1
Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua;
When morning came, all the chief priests and elders of the people conspired against Jesus to put Him to death.
2
wakamfunga, wakamchukua, wakampeleka kwa Pilato aliyekuwa liwali.
They bound Him, led Him away, and handed Him over to Pilate the governor.
3
Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia.
When Judas, who had betrayed Him, saw that Jesus was condemned, he was filled with remorse and returned the thirty pieces of silver to the chief priests and elders.
4
Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.
“I have sinned by betraying innocent blood,” he said. “What is that to us?” they replied. “You bear the responsibility.”
5
Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga.
So Judas threw the silver into the temple and left. Then he went away and hanged himself.
6
Wakuu wa makuhani wakavitwaa vile vipande vya fedha, wakasema, Si halali kuviweka katika sanduku ya sadaka, kwa kuwa ni kima cha damu.
The chief priests picked up the pieces of silver and said, “It is unlawful to put this into the treasury, since it is blood money.”
7
Wakafanya shauri, wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
After conferring together, they used the money to buy the potter’s field as a burial place for foreigners.
8
Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo.
That is why it has been called the Field of Blood to this day.
9
Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima;
Then what was spoken through Jeremiah the prophet was fulfilled: “They took the thirty pieces of silver, the price set on Him by the people of Israel,
10
wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.
and they gave them for the potter’s field, as the Lord had commanded me.”
11
Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, Wewe wasema.
Meanwhile Jesus stood before the governor, who questioned Him: “Are You the King of the Jews?” “You have said so,” Jesus replied.
12
Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno.
And when He was accused by the chief priests and elders, He gave no answer.
13
Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?
Then Pilate asked Him, “Do You not hear how many charges they are bringing against You?”
14
Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana.
But Jesus gave no answer, not even to a single charge, much to the governor’s amazement.
15
Basi wakati wa siku kuu, liwali desturi yake huwafungulia mkutano mfungwa mmoja waliyemtaka.
Now it was the governor’s custom at the feast to release to the crowd a prisoner of their choosing.
16
Basi palikuwa na mfungwa mashuhuri siku zile, aitwaye Baraba.
At that time they were holding a notorious prisoner named Barabbas.
17
Basi walipokutanika, Pilato akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi? Yule Baraba, au Yesu aitwaye Kristo?
So when the crowd had assembled, Pilate asked them, “Which one do you want me to release to you: Barabbas, or Jesus who is called Christ?”
18
Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda.
For he knew it was out of envy that they had handed Jesus over to him.
19
Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.
While Pilate was sitting on the judgment seat, his wife sent him this message: “Have nothing to do with that innocent man, for I have suffered terribly in a dream today because of Him.”
20
Nao wakuu wa makuhani na wazee wakawashawishi makutano ili wamtake Baraba, na kumwangamiza Yesu.
But the chief priests and elders persuaded the crowds to ask for Barabbas and to have Jesus put to death.
21
Basi liwali akajibu, akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi katika hawa wawili? Wakasema, Baraba.
“Which of the two do you want me to release to you?” asked the governor. “Barabbas,” they replied.
22
Pilato akawaambia, Basi, nimtendeje Yesu aitwaye Kristo? Wakasema wote, Asulibiwe.
“What then should I do with Jesus who is called Christ?” Pilate asked. They all answered, “Crucify Him!”
23
Akasema, Kwani? Ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, wakisema, Na asulibiwe.
“Why?” asked Pilate. “What evil has He done?” But they shouted all the louder, “Crucify Him!”
24
Basi Pilato alipoona ya kuwa hafai lo lote, bali ghasia inazidi tu, akatwaa maji, akanawa mikono yake mbele ya mkutano, akasema, Mimi sina hatia katika damu ya mtu huyu mwenye haki; yaangalieni haya ninyi wenyewe.
When Pilate saw that he was accomplishing nothing, but that instead a riot was breaking out, he took water and washed his hands before the crowd. “I am innocent of this man’s blood,” he said. “You bear the responsibility.”
25
Watu wote wakajibu wakasema, Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu.
All the people answered, “His blood be on us and on our children!”
26
Ndipo akawafungulia Baraba; na baada ya kumpiga Yesu mijeledi, akamtoa ili asulibiwe.
So Pilate released Barabbas to them. But he had Jesus flogged, and handed Him over to be crucified.
27
Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima.
Then the governor’s soldiers took Jesus into the Praetorium and gathered the whole company around Him.
28
Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu.
They stripped Him and put a scarlet robe on Him.
29
Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!
And they twisted together a crown of thorns and set it on His head. They put a staff in His right hand, knelt down before Him, and mocked Him, saying, “Hail, King of the Jews!”
30
Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani.
Then they spit on Him and took the staff and struck Him on the head repeatedly.
31
Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha.
After they had mocked Him, they removed the robe and put His own clothes back on Him. Then they led Him away to crucify Him.
32
Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake.
Along the way they found a man from Cyrene, named Simon, and they forced him to carry the cross of Jesus.
33
Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa,
And when they came to a place called Golgotha, which means The Place of the Skull,
34
wakampa kunywa divai iliyochanganyika na nyongo; lakini yeye alipoionja hakutaka kunywa.
they offered Him wine to drink, mixed with gall; but after tasting it, He refused to drink it.
35
Walipokwisha kumsulibisha, waligawa mavazi yake, wakipiga kura; [ili litimie neno lililonenwa na nabii, Waligawa nguo zangu kati yao, na juu ya vazi langu walipiga kura.]
