Upendo Nkone - Nikae Miguuni Pako Lyrics

Nikae Miguuni Pako Lyrics

Eh Bwana Yesu niko mbele zako Baba 
Ninakuomba Baba unisikie 
Nahitaji nikujue niyajue maneno yako 
Yesu sheria zako Mungu zikae ndani yangu 

Uliwaambia waisraeli wazishike sheria zako Bwana 
Kusudi baraka zako ziwe juu yao 
Unishike nisipotee nikaenda kwa njia isiyofaa 
Nikaliacha neno nikapotea 
Unilinde mguu wangu nisiuate mabaya 
Adui asinimeze nikaangamia 
Huduma yangu mimi utumishi wangu mimi 
Popote ninapohudumu nikusifu Yesu 
Kote ulikonitoa mengi umenitendea mimi 
Nisije nikasahau wema wako Mungu 

Mimi nikae miguuni pako 
Ninaomba Baba unifundishe 
Roho wa Mungu mwalimu mwema 
Ninaomba Baba unifundishe 

Utusamehe watumishi mara nyingi tumekukosea Baba 
Tunavyojiinua na tunakusahau 
Miujizi ikitendeka tunasema ni kwa nguvu zako wewe 
Tunasahau kwamba wewe umetenda 
Tunatumia madhabau kuyakuza majina yetu sisi 
Badala ya kulikuza jina lako Yesu 

Tumesahau mapatano tulikuahidi ukituinua Baba 
Tutakuinua Yesu mataifa wakujue 
Hata sisi watumishi tumeshindwa kuzifuata amri zako 
Tunatamani sana kulirekebisha neno 

Na kama ungeturusu tuweze kulirekebisha neno 
Kila mtu angejiongoza anavyotaka yeye 
Tunafanya mazingaombwe kwenye madhabau Yesu 
Tunadhani tunaweza kusaidia Mungu 

Lakini mimi nikae miguuni pako 
Ninaomba Baba unifundishe 
Roho wa Mungu mwalimu mwema 
Ninaomba Baba unifundishe 



Nikae Miguuni Pako Video

Nikae Miguuni Pako Lyrics -  Upendo Nkone

Upendo Nkone Songs

Related Songs