipi, ni kusema, Umesamehewa dhambi zako, au ni kusema, Ondoka, uende?
Which is easier: to say, ‘Your sins are forgiven,’ or to say, ‘Get up and walk’?
6
Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (amwambia yule mwenye kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako.
But so that you may know that the Son of Man has authority on earth to forgive sins...” Then He said to the paralytic, “Get up, pick up your mat, and go home.”
7
Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake.
And the man got up and went home.
8
Makutano walipomwona, walishikwa na hofu, wakamtukuza Mungu, aliyewapa watu amri ya namna hii.
When the crowds saw this, they were filled with awe and glorified God, who had given such authority to men.
9
Naye Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate. Akaondoka, akamfuata.
As Jesus went on from there, He saw a man named Matthew sitting at the tax booth. “Follow Me,” He told him, and Matthew got up and followed Him.
10
Ikawa alipoketi nyumbani ale chakula, tazama, watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuja wakaketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake.
Later, as Jesus was dining at Matthew’s house, many tax collectors and sinners came and ate with Him and His disciples.
11
Mafarisayo walipoona, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?
When the Pharisees saw this, they asked His disciples, “Why does your Teacher eat with tax collectors and sinners?”
12
Naye aliposikia, aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi.
On hearing this, Jesus said, “It is not the healthy who need a doctor, but the sick.
13
Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.
But go and learn what this means: ‘I desire mercy, not sacrifice.’ For I have not come to call the righteous, but sinners.”
14
Wakati ule wanafunzi wake Yohana wakamwendea, wakasema, Kwa nini sisi na Mafarisayo twafunga, bali wanafunzi wako hawafungi?
Then John’s disciples came to Jesus and asked, “Why is it that we and the Pharisees fast so often, but Your disciples do not fast?”
15
Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana arusi; ndipo watakapofunga.
Jesus replied, “How can the guests of the bridegroom mourn while He is with them? But the time will come when the bridegroom will be taken from them; then they will fast.
16
Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu; maana kile kilichotiwa huondoa kipande cha lile vazi, na pale palipotatuka huzidi.
No one sews a patch of unshrunk cloth on an old garment. For the patch will pull away from the garment, and a worse tear will result.
17
Wala watu hawatii divai mpya katika viriba vikuukuu; na kama wakitia, vile viriba hupasuka, divai ikamwagika, na viriba vikaharibika; bali hutia divai mpya katika viriba vipya, vikahifadhika vyote.
Neither do men pour new wine into old wineskins. If they do, the skins will burst, the wine will spill, and the wineskins will be ruined. Instead, they pour new wine into new wineskins, and both are preserved.”
18
Alipokuwa akiwaambia hayo, tazama, akaja jumbe mmoja, akamsujudia, akisema, Binti yangu sasa hivi amekufa; lakini njoo, uweke mkono wako juu yake, naye ataishi.
While Jesus was saying these things, a synagogue leader came and knelt before Him. “My daughter has just died,” he said. “But come and place Your hand on her, and she will live.”
19
Akaondoka Yesu, akamfuata, pamoja na wanafunzi wake.
So Jesus got up and went with him, along with His disciples.
20
Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.
Suddenly a woman who had suffered from bleeding for twelve years came up behind Him and touched the fringe of His cloak.
21
Kwa maana alisema moyoni mwake, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.
She said to herself, “If only I touch His cloak, I will be healed.”
22
Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.
Jesus turned and saw her. “Take courage, daughter,” He said, “your faith has healed you.” And the woman was healed from that very hour.
23
Yesu alipofika nyumbani kwa yule jumbe, aliona wapiga filimbi, na makutano wakifanya maombolezo,
When Jesus entered the house of the synagogue leader, He saw the flute players and the noisy crowd.
24
akawaambia, Ondokeni; kwa maana kijana hakufa, amelala tu. Wakamcheka sana.
“Go away,” He told them. “The girl is not dead, but asleep.” And they laughed at Him.
25
Lakini makutano walipoondoshwa, aliingia, akamshika mkono; yule kijana akasimama.
After the crowd had been put outside, Jesus went in and took the girl by the hand, and she got up.
26
Zikaenea habari hizi katika nchi ile yote.
And the news about this spread throughout that region.
27
Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, Uturehemu, Mwana wa Daudi.
As Jesus went on from there, two blind men followed Him, crying out, “Have mercy on us, Son of David!”
28
Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana.
After Jesus had entered the house, the blind men came to Him. “Do you believe that I am able to do this?” He asked. “Yes, Lord,” they answered.
29
Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate.
Then He touched their eyes and said, “According to your faith will it be done to you.”
30
Macho yao yakafumbuka. Naye Yesu akawaagiza kwa nguvu, akisema, Angalieni hata mtu mmoja asijue.
And their eyes were opened. Jesus warned them sternly, “See that no one finds out about this!”
31
Lakini wakatoka, wakaeneza habari zake katika nchi ile yote.
But they went out and spread the news about Him throughout the land.
32
Hata hao walipokuwa wakitoka, tazama, walimletea mtu bubu mwenye pepo.
As they were leaving, a demon-possessed man who was mute was brought to Jesus.
33
Na pepo alipotolewa, yule bubu alinena, makutano wakastajabu, wakasema, Haijaonekana hivi katika Israeli wakati wo wote.
And when the demon had been driven out, the man began to speak. The crowds were amazed and said, “Nothing like this has ever been seen in Israel!”
34
Lakini Mafarisayo wakasema, Kwa nguvu za mkuu wa pepo atoa pepo.
But the Pharisees said, “It is by the prince of demons that He drives out demons.”
35
Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.
Jesus went through all the towns and villages, teaching in their synagogues, preaching the gospel of the kingdom, and healing every disease and sickness.
36
Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.
When He saw the crowds, He was moved with compassion for them, because they were harassed and helpless, like sheep without a shepherd.
37
Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache.
Then He said to His disciples, “The harvest is plentiful, but the workers are few.
38
Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.
Ask the Lord of the harvest, therefore, to send out workers into His harvest.”