Upendo Nkone - Usalama Wangu Lyrics
Lyrics
Usalama wangu lazima niwe nawewe Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu Kwa kila jambo nalolifanya Kwa kazi zangu za kila siku Usalama wangu lazima niwe na Yesu
Na hata kwenye huduma yangu Majaribu yapo ni mengi Kushinda kwangu lazima niwe na Yesu Nikiwa kazini na wezangu Wakinifanyia ubaya Ushindi wangu najua niko na Yesu
Wakinisengenya chini kwa chini Wakinifanyia mabaya Mtetezi wangu najua niko na Yesu Wakinizushia maneno, wakinifanyia ubaya Mtetezi wangu najua niko na Yesu
Wakinichongea kwa boss wangu Wakitaka mimi nifukuzwe kazi Mtetezi wangu najua ni Bwana Yesu Na majaribu yakinipata Yakiniumiza moyo wangu Faraja yangu najua ni Bwana Yesu wee
Wakinitegea mitego na itawanasa wenyewe Siogopi kitu najua ninaye Yesu Wakinichimbia shimo, watatumbukia wenyewe Sitaangamia sababu ninaye Yesu
Wakikusanyana kwa ubaya Nikisingiziwa kesi Mtetezi wangu najua ni Bwana Yesu Wakienda kwa waganga, wakinifanyia uchawi Hawataniweza sababu niko naye Yesu
Ninalindwa usiku na mchana Malaika wamenizunguka Mlinzi wangu najua ni Bwana Yesu Wakiniwekea sumu, wakitaka kunimaliza Mponyaji wangu najua ni Bwana Yesu Na maneno yao siyaogopi Na vitisho vyao siviogopi Usalama wangu najua ninaye Yesu
Usalama wangu lazima niwe nawewe Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu Usalama wangu lazima niwe nawewe Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu
Usalama wangu lazima niwe nawewe Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu Usalama wangu lazima niwe nawewe Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu
Na Yesu, Na Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu Na Yesu, Na Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu
Na Yesu, Na Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu Na Yesu, Na Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu
Na Yesu, Na Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu Na Yesu, Na Yesu Usalama wangu lazima niwe na Yesu
Video
UPENDO NKONE - USALAMA WANGU (Official Gospel Video)