Upendo Nkone - Utabaki na Mimi Lyrics

Lyrics

Utabaki na mimi, utabaki na mimi Wengine wakiniacha Yesu, utabaki na mimi Utabaki na mimi, utabaki na mimi Baba Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Utabaki na mimi, utabaki na mimi Wengine wakiniacha Yesu, utabaki na mimi Utabaki na mimi, utabaki na mimi  Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Katika pito hili baba (Utabaki na mimi) Kwenye magumu haya baba (Utabaki na mimi) Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Utabaki na mimi baba (Utabaki na mimi) Uwe mfano wangu Yesu (Utabaki na mimi) Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Majaribu ni kama moto yanauchoma moyo Yamenipata mimi moyoni mwangu naumia Nimesongwa pande zote sioni nafuu Yesu njoo uwe na mimi

Kichwa changu kinaniuma moyo una mawazo Jaribu hili baba yangu naona ni nzito sana Limenijia kwa ghafla nimehuzunika sana Yesu njoo nifariji moyo

Utabaki na mimi, utabaki na mimi Wengine wakiniacha Yesu, utabaki na mimi Utabaki na mimi, utabaki na mimi  Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Utabaki na mimi, utabaki na mimi Wengine wakiniacha Yesu, utabaki na mimi Utabaki na mimi, utabaki na mimi  Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Unisimamishe tena baba (Utabaki na mimi) Nishike mkono baba (Utabaki na mimi) Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Unisimamishe tena baba (Utabaki na mimi) Nishike mkono baba (Utabaki na mimi) Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Mimi nalia machozi yangu uyaone baba Mwili wangu umetetemeka pito ni nzito Ewe Mungu wa urejesho unirejeshe tena Yesu wangu uwe na mimi

Nakuomba baba wa huruma unitulize Faraja yako Yesu wangu iwe na mimi Unishike mkono Mungu wangu uniinue tena Yesu njoo uwe na mimi 

Utabaki na mimi, utabaki na mimi Wengine wakiniacha Yesu, utabaki na mimi Utabaki na mimi, utabaki na mimi  Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Utabaki na mimi, utabaki na mimi Wengine wakiniacha Yesu, utabaki na mimi Utabaki na mimi, utabaki na mimi  Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Hata nikiwa mjane baba (Utabaki na mimi) Hata nikiwa yatima (Utabaki na mimi) Usiniache baba, usiniache baba Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Hata ndoa ikiisha (Utabaki na mimi) Hata ndoa ikiisha baba (Utabaki na mimi) Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Hata wakinitenga (Utabaki na mimi) Wakinifukuza mimi (Utabaki na mimi) Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Marafiki wakikimbia (Utabaki na mimi) Na dunia ikinitenga (Utabaki na mimi) Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Washirika wakinigeuka (Utabaki na mimi) Utabaki na mimi Baba (Utabaki na mimi) Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Watoto wangu wakinitenga (Utabaki na mimi) Yesu utabaki na mimi (Utabaki na mimi) Wengine wakiniacha Yesu utabaki na mimi

Wewe faraja ya moyo wangu Yesu mtuliza bahari

Video

Upendo Nkone - UTABAKI NA MIMI (official video )

Thumbnail for Utabaki na Mimi video
Loading...
In Queue
View Lyrics