When they had crucified Him, they divided up His garments by casting lots.
36
Wakaketi, wakamlinda huko.
And sitting down, they kept watch over Him there.
37
Wakaweka juu ya kichwa chake mashitaka yake, yaliyoandikwa HUYU NI YESU, MFALME WA WAYAHUDI.
Above His head they posted the written charge against Him: THIS IS JESUS, THE KING OF THE JEWS.
38
Wakati uo huo wanyang'anyi wawili wakasulibiwa pamoja naye, mmoja mkono wake wa kuume, na mmoja mkono wake wa kushoto.
Two robbers were crucified with Him, one on His right and the other on His left.
39
Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakitikisa-tikisa vichwa vyao, wakisema,
And those who passed by heaped abuse on Him, shaking their heads
40
Ewe mwenye kulivunja hekalu na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe nafsi yako; ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, shuka msalabani.
and saying, “You who are going to destroy the temple and rebuild it in three days, save Yourself! If You are the Son of God, come down from the cross!”
41
Kadhalika na wale wakuu wa makuhani wakamdhihaki pamoja na waandishi na wazee, wakisema, Aliokoa wengine, hawezi kujiokoa mwenyewe.
In the same way, the chief priests, scribes, and elders mocked Him, saying,
42
Yeye ni mfalme wa Israeli; na ashuke sasa msalabani, nasi tutamwamini.
“He saved others, but He cannot save Himself. He is the King of Israel! Let Him come down now from the cross, and we will believe in Him.
43
Amemtegemea Mungu; na amwokoe sasa, kama anamtaka; kwa maana alisema, Mimi ni Mwana wa Mungu.
He trusts in God. Let God deliver Him now if He wants Him. For He said, ‘I am the Son of God.’”
44
Pia wale wanyang'anyi waliosulibiwa pamoja naye walimshutumu vile vile.
In the same way, even the robbers who were crucified with Him berated Him.
45
Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa.
From the sixth hour until the ninth hour darkness came over all the land.
46
Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
About the ninth hour Jesus cried out in a loud voice, “Eli, Eli, lema sabachthani?” which means, “My God, My God, why have You forsaken Me?”
47
Na baadhi yao waliohudhuria, waliposikia, walisema, Huyu anamwita Eliya.
When some of those standing there heard this, they said, “He is calling Elijah.”
48
Mara mmoja wao akaenda mbio, akatwaa sifongo, akaijaza siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha.
One of them quickly ran and brought a sponge. He filled it with sour wine, put it on a reed, and held it up for Jesus to drink.
49
Wale wengine wakasema, Acha; na tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.
But the others said, “Leave Him alone. Let us see if Elijah comes to save Him.”
50
Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.
When Jesus had cried out again in a loud voice, He yielded up His spirit.
51
Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
At that moment the veil of the temple was torn in two from top to bottom. The earth quaked, and the rocks were split.
52
makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;
The tombs broke open, and the bodies of many saints who had fallen asleep were raised.
53
nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.
After Jesus’ resurrection, when they had come out of the tombs, they entered the holy city and appeared to many people.
54
Basi yule akida, na hao waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu, walipoliona tetemeko la nchi na mambo yaliyofanyika, wakaogopa sana, wakisema, Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.
When the centurion and those with him who were guarding Jesus saw the earthquake and all that had happened, they were terrified and said, “Truly this was the Son of God.”
55
Palikuwa na wanawake wengi pale wakitazama kwa mbali, hao ndio waliomfuata Yesu toka Galilaya, na kumtumikia.
And many women were there, watching from a distance. They had followed Jesus from Galilee to minister to Him.
56
Miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo na Yusufu, na mama yao wana wa Zebedayo.
Among them were Mary Magdalene, Mary the mother of James and Joseph, and the mother of Zebedee’s sons.
57
Hata ilipokuwa jioni akafika mtu tajiri wa Arimathaya, jina lake Yusufu, naye mwenyewe alikuwa mwanafunzi wa Yesu;
When it was evening, there came a rich man from Arimathea named Joseph, who himself was a disciple of Jesus.
58
mtu huyu alimwendea Pilato akauomba mwili wa Yesu. Ndipo Pilato akaamuru apewe.
He went to Pilate to ask for the body of Jesus, and Pilate ordered that it be given to him.
59
Yusufu akautwaa mwili, akauzonga-zonga katika sanda ya kitani safi,
So Joseph took the body, wrapped it in a clean linen cloth,
60
akauweka katika kaburi lake jipya, alilokuwa amelichonga mwambani; akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
and placed it in his own new tomb that he had cut into the rock. Then he rolled a great stone across the entrance to the tomb and went away.
61
Na pale walikuwapo Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, wameketi kulielekea kaburi.
Mary Magdalene and the other Mary were sitting there opposite the tomb.
62
Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato,
The next day, the one after Preparation Day, the chief priests and Pharisees assembled before Pilate.
63
wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka.
“Sir,” they said, “we remember that while He was alive that deceiver said, ‘After three days I will rise again.’
64
Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamwiba, na kuwaambia watu, Amefufuka katika wafu; na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza.
So give the order that the tomb be secured until the third day. Otherwise, His disciples may come and steal Him away and tell the people He has risen from the dead. And this last deception would be worse than the first.”
65
Pilato akawaambia, Mna askari; nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo.
“You have a guard,” Pilate said. “Go, make the tomb as secure as you know how.”
66
Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi.
So they went and secured the tomb by sealing the stone and posting the guard.