1
Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza,
When Jesus realized that the Pharisees were aware He was gaining and baptizing more disciples than John
2
(lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake,)
(although it was not Jesus who baptized, but His disciples),
3
aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya.
He left Judea and returned to Galilee.
4
Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.
Now He had to pass through Samaria.
5
Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.
So He came to a town of Samaria called Sychar, near the plot of ground that Jacob had given to his son Joseph.
6
Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.
Since Jacob’s well was there, Jesus, weary from His journey, sat down by the well. It was about the sixth hour.
7
Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.
When a Samaritan woman came to draw water, Jesus said to her, “Give Me a drink.”
8
Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.
(His disciples had gone into the town to buy food.)
9
Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)
“You are a Jew,” said the woman. “How can You ask for a drink from me, a Samaritan woman?” (For Jews do not associate with Samaritans.)
10
Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai.
Jesus answered, “If you knew the gift of God and who is asking you for a drink, you would have asked Him, and He would have given you living water.”
11
Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai?
“Sir,” the woman replied, “You have nothing to draw with and the well is deep. Where then will You get this living water?
12
Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?
Are You greater than our father Jacob, who gave us this well and drank from it himself, as did his sons and his livestock?”
13
Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
Jesus said to her, “Everyone who drinks this water will be thirsty again.
14
walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
But whoever drinks the water I give him will never thirst. Indeed, the water I give him will become in him a fount of water springing up to eternal life.”
15
Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.
The woman said to Him, “Sir, give me this water so that I will not get thirsty and have to keep coming here to draw water.”
16
Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa.
Jesus told her, “Go, call your husband and come back.”
17
Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume;
“I have no husband,” the woman replied. Jesus said to her, “You are correct to say that you have no husband.
18
kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli.
In fact, you have had five husbands, and the man you now have is not your husband. You have spoken truthfully.”
19
Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!
“Sir,” the woman said, “I see that You are a prophet.
20
Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.
Our fathers worshiped on this mountain, but you Jews say that the place where one must worship is in Jerusalem.”
21
Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.
“Believe Me, woman,” Jesus replied, “a time is coming when you will worship the Father neither on this mountain nor in Jerusalem.
22
Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.
You worship what you do not know; we worship what we do know, for salvation is from the Jews.
23
Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.
But a time is coming and has now come when the true worshipers will worship the Father in spirit and in truth, for the Father is seeking such as these to worship Him.
24
Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
God is Spirit, and His worshipers must worship Him in spirit and in truth.”
25
Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.
The woman said, “I know that Messiah” (called Christ) “is coming. When He comes, He will explain everything to us.”
26
Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye.
Jesus answered, “I who speak to you am He.”
27
Mara hiyo wakaja wanafunzi wake, wakastaajabu kwa sababu alikuwa akisema na mwanamke; lakini hakuna aliyesema, Unatafuta nini? Au, Mbona unasema naye?
Just then His disciples returned and were surprised that He was speaking with a woman. But no one asked Him, “What do You want from her?” or “Why are You talking with her?”
28
Basi yule mwanamke akauacha mtungi wake, akaenda zake mjini, akawaambia watu,
Then the woman left her water jar, went back into the town, and said to the people,
29
Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo?
“Come, see a man who told me everything I ever did. Could this be the Christ?”
30
Basi wakatoka mjini, wakamwendea.
So they left the town and made their way toward Jesus.
31
Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.
Meanwhile the disciples urged Him, “Rabbi, eat something.”
32
Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.
But He told them, “I have food to eat that you know nothing about.”
33
Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?
So the disciples asked one another, “Could someone have brought Him food?”
34
Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.
Jesus explained, “My food is to do the will of Him who sent Me and to finish His work.
35
Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.
Do you not say, ‘There are still four months until the harvest’? I tell you, lift up your eyes and look at the fields, for they are ripe for harvest.
36
Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja.
Already the reaper draws his wages and gathers a crop for eternal life, so that the sower and the reaper may rejoice together.
37
Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine.
For in this case the saying ‘One sows and another reaps’ is true.
38
Mimi naliwatuma myavune yale msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao.
I sent you to reap what you have not worked for; others have done the hard work, and now you have taken up their labor.”
39
Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya neno la yule mwanamke, aliyeshuhudia kwamba, Aliniambia mambo yote niliyoyatenda.
Many of the Samaritans from that town believed in Jesus because of the woman’s testimony, “He told me everything I ever did.”
40
Basi wale Wasamaria walipomwendea, walimsihi akae kwao; naye akakaa huko siku mbili.
So when the Samaritans came to Him, they asked Him to stay with them, and He stayed two days.
41
Watu wengi zaidi wakaamini kwa sababu ya neno lake.
And many more believed because of His message.
42
Wakamwambia yule mwanamke, Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu; maana sisi tumesikia wenyewe, tena twajua ya kuwa hakika huyu ndiye Mwokozi wa ulimwengu.
They said to the woman, “We now believe not only because of your words; we have heard for ourselves, and we know that this man truly is the Savior of the world.”
43
Na baada ya siku mbili hizo akaondoka huko, akaenda Galilaya.
After two days, Jesus left for Galilee.
44
Kwa maana Yesu mwenyewe alishuhudia ya kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.
Now He Himself had testified that a prophet has no honor in his own hometown.
45
Basi alipotoka Galilaya, Wagalilaya walimpokea; kwa kuwa wameyaona mambo yote aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu; maana hao nao waliiendea sikukuu.
Yet when He arrived, the Galileans welcomed Him. They had seen all the great things He had done in Jerusalem at the feast, for they had gone there as well.
46
Basi alifika tena Kana ya Galilaya, hapo alipoyafanya yale maji kuwa divai. Na palikuwa na diwani mmoja ambaye mwanawe hawezi huko Kapernaumu.
So once again He came to Cana in Galilee, where He had turned the water into wine. And there was a royal official whose son lay sick at Capernaum.
47
Huyo aliposikia ya kwamba Yesu amekuja kutoka Uyahudi mpaka Galilaya, alimwendea, akamsihi ashuke na kumponya mwanawe; kwa maana alikuwa kufani.
When he heard that Jesus had come from Judea to Galilee, he went and begged Him to come down and heal his son, who was about to die.
48
Basi Yesu akamwambia, Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa?
Jesus said to him, “Unless you people see signs and wonders, you will never believe.”
49
Yule diwani akamwambia, Bwana, ushuke asijakufa mtoto wangu.
“Sir,” the official said, “come down before my child dies.”
50
Yesu akamwambia, Enenda; mwanao yu hai. Mtu yule akalisadiki lile neno aliloambiwa na Yesu, naye akashika njia.
“Go,” said Jesus. “Your son will live.” The man took Jesus at His word and departed.
51
Hata alipokuwa akishuka, watumwa wake walimlaki, wakisema ya kwamba mtoto wake yu hai.
And while he was still on the way, his servants met him with the news that his boy was alive.
52
Basi akawauliza habari ya saa alipoanza kuwa hajambo; nao wakamwambia, Jana, saa saba, homa ilimwacha.
So he inquired as to the hour when his son had recovered, and they told him, “The fever left him yesterday at the seventh hour.”
53
Basi babaye akafahamu ya kuwa ni saa ile ile aliyoambiwa na Yesu, Mwanao yu hai. Akaamini yeye na wote wa nyumbani mwake.
Then the father realized that this was the very hour in which Jesus had told him, “Your son will live.” And he and all his household believed.
54
Hiyo ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu, alipokuwa ametoka Uyahudi kufika Galilaya.
This was now the second sign that Jesus performed after coming from Judea into Galilee.