Japhet Zabron - Napungukiwa Nini Lyrics

Album: Nikumbuke
Released: 19 Mar 2022
iTunes Amazon Music

Lyrics

Ndege, hawavuni
Hawapandi wala hawafanyi kitu
Mihangaiko, ya dunia sahau wala hawasumbukii
Sauti tulivu
Asabuhi huimba nakushukuru
Wanamjua awapae kuishi kamwe hawahofu kitu
Heeh’ ndivyo aishivyo amtumainie, muumba wa mbingu
Hahangaiki hahofii dunia na masumbuko yajayo

Napungukiwa nini, Napungukiwa nini
Nikiwa naye Yesu
Sina kiu ya kitu
Napungukiwa nini, Napungukiwa nini
Nikiwa naye Yesu
Sina kiu ya kitu

Huna tumaini
Umekwama na kesho inakutisha
Hufika muda
Peke yako, njiani waongea na kulia
Maisha mzigo
Umetengwa wapendwa kukukimbia
Nikukumbushe
Yupo Yesu rafiki hata usiwaze kitu
He he, ndivyo aishivyo
Amtumainie muumba wa mbingu
Hahangaikii hahofii dunia na masumbuko yajayo

Napungukiwa nini (nakosa nini)
Napungukiwa nini (zaidi nini Baba)
Nikiwa naye Yesu
Sina kiu ya kitu
Napungukiwa nini, Napungukiwa nini
Nikiwa naye Yesu
Sina kiu ya kitu

Mungu yupo upande wetu
Nani atakae kaa juu yetu
Tulia, tulia, tuliaa kwa Yesu

Video

Napungukiwa Nini by Japhet Zabron

Thumbnail for Napungukiwa Nini video
Loading...
In Queue
View Lyrics